NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ .....BADO wanamtaka, bado wanamtamani, bado wana hamu nae katika safu ya uongozi. Maana wanasema, ameyatekeleza aliyoaahidi, maana wanasema kweli ni mtetezi wa wananchi. Ni Mgombea Uwakilishi Jimbo la Chambani wilaya ya Mkoani, kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi ‘CCM’ Bahati Khamis Kombo, anaewania tena nafasi hiyo kwa mara ya tatu, hapa anaesema kama akipata tena ridhaa, kundi la wanawake wajane na vijana, atawaimarishia miundombinu ya kujiwezesha kiuchumi. Akizungumza na waandishi wa makala hii, mara baada ya uzinduzi wa kampeni eneo la Dodo Pujini, alisema kupitia Ilani ya CCM, mikakati yake, ni kuona na kundi hilo analiwezesha. Alisema, ndani ya jimbo hilo, anajua kuwa wapo vijana wasiokuwa na ajira na wale wajane walionyimwa haki zao kwa njia moja ama nyingine, hivyo nia yake ni kuwawezesha. Alieleza kuwa moja ya mbinu atakazotumia ni kuwapa taaluma ya ujasiriamali na kuwatafutia mikopo, ambayo itakuwa chachu ya kuendesha maisha yao. ...