NA MWANDISHI MAALUM, ZANZIBAR@@@@ AFISA Uchunguzi kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) Ofisi ya Zanzibar, Abdul-latif Ali Sheha amewasihi wazazi na walezi wa Shehiya ya Kinuni, kujenga utamaduni wa kuzilinda na kuziishi haki za watoto kwa vitendo. Abdullatif alitoa nasaha hizo kwa wazazi na walezi 637 katika Madrasatul Thamaraatul Jannah iliyopo Shehia ya Kinuni, Mkoa wa Mjini Magharibi wakati akiwapa hao elimu ya haki za watoto na wajibu wa jamii katika kuzuia vitendo vya ukatili wa watoto na uvunjwaji wa haki za binadamu ikiwa ni mwendelezo wa kutoa elimu na msaada wa sheria wakati wa mwendelezo wa zoezi la Kampeni ya Msaada wa Kisheria wa Mama Samia Awamu ya Pili (MSLAC II) unaoendelea katika Wilaya tatu za Mkoa wa Mjini Magharibi. “Mtoto ana haki ya kuishi katika mazingira salama, kupatiwa elimu na kulindwa dhidi ya aina zote za unyanyasaji" Alisisitiza bw. Abdullatif. Pia aliwaeleza wazazi hao kuwa jamii inapaswa kuachana na tabia ya kuoneana muhali ...