Skip to main content

Posts

Showing posts from May 14, 2023

WAANDISHI HABARI PEMBA WAPEWA NENO RISITI ZA KIELEKTRONIKI

  NA HANIFA SALIM, PEMBA@@@@ AFISA Mdhamini wizara ya maendeleo ya jamii jinsia, wazee na watoto Pemba Hafidh Ali Mohamed, amewataka waandishi wa habari watumie kalamu zao katika kuelimisha jamii juu ya ulipaji wa kodi na matumizi sahihi ya risiti za elektroniki. Alisema kuwa, waandishi wa habari ndio daraja la mawasiliano hivyo, ni vyema kuitumia taaluma yao ya uwandishi wa habari katika uwandaaji wa makala na vipindi vya kila siku kwa lengo la kuielimisha jamii. Aliyasema hayo alipoua akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari, huko ukumbi wa TASAF Chake chake uliyoandaliwa na klabu ya waandishi wa habari wa Pemba (PPC) kwa ufadhili wa mamlaka ya mapato Zanzibar ZRA. "Maadhimisho haya ni muhimu na elimu mutakayoipata hapa itasaidia sana kuwajengea uwelewa juu ya masuala ya kodi, yatawasaidia kuandika habari za kweli, zenye uweledi na zilizofanyiwa utafiti wa kutosha, naomba tuyatumie mafunzo haya kwa vitendo", alis

KIJALUBA, MRADI UNAOLENGA KUKUZA PATO LA WATU WENYE ULEMAVU

  NA HAJI NASSSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI 1876, wakiwemo wanawake 1,122 na wanaume 750, kutoka shehia za wilaya ya Chake chake Pemba, wengi wao wakiwa watu wenye ulemavu, wanatarajiwa kufikiwa na taaluma ya kujikomboa kiuchumi, kupitia mpango wa kuweka akiba. Watu hao, watawezeshwa kupitia vikundi maalum vitakavyoanzishwa katika kila shehia ya wilaya hiyo, ambapo kila kikundi, kitakuwa na wastani wa wanachama kati ya 25 hadi 30. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Msaidizi afisa mradi wa kijaluba Mohamed Salim Khamis, alisema watu hao wanatokea kwenye vikundi 72, ambavyo vyote vitawezeshwa kimafunzo. Alieleza kuwa, vikundi hivyo baada ya kuanzishwa kitaalamu namna ya uwekaji akiba, kisha vitapewa elimu ya ujasiriamali, pamoja na kuunganishwa na taasisi za kifedha. Alifafanua kuwa, mradi huo unakuja kuondoa dhana kuwa watu wenye ulemavu hawezi, badala yake unakuja kuwawezesha, kuanzia mafunzo na kimbinu. Alifahamisha kuwa mradi huo, utakuja kuionesha jamii namna ambavyo w

WADAU HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU WA AKILI PEMBA WATOA RAI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAHARAKATI wa haki za watu wenye ulemvu wakili kisiwani Pemba, wamesema wakati umefika kufanyiwa marekebisho sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai nambari 7 ya mwaka 2018, ili kuongeza kifungu kitakachowanyima dhamana, watuhumiwa watakaowadhalilisha watu wenye ulemavu wa akili.   Walisema, sheria hiyo kwenye kifungu chake cha 151, kimeanisha makosa yasiyo na dhamana ikiwa ni pamoja na kuua kwa makusdi, uhaini, kubaka, kusafirisha kiwango kikubwa cha dawa za kulevya, kuingilia kinyume na maumbile.   Makosa mengine yalioanishwa kwenye kifungu hicho, ambayo hayana dhamana ni kumnajisi mtoto wa kiume, kubaka kwa kundi, kuingilia maharimu pamoja na unyang’anyi wa kutumia silaha.   Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, walisema katika kifungu hicho, haikuanishwa iwapo mtu atambaka, kumnajisi, kumuingilia kinyume na maumbile mtu, mtoto, mwanamke au mwanammke mwenye ulemavu wa akili.   Walisema, kasoro hiyo inaweza kutoa mwanywa kwa wadhali

''WANAWAKE JIAMININI, KUWENI NA MISIMAMO' DK. MZURI

  Na Nafda Hindi,  Zanzibar  Wanawake wametakiwa kujiamini na Kuwa na misimamo imara yenye lengo la kuleta mabadiliko katika nchi. Hayo yamesemwa na Dk. Mzuri Issa Ali wakati akizungumza na wanawake wenye kutia nia kugombea nafasi za Uongozi kutoka vyama mbalimbali vya siasa katika hafla iliofanyika huko Tunguu Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja. Dk.Mzuri amesema wanawake wasirudi nyuma na kubabaishawa na maneno ya baadhi ya watu wasiopenda maendeleo ya wanawake kwa kuwakatisha tama na kuwaekea vikwazo mbalimbali ili wasiweze kutimiza adhma yao hiyo. Amesema utafi uliofanywa kisayansi wanawake wanauwezo wa kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja ikilinganisha na wanaume hivyo wanawake waitumie fursahiyo ili kufikia malengo yao. Naye Mwakilishi mstaafu wa Jimbo la Magomeni Bi Hafsa Said amesema katika kupigania nafasi ya Uongozi alikutana na vikwazo mbalimbali lakini sijambo ambalo lilimkatisha tamaa bali alipambana na hatimae kushika nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka kumi.

