Skip to main content

HANUNA IBRAHIM: KUTOKA SEKRETARI HADI DC. ALIMBWAGA WAZIRI AKAUKWAA UWAKILISHI CHAKECHAKE

 

 


NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@

KATIKATI ya giza nene lililogubika haki ya mwanamke kuwa kiongozi kwa wakati huo, kuna mwanamke alielishinda?.

Alisimama kidedea, yeye na waliomzunguka walihakikisha anafanikiwa na kweli alishika nafasi mbalimbali za uongozi, mpaka kuwa mmoja wa viongozi wanawake walioweka alama isiyofutika katika jamii.

Ni Hanuna Ibrahim Massoud, alieanza kuliona jua mwaka 1959, Kisiwani kwa Binti Abedi wilaya ya Wete kaskazini Pemba.

Alianza kusaka elimu yake ya msingi, mwaka 1965, ambapo aliipata katika skuli tofauti kama Ziwani, Shamiani na Utaani.

Mnamo mwaka 1974, alikamilisha elimu yake ya sekondari kidato cha nne, katika skuli ya Fidel Castro.

“Safari yangu ya masomo haikuwa na kituo kimoja, nilisoma maeneo mengi, lakini huku kulinifanya kuyajuwa na kuyatawala vizuri mazingira,’’anahadithia.

Kumbe wakati huo kuelimika kwa mtoto wa kike hadi kidato cha nne, ilikuwa fursa adimu na nimsingi mkubwa wa ukombozi.

Safari yake ya kutafuta elimu, ikaendelea hadi  miaka ya 1970, alipopata nafasi ya kujiendeleza kimasomoni Mkoani Moshi kwa miezi tisa, ambako alijifunza mafunzo ya uongozi.

Anakiri mafunzo hayo, yalimpa msingi wa uongozi na utawala, usimamizi wa rasilimali watu, na mbinu za kushughulikia kero za wananchi.

Maana mwaka 1987, uwezo wake wa kufanya kazi, uaminifu na uzalendo ukasababisha kuchaguliwa, kuchukuwa kozi ya sayansi ya jamii nchini Urusi.

HANUNA KATIKA UWANJA WA SIASA

Hanuna Ibrahim Massoud, aliwahi kuwa mwanasiasa mwenye ushawishi mkubwa.

Mbio zake za kisiasa, zilianzia mapema skulini akiwa ni mwanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM), aliejiunga na ‘Young Paunia’ (Chipukizi kwa sasa), ambako alishika nafasi mbalimbali, kama Mwenyekiti.

Kisha baada ya kumaliza kidato cha nne, alianza kujihusisha na shughuli za Umoja wa vijana (UVCCM), katika chama chake cha Mapinduzi.

Wakati akiwa huko, alishika nafasi mbalimbali za uongozi katika jumuiya za chama, kama Mjumbe wa Jumuiya ya Wazazi wa tawi lake la Kichungwani na Mjumbe wa UWT tawi hilo.



Nafasi nyengine ni Katibu wa Wazazi katika Tawi la Kichungwani, pia alikuwa Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Vijana na wanawake tawini humo.

“Kwamara ya kwanza kwenye siasa, nilikuwa mwenyekiti wa ‘Young Paunia’ wa skulini, nilipomaliza na kujiunga katika jumuiya ya vijana,’’anakumbukia.

Anasema hapo ndipo akawa anashika nafasi kama ujumbe UWT, Mjumbe wa kamati tekelezaji ya vijana na wanawake tawini.

Losha Hanuna, alichaguliwa kuwa Katibu wa Vijana Wilaya ya Wete, nafasi alioipata baada ya ushindani mkubwa, uliokuwepo baina yake na wanachama wingine ambao wengi walikua wanaume.

Anasema miaka yote hayo, ilikuwa ni kama maandalizi yake, katika kumjengea ujasiri na ukakamavu wa kuwa kiongozi, katika duru za kisiasa.

Safari yake, iliiva rasmi 1990, wakati siasa za Zanzibar zikiwa katika mfumo wa Chama kimoja, ambapo aligombea nafasi ya Uwakilishi Jimbo la Chake Chake.

Maana kwa wakati huo, CCM Chake Chake ilisimamisha wagombea wawili, ambao ni yeye na mwenzake Abdallah Said Haji, aliekuwa na ushawishi na umaarufu mkubwa.

Mwenzake huyo ambae kwa sasa ni marehemu, wakati anasimama jukwaani kuomba ridhaa za wananchi, alikuwa ni Waziri wa Kilimo Zanzibar.

Tena jambo lililomfanya kushindwa kujiamini katika kinyang’anyiro, hicho hasa kwa umaarufu wa mwenzake wake kwenye siasa.

“Mwaka 1990 nilikuwa Ofisini kwangu, akaja dadaangu Ashura Abeid (marehemu), akaniambia nikachukuwe fomu ya kugombea wa Uwakilishi, na Abdallah utamshinda, sikuwa tayari kwa hilo,’’anafafanua.

Anahadithia mchuano huo, ulikuwa wa kihistoria, kwani alimshinda mgombea mwenza aliekuwa Waziri wa Kilimo, kwa wakati huo kwa kura zaidi ya 100 kutoka kwa wananchi.

Anasema jambo hilo, liliwashangaza wengi, kuanzia familia yake, jamii, chama chake na hata yeye mwenyewe, kwani ilikuwa kama “Ngamia kupita katika tundu ya sindano”,

Kampeni zake, ziligubikwa na maneno kama “maajabu mwanamke kugombania”, “wanawake wakae wapike tu” huku wengine wakienda mbali zaidi kwa kusema “na apoteze muda bure, mwanamke hawi kiongozi”.



