SIKU YA WANAWAKE DUNIANI, KILIO, KIGUGUMIZI KWA WANAWAKE WENYE ULEMAVU NA UONGOZI, KATIJA AELEZEA MAGUMU
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WIKI iliyopita, ilikuwa ni siku ya wanawake duani kote. Kwao na jamii, siku ya kimataifa, yenye lengo la kuchanbua matamu na mchungu wanayoyapitia katika maisha yao. Wanawake, ni jamii na jamii ni wanawake, hivyo kila nyanja na ukumbi nao wapo, maana ni binaadamu. Iwenye kwenye uongozi, uchumi, ajira, siasa, uongozi, utamaduni na udumishaji amani na utulivu. Hapa ni Kiuyu Wete, mbele yangu namuoba mjasiriamali, kwa aina ya mwendo wake ambao sio wa kawaida, bila shaka ni mtu mwenye ulemavu wa viungo. Niliharakia, kutaka kumjua ni nani, nilipomkaribia ana nadisha haya…kangaa…kangaaa…na wale wa wapenzi wa madira na vipodozi nipo njooo ujichagulie. Kauli hizo, zilinifanya nisimame pembeni kidogo, mwa nyumba ya Asha Haji Makame, nae mjasiriamali huyo, aligeuka nyuma ghafla, kwa kule kutafuta wateja na alinifuata. …..assalama alyekum, baada ya kuitikia mjasiriamali huyo, alimuuliz...