Skip to main content

Posts

Showing posts from September 28, 2025

MGOMBEA UWAKILISHI CCM CHAMBANI KUWAWEZESHA WAJANE, VIJANA AKIPATA RIDHAA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MGOMBEA Uwakilishi Jimbo la Chambani wilaya ya Mkoani, kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi ‘CCM’ Bahati Khamis Kombo, amesema kama akipata tena ridhaa, kundi la wanawake wajane na vijana, atawaimarishia miundombinu ya kujiwezesha kiuchumi. Akizungumza na waandishi wa habari, mara baada ya uzinduzi wa kampeni eneo la Dodo Pujini, alisema kupitia Ilani ya CCM, mikakati yake, ni kuona na kundi hilo analiwezesha. Alisema, ndani ya jimbo hilo, anajua kuwa wapo vijana wasiokuwa na ajira na wale wajane walionyimwa haki zao kwa njia moja ama nyingine, hivyo nia yake ni kuwawezesha. Alieleza kuwa moja ya mbinu atakazotumia ni kuwapa taaluma ya ujasiriamali na kuwatafutia mikopo, ambayo itakuwa chachu ya kuendesha maisha yao. Alisema njia nyingine ni kuwawezesha kwa kazi za mikono, kama kufuma na kushona, ili iwe njia sahihi ya kufikia ndoto zao. ‘’Hapa ninacho hitaji kutoka kwa wananchi wa jimbo hili, kwanza waweke kando tofauti za vyama, wanipe ...

INSPEKTA KHALFAN AHIMIZA JAMII KUJIKITA KILIMO CHANYE TIJA

NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@  MKAGUZI wa shehia ya Mlindo Wilaya ya Wete Inspekta wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Khalfan Ali Ussi amewataka wananchi wa shehia hiyo kuendelea kukiamini kilimo kwani ndio njia pekee itakayowasaidia kuwainua kiuchumi. Akizungumza katika muendelezo wa ziara yake ya ushirikishwaji wa jamii katika dhana ya ulinzi shirikishi wakati akikagua shamba la Hassan Hamad Hassan na familia yake, aliwapongeza kwa kuamua kujiwekeza kwenye kilimo na ufungaji kwa ajili ya kujipatia kipato cha kujikimu kimaisha. Alisema kuwa, kilimo ni uti wa mgongo wa maendeleo katika nchi, hivyo ni vyema wakakiamini na kuelekeza nguvu zao zaidi huko, ili kiwaletee manufaa katika familia zao na jamii kwa ujumla.  "Ninachowashauri tu msitumie jembe la mkono kwa sababu mnachoka sana kwani mnatumia nguvu nyingi, hivyo mulime kwa kutumia zana za kisasa, pia mjitahidi kuzingatia uhifadhi wa mazingira kwa kutumia mbolea rafiki ili kilimo chenu kiwe endelevu na kuzalisha mazao b...

HAYA HAPA MAAJABU YA ARV DHIDI YA MTOTO MCHANGA, PINDI UKIFUATA..........

  NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@ ARV ni dawa zinazopambana na virusi vya VVU kwa mtu anayeishi na maambikizi ya virusi hiyo. Wataalamu wa afya mwanadamu wanakubali kuwa, dawa hizo zinasaidia mno kumpa uhakika wa kusihi , mtu anayeishi na VV. Wanakubali kuwa, zenyewe hazitibu VVU, bali huzuia virusi kuongezeka na kulinda kinga ya mwili. Lengo ni kupunguza virusi hadi kufikia kiwango cha kutogundulika ( undetectable ) . Wataalamu wa afya wanasema d awa za ARV , zinai ngia ndani ya seli za kinga na kuzaliana, na kisha h ukatiza hatua za uzalishaji wa virusi k wa njia hiyo . Kitaalamu k una madaraja mbali mbali ya ARV, lakini huwa hutolewa kwa pamoja kama mchanganyiko.   Mfano, ’ T + L + D ’ huu ni mfumo wa kitaalamu ambao ni mchanganyiko wa kidonge kimoja chenye dawa tatu , ambapo d aktari huchagua dawa kulingana na afya y a mgonjwa.   Daktari Khamis Hamad Ali ambae ni Mratibu wa kitengo cha maradhi ya Ukimwi, homa ya Ini, Kifua kikuu...

OTHMAN KUJA NA MPANGO WA UBINAFSISHAJI ZAO LA KARFUU ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MGOMBEA Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya ACT- Wazalendo Othman Massoud Othman, amesema kama akipata ridhaa ya kuiongoza Zanzibar, atakuza uchumi, kwa kulibinafsisha zao la karafuu. Mgombea huyo wa urais wa aliyasema hayo leo Septemba 30, 2025, uwanja wa mpira wa Daya Jimbo la Mtambwe wilaya ya Wete Pemba, wakati akizungumza, kwenye mkutano wa hadhara wa chama hicho, jimboni humo. Alisema, Zanzibar katika eneo moja la kukuza uchumi ni wakulima wa karafuu, hivyo atahakikisha analiimarisha zao hilo kwa kulibinafsisha. Alieleza kuwa, anachohitaji ni kupewa ridhaa kutoka kwa wananchi, ili kuhakikisha zao la karafuu analiongezea thamani na kurudi mikononi kwa wakulima. Alieleza kuwa katika eneo hilo, atahakikisha anaongeza pia bei na kufikia kilo moja shilingi 20,000 ili kuhakikisha linamnufaisha mkulima. Aidha mgombea huyo wa urais, alisema ili kuhakikisha mkulimana anafaidi zao hilo la taifa, nni kulibinafsisha. ‘’Mkinipa ridhaa nitahakikisha za...

MAAFISA JESHI LA POLISI WATAKIWA KUHESHIMU HAKI ZA BINAADAMU

NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ KAMISHNA wa Tume ya Haki za Binadamu Zanzibar Khatib Mwinchande amesema, maafisa wa utekelezaji wa Sheria kwa nyakati zote wanapaswa kutimiza wajibu walioekewa kisheria kwa kuhudumia jamii na kulinda watu wote dhidi ya vitendo vinavyoenda kinyume na Sheria, kwa kuzingatia kiwango cha juu cha uwajibikaji kinachohitajika na taaluma yao. Akizungumza na maafisa wa Jeshi la Polisi Pemba katika mafunzo ya uzingatiwaji wa haki za binadamu na misingi ya Utawala Bora katika mchakato wa uchaguzi mkuu 2025 yaliyofanyika katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Wete, kamishna huyo alisema, katika kipindi cha uchaguzi Jeshi la Polisi lina wajibu wa kujiepusha na migogoro isiyo ya lazima na badala yake wahakikishe usalama wa watu na mali zao katika kipindi chote cha uchaguzi. Alisema kuwa, ni wajibu wa Jeshi la Polisi kusimamia uhuru, haki na amani ili wananchi waweze kutimiza haki yao ya kikatiba katika kuchagua viongozi wao, huku wanapotekeleza majukumu yao wazingatie maadi...