Skip to main content

Posts

Showing posts from June 9, 2024

WAALIMU WA SKULI PEMBA WAPIGWA MSASA MRADI WA ‘ECO-SCHOOLS’

  NA ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@    WAALIMU wa skuli kisiwani Pemba, wametakiwa kujenga ushirikiano wa pamoja katika kuwaelimisha wanafunzi, juu ya kupata uwelewa wa mradi wa ‘Eco-Schools’ na kuingiza katika mitaala yao ya kimasomo, ili kupata elimu ya utunzaji wa mazingira.     Hayo yameelezwa na Meneja wa Mradi wa ‘Eco-Schools’ Talib Kassim Abdi kwenye mafunzo ya utunzaji wa mazingira, kwa walimu hao, waliomo katika mradi huo, yaliyofanyika ukumbi wa TASAF Chake chake Pemba.    Alisema, ipo haja kwa waalimu hao kuyatumia mafunzo hayo, yatokanayo na mradi huo, kwani yatawajengea uwelewa, wakati wa kuwafundisha wanafunzi, mada zinazo za utunzaji na athari za kimazingira zitokanazo na mabadiliko tabia nchi.    Mapema akifungua mafunzo hayo ya siku mbili, Afisa Elimu na Mafunzo ya Amali Mkoa wa kusini Pemba, Mohamed Shamte Omar, alisema utekelezaji wa mpango huo, ni fursa kwa wanafunzi kuzipatia ufumbuzi changamoto za kimazingira zilizopo, katika maeneo wanayojifunzia. Aidh

RC KUSINI PEMBA, AWAPA DARSA WATENDAJI WA BANDARI MKOANI

    ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@  MKUU wa Mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, amewataka watendaji wa bandari ya Mkoani kisiwani humo, kufuata na miongozo iliyowekwa, ili kutoa huduma bora kwa wananchi wanaotumia bandari hiyo.   Aliyasema hayo wakati alipokua na ziara ya kutembelea taasisi mbalimbali pamoja na Mamlaka ya Bandari na kuelezea changamoto ambazo zinajitokeza, katika bandari ya Mkoani kisiwani Pemba.   Alisema kua madhumuni makubwa ya ziara hiyo nikuangalia utendaji wa bandari ya Mkoani, jinsi inavyo fanya kazi na kuangalia changamoto za wananchi na kuona namna gani wataweza kuzitatua.   "Tumepata nafasi ya kuzungumza na taasisi mbali mbali zinazofanya kazi bandarini hapa na tumekubaliana mambo ya msingi, namna ya kurekebisha changamoto hizi na nmna yakuahudumia vizuri wananchi,"aliesema.   Hata hivyo, aliwaomba wanachi kutumia bandari hiyo kwa kufuata taratibu na sheria, ambazo wanaelekezwa na uongozi, ili kuhakikisha wanapata usafiri wa uhakik

'WORLD VEGETABLE CENTER ' ’ ZEEA WASUKA MPANGO KWA WAJASIRIAMALI

    NA ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@   MRADI wa ‘world vegetable center’ kwa kushirikiana  na wakala wa uwezesha wananchi kiuchumi (ZEEA),  wameweka mpango mkakati wa kuwapa taaluma wajasiramali wadogo, kwa lengo la kuhakikisha wanapata soko la bidhaa zao ndani nan je ya Pemba.   Aliyasema hayo Mtaalamu wa kilimo cha mbogamboga Renatha Edgar, kutoka mradi huo,   kwenye kiwanda cha usindikaji cha wajasiriamali kilichoko Pujini Wilaya ya Chake chake, mara baada ya kukagua na kufanya tathmini, kwa wajasiriamali ambao wamepatiwa mafunzo ya kuzalisha na kusarifu mchicha lishe.   Alisema, lengo la kutoa taaluma kwa wajasiriamali hao ni kuweza kujipatia fursa mbali mbali, ambazo zitawaongezea thamani ya bidhaa zao, na kupata soko ambalo, litawaongezea kipato.   “Kwa sasa tumepiga hatua kwa kufanya mafunzo kwa wajasiriamali zaidi ya 200, ambao kati yao wameshaanza kufanya hii kazi, ya kuongeza thamani za bidhaa zao kwa kutengeneza unga wa mchicha lishe,’’alifafanuwa.   Hata hivyo

WASIADIZI WA SHERIA, SHEHA WAWI WAFUMUA MIPANGO KUOZESHWA MWANAFUNZI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ UONGOZI wa shehia ya Wawi, wasaidizi wa sheria na askari wa shehia hiyo, wametiribua mpango unaosukwa na familia, ya kijiji cha Vikutani shehiani humo, wa kutaka kumuozesha mtoto wao, anaesoma darasa la saba, ambae anadaiwa kuwa na ujuzito. Kwa mujibu wa taarifa kutoka shehiani humo, iliyopatikana Juni 11, 2024 familia hiyo baada ya kupewa taarifa na wasamaria wema, juu ya mabadiliko ya mtoto wao, waliamua kumfikisha hospitali kumfanyia vipimo. Ilielezwa kuwa, baada familia kugundua kuwa mtoto wao anaujauzito unaokisiwa wa miezi sita, waliamua kumfuatilia kijana anaesadikiwa kuwa amempa ujauzito huo, ili kumfungisha ndoa. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, sheha wa shehia ya Wawi Sharifa Waziri Abdalla, alisema baada ya kugundua mpango huo, sasa wameshaifuata familia hiyo, na kuitahadharisha juu ya uamuzi wao huo. Alieleza kuwa, kwa sasa wamekuwa karibu mno kumfuatilia mtoto huyo, ili kuhakikisha kwanza anarejshwa skuli, kuendelea na maso

WAWI STAR YAITEMBEZEA BAKORA 3 FFC

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@ MICHUANO ya soka ya ligi daraja la kwanza kanda ya Pemba, imendelea tena jana, kwa timu ya Wawi star, kuwafariji washabiki wake, baada ya kuiadabisha timu ya Fufuni Sports Club ‘FFC’ kwa mabao 3-0. Mchezo huo uliohudhuria na washabiki wengi kiasi, ulipigwa uwanja wa Ngere ngere Jeshini, majira ya saa 10:30 jioni, huku kila timu ikisaka alama tatu muhimu, katika michuano hiyo. Wawi star, ilishuka dimbani humo ikiwa na njaa la alama, baada ya mchezo uliopita, kutandikwa mabao 2-0 na timu ya Mila, huku FFC ikiwa na kumbu kumbu ya kushinda, mchezo uliopita mbele ya Mgogoni star. Wawi star, ambayo ilionekana na hamu ya ushindi, nusura dakika 29, ilijipatie bao la kuongoza, baada ya kutokezea piga nikupige langoni mwa FFC, na kisha shuti la nahoza wao Azhar Mbarouk, kuokolewa na mlinda mlango. FFC, walijibu shambulizi hilo dakika nne baadae, baada ya mpira aliounza mlinda mlango wao na kumfikia mshambuliaji Habib Said, nae kugawa pasi kwa Yassiri Seif,