Skip to main content

Posts

Showing posts from September 8, 2024

WAKULIMA MRADI WA VIUNGO WAKABIDHIWA VIFAA

  NA NAFDA HINDI, ZANZIBAR@@@@  WAKULIMA wanaojishughulisha na kilimo cha  mboga mboga, matunda na viungo kupitia  MRADI wa  VIUNGO (AGRI-CONNECT)  wamekabidhiwa vifaa vitakavyowasaidia kuongeza nguvu katika uzalishaji wa bidhaa bora zitakazokidhi masoko. Akizungumza katika hafla ya kukabidhi vifaa hivyo iliofanyika katika jengo la Kificho Mwanakwerekwe Meneja Mkuu wa mradi huo Simon Makobe alisema  vifaa hivyo vitatumika kusaidia kuongeza uzalishaji na kufikia malengo ya utekelezaji wa mradi huo. Alisema MRADI wa VIUNGO ulilenga mambo mbalimbali ikiwemo kufungua fursa na kuongeza mnyororo wa thamani ya mazao hapa Zanzibar pamoja na kupatiwa vifaa kwa lengo la kuwawezesha wakulima kuwa na nyenzo muhimu ili kulima kilimo bora kitakachowasaidia kujikwamua kiuchumi,”alisema.  “Ugawaji wa vifaa hivyo ni moja ya mikakati ya utekelezaji wa mradi huo pamoja na kutumia ujuzi mulioupata juu ya matumizi ya teknolojia muliyojifunza kipindi chote cha utekelezaji wake,” alisema Makobe. Alifahamisha

'WANAWAKE KUSAIDIA KIUCHUMI' : WAZIRI PEMBE

             Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto imeahidi kuendelea kushirikiana na Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (ZEEA) katika kuwapatia wananchi fursa zitakazoweza kuwasaidia kujikwamua kimaisha na kuwajengea uwezo ikiwa ni ya chachu ya maendeleo yaliokusudiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ). Kauli hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki iliyopita na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Riziki Pembe Juma wakati akiwa katika ziara ya Chuo cha Wajasirimali Wanawake (Bare foot Collage) kiliopo Kinyasini Mkoa wa Kaskazini Unguja. Amesema lengo la ziara yake ni kujifunza pamoja na kuona jitihada zinazofanywa na wanawake katika jamii, hivyo Wizara itaendelea kushirikiana na Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (ZEEA) katika kuwapatia wanawake fursa na kuondokana na ugumu wa maisha. Amefahamisha kwamba kila mwanamke ni kiongozi katika familia hivyo Serikali   itaendelea kuwaunga mkono wanawake na kuwashauri wajasirimali Wanawake kuto

MWAKILISHI CUP CHAMBANI YAZINDULIWA, NADHAF YATUPWA NJE

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ TIMU ya soka ya Nadhaf ya Wambaa, imetupwa nje kwa matuta na timu ya Mkaa, kwenye michauano ya kuwania kombe la Mwakilishi wa Jimbo la Chambani, baada ya kutoshana nguvu kwenye dakika 90. Mchezo huo uliovuta hisia za wingi, ulikuwa wa ufunguzi, ulipigwa uwanja wa Wambaa, ambapo wanacheza kwa mtindo wa mtoano, na bingwa ataondoka na kitita cha shilingi milioni 1, kutokwa kwa Mwakilishi huyo. Wakati wanaume hao wakishindwa kutambiana kwenye dakika za kawaida, hatua ya kupigiana mikaju ya penalti, ilifanyika na timu ya Nadhaf, ikipoteza mkwaju mmoja, na wenzao kundoka na yote mitano. Kabla ya ngarambe hizo, Mwakilishi wa Jimbo la Chambani Bahati Khamis Kombo, alisema huo ni mwanzo, lakini kuna mashindani makubwa zaidi ya ngazi ya shehia yanakuja. Alisema, mashindani ya msimu huu yenye zaidi ya timu 12, ni madogo na mshindi amepanga kupata shilingi milioni 1, ingawa hayanyokuja mshindi ataondoka na shilingi milioni 5. Alieleza kuwa, wameamua kuan

SHEIKH SAID, AWAONESHA NJIA WAZAZI CHUMBAGENI KUWA NA KIZAZI CHEMA

    NA SALIM HAMAD, PEMBA@@@@ WAZAZI na walezi katika shehia ya Chumbageni wilaya ya Mkoani Pemba, wamehimizwa kuwasomomesha watoto wao kitabu kitukufu cha Qu-ran, ili kupatikana kwa kizazi chenye misingi ya maadili mema leo na baadae. Shekh Said Abdalla Nasor, ametoa kauli hiyo leo Septemba 8, 2024, wakati akizungumza na wazazi, walimu na wanafunzi wa Amladrasatul Imanniya ya Chumbageni Wambaa wilayani humo, katika mahafali ya kuwatunuku vyeti wanafunzi waliomaliza juzuu 30, na tathmini ya mwaka uliopita kwa madrssa hiyo. Alisema ili kupatikana kwa viongozi bora wa nchi, maimamu, masheikhe na hata watumishi wa umma wa baadae, hakuna budi kwa wazazi katika kuwabidiisha watoto wao, kukisoma kitabu hicho. Alieleza kuwa, taifa linahitajia madaktari, wakuu wa wilaya, waalimu wa madrassa na masheikhe wenye misingi ya dhati ya dini ya kiislamu, ambapo hilo litafanikiwa, ikiwa watakisoma kwa dhati kitabu hicho. ‘’Nichukuwe nafasi hii, kuwataka wazazi na walezi wetu, kuhakikisha tu