Skip to main content

Posts

Showing posts from December 31, 2023

BITEKO AWEKA JIWE LA MSINGI OFISI, MAAKAZI YA UHAMIAJI MKOANI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ NAIBU Waziri Mkuu, ambae pia ni Waziri wa Nishati wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Doto Mashaka Biteko, amesema kitendo cha kufanyika kwa mapinduzi ya Zanzibar, kilikuwa chema, kwani kililenga kuwapa uhuru wa wananchi, kusafiri nje ya mipaka kadiri wapendavyo. Naibu Waziri huyo Mkuu, aliyasema hayo Disemba 6, mwaka 2024 uwanjwa wa Umoja ni nguvu Mkoani Pemba, mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi, wa ofisi na makaazi ya maafisa wa Uhamiaji, wilayani humo, ikiwa ni shamra shamra za miaka 60 ya mapinduzi. Alisema, mapinduzi hayo, yalikuwa yanafaa mno kuona wazanzibari na wananchi wote, wanatumia haki yao kwenda watakako kwa mujibu wa sheria, uhuru ambao hawakuwa nayo, kabla ya mapinduzi. Alieleza kuwa, mapinduzi hayo kupitia viongozi na wakuu wa nchi tokea mwaka 1964 hadi leo, wanaendelea kusimamia haki hiyo, ili kuhakikisha wananchi, wanasafiri zaidi nje ya mipaka ya Tanzania. ‘’Kila mmoja ni shahidi, baada ya kufanyika kwa mapinduzi haya n

DK. MWINYI AZINDUA BARABARA YA LAMI BIRIKAU, AWAPA NENO MADEREVA

   NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema serikali ya awamu ya nane, itaendeleza kwa vitendo, malengo ya mapinduzi ya Zanzibar, ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya kisasa, kama vile barabara. Dk. Mwinyi aliyasema hayo Disemba 4, mwaka 2024, uwanja wa mpira wa Birikau shehia ya Michungwani, wilaya ya Chake chake Pemba, mara baada ya kuizindua barabara ya Kijangwani- Birikau, yenye urefu wa kilomita 4.2, ikiwa ni shamra shamra za miaka 60 ya mapinduzi Zanzibar. Alisema, kwa vile ujenzi wa miundombinu ya barabara za kisasa, ni miongoni mwa matunda ya mapinduzi, hivyo serikali anayoingoza imedhamiria kufanya jitihada za makusdi, za kuimarisha miundombinu hayo, katika maeneo ya mijini na vijijini kwa Unguja na Pemba. Alieleza kuwa, malengo hasa ya serikali ni kuziimarisha barabara zote zilizopo na kujenga nyingine mpya, katika maeneo ambayo barabra hazijafika, ili kuimarisha mtandao wa barabara hapa Zanzibar. Dk.

MKURUGENZI MKALIMOTO AONA MBALI JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO

  Na Maulid Yussuf, Zanzibar Mkurugenzi Idara ya Mipango, Sera na Utafiti, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi Daima Mohamed Mkalimoto amesema hatua ya uanzishwaji wa   Jukwaa la haki za watoto kwa wadau wanayoshughulikia maendeleo ya watoto itasaidia kuweka pamoja na kuunganisha shughuli za watoa huduma za watoto. Amesema hayo jana katika ukumbi wa UN Women wakati akifungua mkutano wa wadau wanaoshughulikia masuala ya Watoto kutoka taasisi za umma, binafsi na Washirika wa Maendeleo, ambapo mkutano huo ulilenga uanzishwaji wa Jukwaa la haki za Watoto Zanzibar. Bi Daima amesema hatua hiyo itasaidia kuwaweka pamoja wadau hao katika uratibu wa utekelezaji wa shughuli zinazogusa Maendeleo ya watoto nchini. Hivyo amewaomba wadau hao kutoa maoni yao ili yafanyiwe kazi na kuingizwa katika mapendekezo ya kuanzishwa kwa jukwaa hilo. “Kuna umuhimu wa uratibu na usimamizi wa pamoja wa uanzishwaji wa jukwaa la haki ya watoto ili kuweza kutoa huduma bora za watoto katik

BALOZI SEIF, MAONESHA CHACHU YA MAENDELEO NCHINI

 Na Mwandishi wetu, Zanzibar@@@@ Taasisi za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Binafsi zimetakiwa kuendelea kufanya maonesha ili kutangaza kazi zao pamoja na kukuza uchumi wa nchi, kuleta maendeleo, sambamba na kuinua kipato cha mtu mmoja mmoja na Taifa kiujumla.  Kauli hiyo imetolewa na Makamo wa Pili wa Rais Mstaafu Balozi Seif Ali Iddi huko Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Kisonge, Unguja mara baada ya kuyapokea maonesho yaliyopita kwa njia ya kutumia magari ikiwa ni shamrashamra katika kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar. Amesema iwapo maonesho hayo yataendelezwa na kudumishwa yatasaidia taasisi hizo kutangaza kazi zao pamoja na kukuza uchumi wa nchi, kuleta maendeleo, sambamba na kuinua kipato cha mtu mmoja mmoja na hatimae pato la taifa kuongezeka. Hivyo Mhe. Balozi Seif ameitaka Afisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji kuendelea kusimamia maonesho ya kazi zinazofanywa na taasisi mbalimbali za Serikali na Binafsi ili kutoa fursa kwa wananchi kuweza k