Hanuna anaeleza, aliitumikia nafasi ya Uwakilishi wa jimbo la chake chake kwa mitano hadi, ulipokuja mfumo wa vyama vingi.

Mwenyewe anaeleza “uchaguzi wa mwanzo wa vyama vingi wananchi waliniambia nigombee na tuko pamoja na wewe, isipokuwa mara hii chama chako kiwe CUF, sikuweza kuiacha CCM.

MCHANGO WAKE KATIKA JAMII

Mkaazi wa Chake Chake Mohamed Ali Mohamed anaeleza, baada ya kuingia katika baraza la Wawakilishi Hanuna, alielekeza nguvu zake, katika kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi.

“……hee!! Hanuna alituziba midomo, zile zana za mwanamke hawezi ziliishia pale, alikuwa Mwakilishi mzuri wa wananchi, alipita kusikiliza kero zetu na alizifanyia kazi”, anahadithia.

Anasema Hanuna, akiwa Mwakilishi ndie aliepigania ujenzi na ukarabati wa madarasa katika skuli ya Pondeani na Michakaini msingi kwa wakati huo.

Salma Ali wa Shungi, anasema Hanuna alipokuwa Mwakilishi wao, alipambania ujenzi wa kituo cha Afya Shungi, kwa kuomba ufadhili wa vifaa kama bati na saruji.

“Tulikuwa na changamoto ya kituo cha afya, Hanuna alipopata Uwakilishi, alitafuta wafadhili, mpaka ujenzi ukakamilika na hadi sasa kinatumika” anaeleza.

Said Kheir Said mkaazi wa Pondeani anasema, akiwa Mwakilishi mwanamke huyo, aliwatatulia changamoto ya ubovu wa daraja la Pondeani na lile la Bandataka, ili kurahisisha usafiri.

BAADA YA HAPO

Kutokana na uzoefu wake katika utawala usiyotikisika, mwaka 1996, Hanuna aliteuliwa kuwa Afisa Tawala wilaya ya Chake Chake nafasi aliodumu nayo hadi 2002.

Ambapo Rais Amani Abeid Karume, alimteua kuwa Afisa Tawala na baadae kuwa Mkuu wa wilaya ya Chake Chake.

Hadi 2017, akateuliwa kuwa Msaidizi wa Rais kisiwani Pemba, akijikita katika kuhudumia jamii na kusikiliza kero za wanachi.

Katika mwaka huo huo, aliteuliwa kuwa Afisa Mdhamini wa Tume ya Maadili Pemba, nafasi aliyoihudumu nayo, mpaka alipostaafu mwaka 2019, akiwa afisa mdhamini wa mwanzo wa tume hiyo.

Hanuna baada ya kustaafu, mwaka 2020 alihudumu kama Mkuu wa Utawala wa Chuo cha Mwalimu Nyerere Tawi la Pemba, na baadae sheria ilipobadilika, alihudumu kama Afisa Utumishi wa Chuo hicho.

KABLA YA SIASA

Ajira yake ya mwanzo, ni katika Wizara ya Biashara alikuwa anafanyakazi kama Karani wa Fedha, pia aliwahi kufanya kazi Ikulu ya Wete Pemba  kama msimamizi.

Mtumwa Ali Khalifa ni miongoni mwa watu waliofanyakazi kwa karibu na Hanuna anasema, utendaji wake ni kizalendo, ujasiri na kupenda wenzake.

 

Aidha aliwahi kuhudumu kama Mpiga Chapa wa katibu wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar, pia Katibu Muhtasi wa wilaya ya Chake Chake na Katibu Muhtasi wa Mkuu wa mkoa wa Kusini Pemba.

Hanuna Masoud “Bihanuna” kama wanavyopenda kuitawatu wengi, ni mama wa familia wa watoto sita.

Anakiri mwanamke kuwa kiongozi, haibadilishi lolote juu ya wajibu wa kuitumikia familia yake, anawasihi wanawake viongozi kujituma, kuwajibika na kujiheshimu.

Anawasihi wanaume kuiga mfano wa mumewake, katika kuwaunga mkono wanawake, kushiriki katika uongozi.

Mumewe wake Hanuna, Abuu-bakar Mohamed Ali anasema anamuona mkewe ni kielelezo cha mwanamke shujaa, aliyetumia ujana na utu uzima wake wote, kutumikia wananchi.

Bali haya hayakuja hivihivi, isipokuwa kwa juhudi za serikali na wadau wengine wa kupambania haki za wanawake.

Mfano serikali ikaridhia Mkataba wa umoja wa Mataifa wa kutokomeza aina zote za udhalilishaji (CEDAW) wa 1979, wenye ibara ya 7 inayoeleza inagusia hilo,

“Nchi wanachama zihakikishe zinawapa wanawake fursa za kushiriki katika uongozi,’’ infafanua ibara hiyo.



Lengo Namba 5.5 la maendeleo endelevu (SDGs,2015/2030), lililozitaka nchi zote kuhakikisha, ushiriki kamili na waufanisi wa wanawake na fursa sawa za uongozi, katika ngazi zote, iwe kisiasa na kiuchumi.

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, ibara yake ya 21 (1) inayoeleza kila Mzanzibari anayo haki ya kushiriki, katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia Wawakilishi waliochaguliwa kwa hiari.

Hadi sasa TAMWA –Zanzibar wakiwa ni wadau wa kuhamasisha na kutetea haki za wanawake, katika kupata fursa za uongozi, wamekua wakiwapa mafunzo yakujitambua na kupambania haki zao.



Aidha TAMWA-Zanzibar wamekua wakitoa mafunzo kwa waandishi wa habari, ili waweze kuandika habari zitakazoshajihisha wanawake kuingia katika uongozi.

MWISHO

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...