Skip to main content

Posts

Showing posts from June 16, 2024

PACSO, YAJENGA DARAJA KWA WAANDISHI, WANAASASI PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAANDISHI wa habari na wana asasi za kiraia Pemba, wametakiwa kufanyakazi kama mwili mmoja, ili wanapofuatilia kero za wananchi, iwe kazi rahisi kuzipatia ufumbuzi.   Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ Mohamed Najim Omar, wakati akiufungua mkutano wa siku moja, kwa waandishi hao wa habari na wanaasasi za kiraia Pemba, mkutano uliofanyika leo Juni 21, 2024 ukumbi wa Maktba Chake chake.   Alisema, waandishi wa habari na wanaasasi za kiraia, imegundulika wote wanawatetea wananchi wanaokabiliwa na changamoto, mfano ya ukosefu wa barabara, hivyo ni vyema wakashirikiana katika hilo.   Katika hatua nyingine Najim, alisema ushirikiano kati ya pande mbili hizo, unaweza hata kubadilisha sera na sheria, ambazo zinaonekana kupitwa na wakati, katika uendeshaji wa shughuli zao.   Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa ‘PACSO’ Sifuni Ali Haji, alisema anategemea baada ya kumalizika kwa mradi huo, kuweko na mabadiliko makub

WANAOJIFUNGULIA MAJUMBANI WAZUNGURUKWA NA MAJANGA LUKUKI, KIFO KUPOTEZA DAMU VIMO

  NA FATMA HAMAD, PEMBA@@@@ ‘MIMBA yangu ya nne manusura niiage dunia’. Asha Said mama wa watoto wanne ambae sio jina lake halisi anasema, mimba yake ya pili alijifungulia nyumbani, na alipata tatizo la kutokwa na damu nyingi, na kupelekea hadi kupoteza fahamu. ‘’Baada tu ya kujifungua sikujifahamu tena, mpaka nilikuja kuzinduka nimewekewa chupa ya maji hospitali ya Micheweni,’’anaeleza. Mume wa mama huyo ambae hakupenda jina lake lichapishwe, anasema baada ya kuona hali ya mke wake imeshakuwa mbaya, ndipo usiku huo, alipokodi gari na kumpeleka Hospitali. Hivyo alipatwa na huzuni, hali ambayo ilipelekea kupoteza gharama kubwa ya matibabu, kwa ajili ya kuokoa maisha ya mke wake, pamoja na mtoto.   ‘’Nilipata funzo na sasa nikimuona tu uchungu umeanza namuwahisha hospitali haraka, kwani huko akipata matatizo anaweza akawahiwa mapema na watalamu wa afya,’’anaeleza.   Maryam Said mkaazi wa Chake chake ambae anaishi na virusi vya ukimwi kwa muda wa miaka 18, alimuambukiza mtot

USHIRIKA 'JAMBO NIA' MFIKIWA KUVUNA 'MAHELA' KWA UVUNAJI ASALI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAUSHIRIKA wa ‘jambo nia’ wa kijiji cha Fuuweni shehia ya Mfikiwa wilaya ya Chake chake, wanaojishughulisha na ufugaji wa nyuki, wamesema wanategemea, kujiingizia wastani wa shilingi milioni 1.6, ikiwa mizinga yao 13, itazalisha chupa 65 za asali. Walisema, fedha hizo wanategemeza kuzipata, miezi minne ijayo kutoka sasa, kupitia mzinga yao 13 walioitega mwaka jana. Walieleza kuwa, fedha hizo zitatokana na kuuza chupa 65, wastani wa shilingi 25,000 hadi 30,000 kwa chupa moja, yenye ujazo wa lita moja. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kijijini hapo, walisema waliamua kuanzisha kilimo cha nyuki, kwa malengo kadhaa, ikiwemo kujipatia kipato na kuhifadhi mazingira. Walieleza kuwa, kupitia mizinga hiyo 13, kama hakutavuna upepo mkali ukiambatana na mvua, wanategemea kila mzingia, kuvuna chupa tano, na kujipatia chupa 65 kwa mizinga yote. Mwenyekiti wa ushirika huo Hassein Khamis Salum, alisema wazo hilo, lilikuja kuanzia mwaka 2022, baada ya

