NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MKUU wa mkoa wa kusini Pemba Rashid Hadid Rashid, amesema jumuiya ya kitaifa ya wafanyabiashara Zanzibar ‘ZNCC’ imekuwa chanzo kikuu cha kuwaonesha njia za kujiajiri vijana, kutokana na juhudi zake mbalimbali. Mkuu huyo wa mkoa, aliyasema hayo leo Julai 11, 2026 ukumbi wa Kiwanja cha kufurahishia watoto Tibirinzi Chake chake, kwenye hafla ya kukabidhi ruzuku kwa wajasiriamali, kupitia mradi wa ‘ Inclucities’ , unoaendeshwa kwa pamoja na jumuiya hiyo na Trias na Enabel kama mtekelezaji mkuu. Alisema ZNCC, imekuwa ikihangaika huku na kule, ili kuhakikisha wajasiriamali, wanaendelea kujiajiri wakiwa na uhakika wa uwezeshaji, kama mfano wa ruzuku kama hizo zilizotolewa. Alifahamisha kuwa, kwa ZNCC kufanya hivyo, ndio maono ya serikali iliyomadarakani, kuhakikisha wajasiriamali wanawezeshwa kwa njia tofauti. ‘’Kwanza niwapongeze sana wenzetu wa ZNCC kwa kushirikiana na Trias na Enabel, ambapo leo tunashuhudia utoaji wa ruzuku, kwa wajasiriamali wetu,...