Skip to main content

Posts

Showing posts from July 30, 2023

SMZ YAPANDISHA BEI YA KARAFUU MSIMU 2023/2024

  SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar,  imepandisha bei ya karafuu kutoka shilingi 14000 hadi shilingi 15000  kwa kilo moja ya  Daraja la Kwanza kwa mwaka 2023-2024. Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Omar Said Shaaban wakati akitoa taarifa kwa Waandishi wa Habari kuhusiana na kufunguliwa kwa vituo vya kununulia karafuu kwa Unguja na Pemba katika ofisi za Wizara hiyo Kinazini. Alisema Shirika la Biashara la Taifa litafungua vituo mbali mbali vya kuauzia karafuu kuanzia tarehe 3   mwezi huu  Unguja na Pemba hivyo amewataka wananachi kuuza karafuu zote katika Shirika hilo  la Biashara la Taifa ZSTC. Alifahamisha kuwa kwa hatua ya awali shirika litaanza kufungua kituo cha Saateni kwa Unguja na kwa upande wa Pemba watatumia Kituo cha Mkoani,Madungu na Bandarini Wete kuuzia zao hilo na kauahidi kuongeza kufungua Vituo vyengine kulingana na mahitaji. Akizungumzia suala la malipo kwa wakulima wazao hilo alisema shirika limejipanga kuwalipa wananchi hapohapo kwa mfumo wa  Kielektroniki k

MDHAMINI AFYA AWAONESHA NJIA WAANDISHI WA HABARI ELIMU AFYA YA UZAZI

  HABIBA ZARALI, PEMBA   Ofisa Mdhmini Wizara ya Afya Pemba, Khamis Bilali Ali amewataka waandishi wa habari kuendelea kuelimisha jamii ili wafahamu umuhimu wa afya ya uzazi.   Alisema, moja ya kipaombele cha Wizara ya Afya ni kupunguza vifo vya mama na mtoto, hivyo endapo waandishi wa habari watatumia nafasi yao kutoa elimu hiyo, hakuna shaka kwani lengo litafikiwa.    Afisa Mdhamini aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya ufungaji wa mafunzo ya siku tatu yanayohusiana na afya ya uzazi yaliyofanyika katika ofisi ya TAMWA Mkanjuni Chake Chake.   Alisema, bado kuna uwelewa mdogo kwa jamii katika kutambua afya ya uzazi, jambo ambalo linachangia kukosekana kwa afya bora kwa mama na mtoto.   Alieleza kuwa, Wizara ya Afya inathamini sana mchango wa waandishi wa habari katika kutoa taaluma mbali mbali na kuifanya jamii kuweza kubadilika na hatimae kufikia malengo mazuri yaliyokusudiwa.    "Nyinyi waandishi ni kioo kwa jamii kwani