Skip to main content

Posts

Showing posts from July 28, 2024

WIKI YA MWANANCHI, MAMBO NI MOTOOO....MASHABIKI BAGAMOYO WATOA MSAADA WA MADAWATI

  Na Mwandishi Wetu@@@@ Kuelekea wiki ya Mwananchi, Mashariki wa klabu ya Yanga wa Kijiji cha Buma kilichopo Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani,  wamejitokeza kutoa misaada mbalimbali ya kijamii ikiwamo madawati. Mashabiki hao walikabidhi madawati hayo katika  shule ya Msingi Buma iliyopo kijijini hapo ikiwa ni mwendelezo wa kutoa misaada kwa jamii kuelekea siku ya Mwananchi inayotarajiwa kufanyika Agosti 4 Mwaka huu katika Uwanja wa Benjamin Mkapa maarufu 'Lupaso'. Akizungumza katika makabidhiano hayo, Mwenyekiti wa Klabu hiyo Tawi la Buma Ismail Omary amesema kuwa, wanachama  wamekua na utaratibu wa kutoa misaada mbalimbali kwa jamii, lengo ni kurudisha hisani kwa wananchi wanaowazunguka kutokana na mwendelezo mzuri wa timu yao. " Leo tumejitokeza kwenye viwanja vya shule ya msingi Buma lengo ni kutoa msaada wa madawati ili wanafunzi waweze kuyatumia wakati wa masomo, huu ni utaratibu wetu wa kurudisha fadhira kwa wananchi kutokana na  hamasa tunqzozipata za timu yetu kuch

'MAREKEBISHO KANUNI ZA MAADILI VYAMA VYA SIASA KUJALI USAWA WA KIJINSIA'

  ZANZIBAR                                                                                             Naibu Msajili wa vyama vya siasa Mohammed Ali Ahmed amesema sheria na kanuni za maadili ya vyama vya siasa zinaendelea   kufanyiwa marekebisho kwa lengo la kuweka usawa wa kijinsia pamoja na kukuza uwajibikaji na kuzuia unyanyasaji dhidi ya wanawake ili waweza kushiriki kikamilifu katika siasa na   demokrasia nchini. Akizungumza kwa niaba ya Naibu Msajili wa vyama vya siasa, Afisa sheria Mwandamizi kutoka ofisi hiyo Abdulrazak Ali kwenye mkutano wa tathmini iliyoangalia vikwazo vinavyowakwaza wanawake katika kugombea na kushiriki masuala ya kisiasa   uliofanyika   ukumbi wa ZURA Maisara mjini Unguja, ambao uliowashirikisha wadau mbalimbali kutoka taasisi za Serikali, vyama vya siasa, Asasi za kiraia, wanaharakati na viongozi wa dini. Akizitaja sheria na kanuni zinazoendelea kufanyiwa marekebisho ni pamoja na Political Parties Act (2019), Political Parties Code of Conduct (CAP.25