Skip to main content

Posts

Showing posts from November 30, 2025

DISEMBA 3 YA MWAKA HUU, ITUKUMBUSHE UJUMUISHI KWA KILA JAMBO

    NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ DISEMBA 3 ya   kila mwaka dunia huadhimisha siku ya kimataifa ya watu wenye ulemavu. Siku hii ilianza kuadhimishwa mwaka 1992 na umoja wa mataifa, lengo likiwa ni kuongeza uwelewa juu ya mambo yanayo husu watu wenye ulemavu. Pia   inalenga kutoa elimu kwao na kwa jamii   juu ya haki zao na kuongeza ufahamu juu ya uungwaji mkono kwa ajili ya utu, heshima na ustawi wao. Historia inaonyesha watu wenye ulemavu walikua na wakati mgumu zaidi kwa miaka iliopita. Kwakile kinachooeleza kua walikabiliwa na changamoto kadhaa ikiwa ni pamoja na kutelekezwa na   kunyimwa haki zao za msingi ikiwemo ya kuishi. Hivyo uwepo wa siku hii ni kuthamini na kuenzi utu na heshima ya watu wenye ulemavu ambavyo vilitiwa kapuni kwa miaka mengi. Hivyo Disemba 3 ni wito wa kukumbatia utofauti wa kimaumbile tulio nao, kuvunja vizuizi na kuhakikisha mustakbali uliojumuishi zaidi kwa watu wote. Ikizingatiwa kwamba takribani watu bilioni 1.3 d...

MDHAMINI MAKAMU WA KWANZA, AELEZEA UBORA MATUMIZI YA GESI

  NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ AFISA Mdhamini Afisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Ahmed Abuubakar Mohamed, amesema mazingira mazuri ni kuunga mkono kwa kutumia nishati salama ya gesi, ikiwa ni njia moja wapo ya kulinda mazingira yao, ili kuweka mabadiliko yanayotokezea kutokuwa na hali nzuri ya kimazingira. Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza wafanyabiasha ya ‘Oryx gas’ juu ya matumizi salama ya nishati safi ya kupikia, ukumbi wa Tibirinzi Chake chake Pemba. Alisema kuwa utumiaji mzuri wa gesi na uhamasishaji, wanaweza kulinda hali ya mazingira, ukataji wa miti ovyo na uchimbaji wa nchanga na uharibifu wa viunbe hai ambavyo vinaweza kuwa mazingira mazuri. " Uwepo wenu kutasaidia wananchi kutumia nishati safi na salama ya kupikia, pamoja na kuacha kukata miti na mbadala wake, kutumia gesi, ili kuhakikisha hali ya mazingira inakuwa salama," alifafanua.     Meneja Mkuu wa taasisi ya Oryx gas Zanzibar Shuwekha Khamis Omar, alisema kuwa, wanadhamira ya kuhak...

LEO SIKU YA WATU WENYE ULEMAVU DUNIANI, MATAMU YAO HAYA HAPA KWA ZANZIBAR

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SIKU ya kimataifa ya watu wenye ulemavu duniani, ilianza kuadhimishwa mwaka 1992 na Umoja wa Mataifa. Ta ngu kuanzishwa kwa siku hii, kumekuwa na mafanikio mbalimbali duniani, ambapo kwa Zanzibar pekee, ni kuwepo wa sheria nambari 8 ya mwaka 2022. Malengo ya siku hii, ni kuongeza uelewa juu ya mambo yanayohusu watu wenye ulemavu, pamoja na kutoa elimu juu ya haki na fursa zao. Taarifa za mitandao zinafafanua kuwa, siku hii hutazamiwa kuongeza uelewa kwa watu wenye ulemavu, katika masuala kadhaa, likiwemo la uchumi wao. Malengo endelevu ya dunia Sustainable Development Goals ‘SDGs’ ni mkusanyiko wa malengo 17 yalopangiliwa kwa faida ya watu wote ulimwenguni, wakiwemo wao. Maana, malengo haya yalianzishwa mwaka 2015 na Baraza kuu la umoja wa mataifa, yalikiwa na malengo ya kufikiwa mwaka 2030, kama sehemu za ajenda za mwaka huo. Kwani inafahamika kuwa, miongoni mwa malengo hayo endelevu ni pamoja...