WADAU WA KUPINGA UDHALILISHAJI PEMBA, WATAKA SHERIA INAYOTAJA KIWANGO CHA FIDIA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WADAU wa haki jinai kisiwani Pemba, wamesema wakati umefika sasa, kuwepo kwa kifungu maalum cha sheria, kinachotaja kiwango mahasusi cha fidia, kwa mtu aliyedhalilishwa. Walisema, kifungu hicho cha sheria, pamoja na kutaja kiwango, kiweke ulazima wa kulipwa kwa muhanga huyo, na hasa pia kuilazimisha Mahakama, kuzingatia maumivu ya muathirika huyo. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, walisema kwa sasa hakuna kifungu cha sheria, kinachoonesha kiwango maalum, hasa kulingana na maumivu aliyoyapata aliyedhalilishwa, hali inayopelekea kupata athari mara mbili. Walisema, kwa sasa Mahakama hufanya makisio ya kutamka kiwango cha fidia, ingawa imekuwa vigumu kutaja kiwango kwa upana wa maumvivu. Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-Hya Mussa Said, alisema wapo watoto hudhalilishwa na wengine kupoteza utu wao na wengine kupata ulemavu, ingawa fidia inayotajwa huwa ni ndogo. Alieleza kuwa, haiwezekani mt

BAADA YA KUTOFIKIWA NA ELIMU CHANJO YA UVIKO19, VIZIWI PEMBA WATOA RAI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ KUNDI la watu wenye uziwi kisiwani Pemba, limetoa raia kwa mamla husika, kuacha kuwachanganya na wengine bila ya wakalimani, wanapowafikishia taaluma za kitaifa. Wanasema, wamekuwa wakiishia kucheka na kupiga kofi, kwenye vikao na mikutano ya kutoa elimu, kwa kule kukosekana kwa mkalimani. Wameonya kuwa, kwa mfano kwenye elimu ya ugonjwa wa Uviko19, samba mba na ujio wa chanjo yake, hawakutengewa mikutano yao ya kielimu, wakiwa na wakalimani. Asha Suleiman, mkalini anayetambulika kisiwani Pemba, anasema hakuwahi kushirikishwa na wizara husika, juu ya kuwakusanya viziwi kupatiwa elimu hiyo. Hilo, anasema lilisababisha kundi la viziwi kukosa taarifa za sahihi za chanjo ya Uviko19, jambo ambalo liliwakoseha kufanya uamuzi sahihi. ‘’Shughuli kadhaa za kitaifa huwa nashirikishwa na kundi la watu wangu, lakini kwenye elimu ya chanjo ya Uviko19, hautukuwahi kuitwa,’’analalamika. WANATOA RAIA GANI KWA SERIKALI Anasema, kama

ZIJUE POSA ZA MICHEWENI ZINAVYOTOFAUTIANA NA MAENEO MENGINE

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘’NILIVUNJIKA mkono, baada ya kuparamia nyumba kumkimbia muume mtarajiwa alipokuja kwetu, ili tusionane,’’anasema Saada Khsmi Kombo (65) wa Micheweni. Hadi leo mkoni wake mmoja wa kushoto, eneo vilipootea vidole hapako sawa,baada ya ajali hiyo. Kwa utamduni ulivyokuwa enza hizo, ilikuwa mwanaume hata kwa ambae alishabisha hodi na kuweka nia ya kufunga ndoa, haikuwa rahisi, kukutana na mtarajiwa wake. Ndio maana Saada anasema, alilazimika kwenda mbio nyingi, kwani hakuwa na hamu ya kukutana na mume wake mtarajiwa, hasa kutokana na malezi yalivyokuwa. KWANINI ILIKUWA HAWAONANI? Rehema Faki Sheha (60), baada ya muume kuweka nia na posa kufuata, hapo mwanamke hukosa hamu hata ya kula, na hakukua na jambo la ushawishi la kukutana nae. Anasema huo ndio utamaduni wa Micheweni, na wao wakiurithi tokea enzi na karne, ingawa hayo anasema ilitokana na mafundisho ya wazazi wao. Walikuwa wakielezwa, kuwa mara baada ya mtoto wa kike kufikia utuuzima (kuv