CP-HAMAD: 'MSITOE VIBALI VYA MUZIKI OVYO OVYO"

  NA OMAR HASSAN, ZANZIBAR@@@ Kamishna wa Polisi Zanzibar CP HAMAD KHAMIS HAMAD amewataka watendaji wa Baraza la Sanaa Sensa ya Filamu na Utamaduni kufuata sheria katika kutekeleza majukumu yao na wasitoe vibali vya kupiga muziki kwa watu wasiokuwa na sifa ili kuondoa kero kwa wananchi zinazosababishwa na wapiga muziki. Akizungumza na Viongozi wa Baraza hilo ambao wameteuliwa hivi karibuni, waliofika Makao Makuu ya Polisi Zanzibar kujitambulisha, CP HAMAD amewataka kuwachukulia hatua bila ya kuwaonea muhali wanaokiuka sheria ili wananchi waendelee kuwa na Imani na Serikali yao kakika kuwaondolea kero. Nae Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa Sensa ya Filamu na Utamaduni JUMA CHOUM JUMA ameliomba Jeshi la Polisi kuendelea kushirikiana nao ili kufanikisha kazi za Baraza hilo. Kwa upande wake Mkuu wa Polisi Jamii Zanzibar, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP JONAS MAHANGA amelihimiza Baraza la Sanaa kuwasimamia wasanii kutoa maudhui yenye maadili na kuhamasisha Uzalendo. MWISHO

POLISI SHEHIA, MASHEHA PANGENI MIKAKATI YA KUZUIA UHALIFU – CP HAMAD

  NA OMAR HASSAN, PEMBA@@@@                                                     KAMISHAN wa Polisi Zanzibar CP. HAMAD KHAMIS HAMAD amewataka Wakaguzi wa Shehia na Watendajiwa Madawati ya Jinsia na Watoto kuweka mikakati itakayoishirikisha jamii kubaini na kuzuwia uhalifu ikiwemo vitendo vya udhalilishaji ili jamii ibaki salama. Akizungumza na Maafisa, Wakaguzi na Askari wa Mikoa ya Kaskazini na Kusini Pemba huko Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Wete amesema watendaji wa Polisi wanafanya kazi kubwa ya kutoa elimu kwa jamii lakini bado makosa yanaendelea kufanywa hivyo ametoa rai ya kufanya kwa kufanya tathmini sambamba na kuishawishi jamii kutekeleza wajibu wao wa kushiriki katika kujiwekea ulinzi. Nae Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP WILLIAM MWAMPAGHALE amesema Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba limejipanga kuweka ulinzi hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Skuu ya Idd El Adh-ha. Add reaction

SIKU YA MTOTO WA AFRIKA, FAMILIA ZIWAPE UHURU WA KUCHEZA WATOTO WENYE ULEMAVU KUWAFUNGIA NI KUDIDIMIZA VIPAJI VYAO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SIKU ya mtoto wa Afrika, ni siku maalum inayoadhimishwa kila mwaka, kwa lengo la kujenga ufahamu na kuongeza juhudi za kuimarisha hali ya watoto barani Afrika . Ambapo kilele cha siku hii, iliadhimishwa Juni 16 ya kila mwaka, kwa lengo la kuwakutanisha watoto, kujadili mafanikio na changamoto zao. Siku hii, inaanzia pale mwaka 1991, wakati wa mkutano wa kwanza wa baraza la mawaziri wa Umoja wa nchi za Afrika (OAU). Ulifanyika nchini Cairo Misri, ambapo katika mkutano huo, baraza la mawaziri, lilipendekeza kuanzishwa kwa siku ya maalum ya mtoto wa Afrika. Ukitaka kuiweka haki na ustawi wa watoto, kwenye ajenda ya kisiasa, kiutamaduni na kijamii barani Afrika. Ndipo hapo, ilipozaliwa Juni16 ya kila mwaka, iwe ni siku ya mtoto wa Afrika, kutokana na tukio la kusikitisha lililotokea mwaka 1976, Soweto nchini Afrika Kusini.   Siku hiyo, taarifa zinaeleza kuwa, maelfu ya wanafunzi wa skuli za upili, walijitokeza kuandamana kupinga ubaguzi wa rangi