MWAKILISHI WA VIJANA WA BARA: MMISRI AKABIDHI MATOKEO YA MKUTANO WA VIJANA KWA MEYA WA JOHNNESBURG

  * TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KWA AJILI YA KUCHAPISHWA...* Hassan Ghazaly, Mmisri na mwanachama wa Kamati ya Mawasiliano ya Mfuko wa Ukaguzi wa Maridhiano wa Afrika (APRM) na Mwanzilishi wa Mtandao wa Mshikamano wa Kimataifa, amekabidhi matokeo ya Mkutano wa Tano wa Vijana wa Afrika uliofanyika Afrika Kusini kwa Mheshimiwa Dada Morero, Meya wa Jiji la Johannesburg, na Balozi Marie Antoinette, Mwenyekiti wa APRM. Hii ilifanyika katika hitimisho la Mkutano wa Vijana wa Afrika, uliofanyika katika Bunge la Panafrika, Afrika Kusini, chini ya kaulimbiu: “Vijana katika Utawala: Kutoka Ahadi hadi Ustawi.” Katika muktadha wa shughuli za mkutano huo, vikao vilishuhudia ushiriki mkubwa wa baadhi ya viongozi mashuhuri wa kikanda na kimataifa, wakiwemo: Rais Heshima wa Mkutano, Sharif Fortun Zivania Sharombera; Rais wa Bunge la Afrika, Laila Dahi; Mwenyekiti wa Kamati ya Vijana ya Bunge la Afrika, Ahmed Bening; Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Afrika, Dkt. Sunshine Minenhl Miendi; Mwenyeki...

KIDUTANI WAPITISHA KANUNI KUSIMAMIA MALEZI YA VIJANA WAO

    NA MOZA SHAABAN, PEMBA @@@@ KAMATI ya maadili na taaluma ya kijiji cha Kidutani shehia ya Chumbageni Wilaya ya Mkoani Pemba, imepitisha kanuni 19 zitakazowaongoza katika kusimamia malezi ya watoto na vijana. Akizungumza kijijini hapo   katika kikao cha kupitisha kanuni hizo kilichoandaliwa na   kamati hiyo Mwakilishi wa sheha ambae pia ni Mratibu wa kamati ya maadili ya shehia hiyo Abrahman Mohamed Khamis alisema, Ofisi ya sheha ipo tayari kushirikiana na wanakijiji   katika kusimamia kanuni hizo. Alisema ni vyema wananchi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa kamati hiyo, ili lengo liweze kufanikiwa, huku akiwataka wanakamati hao iwapo patakua na kikwazo chochote katika utekelezaji majukumu yao, kupeleka changamoto zao kwa sheha. "Ofisi ya sheha ipo tayari kushirikiana na nyinyi katika hili, naomba na wananchi mutoe ushirikiano wa kutosha ili kufanikisha jambo hili, na iwapo patatokezea kikwazo   katika utendaji kazi wenu musisite kuripoti kwa sheha...

TUME YA MIPANGO YAWANOA MAAFISA UFUATILIAJI NA TATHMINI

    NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ Maafisa ufuatiliaji na tathmini wa wizara mbali mbali   Pemba wameshiriki katika mafunzo ya   kujengewa uwezo juu ya ufuatiliaji na tathmini za miradi, ili kufanya kazi zao kwa ufanisi. Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo    katika ukumbi wa makonyo Wawi chake chake Pemba   mgeni rasmi kwa niaba ya   Kaimu   Katibu mtendaji   Tume ya mipango Zanzibar, Kamishna idara ya Uchumi   Ameir Haji Sheha alisema, mafunzo hayo ni muhimu kwa maafisa hao katika utekelezaji wa majukumu yao ya kikazi. Alisema mafunzo hayo yatasaidia kujenga utamaduni wa kufuatilia na  kutathmini ili  kupata takwimu sahihi za utekelezaji miradi na shughuli za maendeleo , ambazo mara nyingi hutumika katika utaarishaji wa mpango wa maendeleo ya Zanzibar. Alisema ufuatiliaji na tathmini husaidia watekelezaji wa miradi kujua mwelekeo wa utekelezaji   wa kazi zao, ili kuhakikisha utimilifu wa malengo ya mda mr...