Skip to main content

Posts

Showing posts from October 12, 2025

KAMPENI ZA KISIASA MAJI MTUNGINI, WALIO NJE YA PEMBA HAWAAMINI MASIKIO YAO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ACHA kufukua makaburi, kujua yaliopita kwa siasa za Pemba.   Maana chaguzi sita za vyama vingi, zilizokwishapita, ukiamua kufuakua makaburi, wapo watakolia, watakaofuta machozi na wingine kupoteza fahamu.   Acha kabisa, kuuliza, kufungua ripoti, kusaka takwimu, kuingia kwenye mitandao ya kijamii au kusililiza rikodi, za maovu yaliopita.   Wewe jua tu, kuwa taifa la Tanzania tokea pale lilipofanya uchaguzi wa kwanza mwaka 1995, sasa linaingia uchaguzi mkuu wa saba Oktoba 29, mwaka huu.   Narejea tena, acha kabisa kutaka kujua siasa za Pemba, jinsi zilivyokuwa na nguvu hadi kupindukia mipaka, tena ndani miezi kama hii ya kmapeni. SIASA ZA MWAKA HUU ZINATOFAUTI GANI? Juzi nilishuhudia siasa za kiungwana, kistaarabu na za kisheria, kwa wafusia wa vyama vya CCM kubishana kwa hoja za sera, na wenzao wa ACT-Wazalendo.   ‘’Huyu Dk. Mwinyi anafaa, maana kwanza ni daktari atawafanyia uchunguuzi na kisha kuwatibu nyote...

IDADI YA WANAWAKE WATIA NIA NAFASI ZA UONGOZI UCHAGUZI 2025, YAWA TOFAUTI NA YA 2020

  Na Amrat Kombo, Zanzibar @@@@ UPEPO wa mabadiliko unaendelea kuvuma katika siasa za Zanzibar, safari hii ukivumisha na sauti ya mwanamke.  Kadri Uchaguzi Mkuu wa 2025 unavyokaribia, idadi ya wanawake wanaotia nia kugombea nafasi za udiwani, ubunge na uwakilishi imeongezeka kwa kiwango kikubwa ikilinganishwa na mwaka 2020. Ni dalili ya ujasiri, elimu na hamasa ya kijinsia katika uongozi wa kitaifa ,ishara kwamba wanawake sasa wanajitokeza kwa kujiamini zaidi kushika hatua za maamuzi. Mwelekeo huu si wa bahati, bali ni matokeo ya juhudi za muda mrefu za serikali, mashirika ya kiraia na jumuiya za kimataifa kuhimiza usawa wa kijinsia katika uongozi. Kwa mujibu wa takwimu za uchaguzi wa mwaka 2020, Zanzibar ilirekodi idadi ndogo ya wanawake waliofanikiwa kushinda nafasi za uongozi. Kati ya wagombea wa ubunge walioteuliwa na vyama, wanaume walikuwa 257 na wanawake 81, ambapo wanawake walioweza kushinda walikuwa wanne pekee. Lakini mwaka 2025 hali imebadilika. Tume ya Uchaguzi ya ...

CHUMU JUMA ABDALLAH: ANAYEINUA SAUTI YA WANAWAKE KATIKA UONGOZI

  Na AMRAT KOMBO , ZANZIBAR @@@ Kwa miaka mingi, siasa imekuwa ikitazamwa kama uwanja wa wanaume. Lakini kwa Chumu Juma Abdallah, mwanamke mwenye umri wa miaka 40, mtazamo huo unabadilika taratibu, Kutoka kuwa kijana aliyekuwa na shaka ya uwezo wake.  leo amekuwa kiongozi anayetazamwa kwa heshima, akigombea Uwakilishi wa Viti Maalum na nafasi ya Makamu Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Alliance for African Federal Party (AAFP) kwa upande wa Zanzibar. “Nilianza nikiwa ninaogopa, nikiamini siwezi, lakini viongozi wangu walinipa moyo. Waliniambia ninaweza, nami nikaamua kuthibitisha,” Amesema Chumu. Safari ya Chumu kielimu ilianza mwaka 1990 katika Skuli ya Msingi Hurumzi, kisha akaendelea na Skuli ya Sekondari Hamamni mwaka 2000. Mwaka 2002, alijiunga na Chuo cha Muslimu Mazizini, hatua aliyosema ilimsaidia kujijenga katika maadili na kujiamini. Akiwa mtoto wa nne kati ya watoto nane wa Mzee Abdallah, Chumu anakumbuka jinsi wazazi wake walivyokuwa na mashaka kuhusu azma yake ya kuin...

BADRIA ATAI MASOUD'S JOURNEY TO POLITICAL LEADERSHIP

  By Nusra Juma@@@@ FOR many years, Badria Atai Masoud, a mother of three sons and a candidate for the   Kijini   constituency representative seat under the Chama Cha Mapinduzi (CCM) party, she has devoted herself to public service with dedication, discipline, and accountability. Though this is her first time venturing into politics, Badria has emerged with remarkable energy and determination, proving that true leadership requires a sincere heart committed to serving the people. A Journey of education and professional growth Badria Atai Masoud was born on April 10, 1990, in Zanzibar, where her journey in education began in 1998 at Kajificheni Primary School, where she studied until 2004. After completing primary education, she enrolled at Benbella Secondary School in 2005, then moved to Laureate International School and graduated from Form Four in 2008. She continued her secondary education at SOS Secondary School from 2009 to 2011 before enrolling at the Mu...