Skip to main content

Posts

Showing posts from July 21, 2024

BONANZA LA MAZOEZI PEMBA: MAKAMU WA KWANZA ATOA RAI KUNDOA DHANA POTOFU MICHEZONI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAKAMU wa Kwanza wa Rais Zanzibar Othman Massoud Othman, amevishauri vilabu ya mazoezi nchini, kujitengenezea kanuni, zitakazowavutia watu wingi zaidi kujiunga kwenye mazoezi, ili kuondoa dhama potofu ya mazoezi ni uhuni. Alisema, kama kundi kubwa la watu wanadhana kuwa mazoezi ni uhuni na kuvunja maadili, ni wakati sasa kwa vilabu vya mazoezi na michezo, kuwa na kanuni zitakazofuta dhana hiyo. Makamu huyo wa Kwanza, aliyasema hayo leo Julai 28, 2024 uwanja wa michezo Gombani Chake chake, kwenye bonanza la miaka 10, tokea kuanzishwa kwa ‘Gombani Fitness Club’ lilioandaliwa kwa pamoja na TAMWA-Zanzibar na Shirika la Bima. Alieleza kuwa, kwa vile mozoezi ni jambo muhimu kwa kila mmoja, ni vyema kuwepo na kanuni ndogo ndogo, ambazo zitawavutia wengine, kushiriki katika kupata kinga ya miili yao. Alifahamisha kuwa, ni kweli kama kuna viashiria vya uvunjifu wa maadili, inaweza kuwa sababu kwa baadhi ya watu, kuona sio sehemu salama, ingawa zikiwepo

IDARA YA KATIBA: ''WANAWAKE MSIOGOPE TALAKA TOWENI USHAHIDI MAHKAMANI'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ IDARA ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, imewataka wanawake wa Junguni wilaya ya Wete, kutoacha kuzisimamia kasi za udhalilishaji hata kama mtendaji ni muume wake, kwa hofu ya kutishiwa talaka. Kauli hiyo imetolewa leo Julai 25, 2024 na Afisa sheria kutoka Idara hiyo Ali Haji Hassan, wakati akizungumza na wananchi wa shehia ya Junguni wilaya ya Wete, kwenye muendelezo wa mikutano ya wazi, ya kuihamasisha jamii, kutoa ushahidi na kuziripoti za kesi za udhalilishaji, ulioandaliwa kwa ushirikiano na Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar. Alisema, kama muume amebainika kwa kosa ubakaji, mwanamke lazima ashirikiane na vyombo vya sheria na kuondoa hofu ya talaka, ikiwa ni njia moja wapo ya kutokomeza matendo hayo. ‘’Hakuna hatia pasi na mwananchi kufika mahkamani kutoa ushahidi, sasa niwaombe wanandoa, wasiogope kuachika na wasimamie haki ya mtoto mahkamani,’’alishauri. Katika hatua nyingine, Afisa huyo sheria, alisema bado jamii haijakuwa tay

DODO PUJINI WATOA RAI KUMALIZA UDHALILISHAJI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa shehia ya Dodo wilaya ya Mkoani Pemba, wamesema njia moja ya kupunguza matendo ya udhalilishaji ndani ya jamii, ni wakati sasa kwa sheria kubadilishwa, ili mwanamke naye aliyechangia kutokea kwa tendo hilo, atiwe hatiani. Walisema, wapo wanawake wameshasababisha kufungwa kwa wanaume wengi, nae akiendelea na shughuli zake mtaani, jambo ambalo linaweza kuwapoteza wanaume hapo baadae. Wananchi hao, waliyasema hayo leo Juni 24, 2024 Dodo Pujini, wakati wa mkutano, ulioandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, kwa kushirikiana na Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka, kwa ufadhili wa ‘UNDP’ kupitia mradi wake wa upatikanaji haki Zanzibar. Walisema, bado makosa ya ubakaji yanawaelekea wanaume pekee, hata kama mwanamke mwenye umri unaopindukia miaka 18, nae alichangia kwa njia moja ama nyingine. Haji Shaibu Hamad miaka (70), alisema ubakaji ambao uko wazi ni ule wa mwanamme kumtumia nguvu mwanamke, lakini ule wa kuridhiana ni vyema sher