NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@ MATAIFA kadhaa ulimwengini, Tanzania ikiwemo zimeridhia mikataba na matamko ya usawa wa kijinsia na uwezeshaji wanawake kwenye uongozi. Hii ni kama ilielezwa katika tamko maarufu la la Haki za Binadamu la mwaka 1948. Zanzibar imesaini mikataba ya kikanda na kimataifa, lakini safari ya utekelezaji ni ndefu kwa sababu hadhi sawa kwa wanawake na wanaunme katika uongoz. Mara nyingi unapofanyika uteuzi nafasi wanazopewa wanawake huwa hazina hadhi sawa na zile wanazokabidhiwa wanaume. Vyama vya siasa navyo vinawaacha nyuma wanawake katika kuwapa nafasi za kugombea kama, inavofanyika kwa wanaume na jina la mwanamke likipita huwa kama bahati mbaya. Taarifa ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC, inafafanua kuwa, kwa uchaguzi wa 2020, wanaume walioteuliwa na vyama kugombea kuingia katika Baraza la Wawakilishi walikua 190 na walioshinda ni 42 wakati wanawake walikuwa 61 na walioshinda ni wanane (...