DK. MWINYI AWEKA JIWE LA MSINGI NYUMBA ZA MADAKTARI MKOANI, AAHIDI UJENZI WA HOSPITAL YA RUFAA KILA MKOA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema ujenzi wa nyumba za madaktari karibu na hospitali, kutaondoa adha kwao na wagonjwa, kwa kumudu kutoa huduma saa 24. Dk. Mwinyi aliyasema hayo Disemba 3, mwaka 2024, uwanja wa mikutano bandarini Mkoani, mara baada ya kuziwekea jiwe la msingi, nyumba za madaktari zilizopo hospital ya Abdalla Mzee Mkoani Pemba, ikiwa ni shamra shamra za kuelekea miaka 60 ya mapinduzi Zanzibar. Alisema, nyumba hizo zitakapokamilika, zinatarajiwa kuondoa usumbufu kwa madaktari hao na wagonjwa wanaokwenda hospitali, kwa kule kuwa karibu na sehemu zao za kazi. Alieleza kuwa, serikali pia itapunguza gharama za kuwafuata madaktari kwenye maakazi yao ya uraiani, pale inapotokezea wagonjwa wa dharura, hasa nyakati za usiku. ‘’Leo (jana) tumeshaziwekea jiwe la msingi nyumba za madaktari wetu, ni matumaini yetu sasa huduma zote za kitabibu, zitapatikana saa 24, kwa vile madaktari watakuwa

WAZIRI SHAMATA AZINDUA OFISI YA ELIMU MKOANI ATAMANI UFAULU UPAE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAZIRI wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Shamata Shaame Khamis, amesema kukamilika kwa ofisi ya kisasa ya elimu wilaya ya Mkoani Pemba, iwe chachu ya kuongeza ufaulu na ufuatiliaji wa masomo, wilayani humo. Waziri Shamata aliyasema hayo Disemba 2, 2024 mara baada ya ufunguzi wa ofisi hiyo, ikiwa ni sehemu za shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar ya mwaka 1964. Alisema, tokea kufanyika kwa mapinduzi hayo, hakujawahi kuwa na ofisi mpya na ya kisasa ya elimu ya wilaya, ambapo wakati huo watendaji hao walikuwa wakifanyakazi katika mazingira magumu. Alieleza kuwa, kama sasa imeshajengwa ofisi ya kisasa na yenye vifaa vipya, iwe chachu ya kuongeza ufaulu na suala la ufuatiliaji wa masomo kwa wilaya ya Mkoani. ‘’Leo (jana) tumeshaifunfua ofisi mpya na ya kisasa, hivyo ni matumaini yangu kuwa, itakuwa chachu ya kuongeza ufaulu, lakini pia suala la kufanya ufuatiliaji kwa skuli mbali mbali wilayani humo,’’alieleza. Katika hat

WAKULIMA MAZAO YA BIASHARA MKOANI WAAHIDI KULITUMIA SOKO JIPYA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA WAKULIMA wa mazao ya kilimo cha biashara ikiwemo ndizi, chungwa na muhogo, wa shehia za Mtambile, Mizingani, Chumbagaeni na Wambaa wilaya ya Mkoani Pemba, wamahidi kulitumia soko jipya la Mtambile, ili kuongeza thamani ya biadhaa zao.   Walisema, kwa sasa wamepata mkombozi wa bidhaa zao, na hwenda ikiwa ndio mwisho wa kulanguliwa na wachuuzi wa bidhaa mbali mbali wanaosafirisha nje ya Pemba, kw akule kuwalalia kibei. Wakizungumza na mwandishi wa habari mara baada ya kufunguliwa kwa soko hilo, na Waziri wa Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar Shamata Shaame Khamis, walisema kwa vile wameshakabidhiwa, sasa ni kulitumia kwa kuuzia bidhaa zao. Mmoja katuia ya wakuliuma hao anaejishughulisha na kilimo cha ndizi za mtwike, pukusa na koroboi Haji Kassim Khamis wa Mtambile, alisema sasa baada ya kuvuna atakimbila kwenye mdana sokoni hapo. ‘’Kwa vile tumeshaelezwa kuwa, mnada wa bidhaa kama za ndizi utakuwepo, sitouza tena ndizi zangu chochoroni na kulal

WAZIRI RIZIKI PEMBE AIPA TANO PBZ

  Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na watoto Mhe. Riziki Pembe Juma ameipongeza Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Kwa Kazi kubwa waliyoifanya ya kuingizia faida ya Bilioni 78 Kwa mwaka 2023 kulinganisha na Bilioni 22 Kwa mwaka 2022 Jambo ambalo litasaidia kuipatia gawio kubwa Serikali. Akitoa kauli hiyo wakati wa ufunguzi wa Tawi la Benki ya Watu wa Zanzibar, (PBZ) huko Nungwi Wilaya ya Kaskazini 'A,' Unguja ikiwa ni miongoni mwa Shamrashamra ya Maadhimisho ya Miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar .   Amesema mafanikio hayo yanatokana na miongozo ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi kupitia Wizara ya Fedha na Mipango Kwa kusimamia na kujenga vianzio vingi vya fedha.  Aidha amesema Benki hiyo imeweza kutoa mikopo ya Trilioni moja Kwa wateja wake na kuendeleza kuwa kiungo muhimu katika Taifa, ndani ya Zanzibar na Tanzania Bara kiujumla.    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango. Dkt. Juma Malik amesema  Sera miongozo pamoja

'WANAWAKE WAJASIRIAMALI WAANZISHIWA CHOMBO CHA KUDAI HAKI ZAO'

  NA MCHANGA HAROUB, WMJJWW-PEMBA IMEELEZWA kuwa, uanzishwaji wa jukwaa la wanawake wajasiriamali, kutasaidia kwa kiasi kikubwa kutatua changamoto zinazowakabili akina mama hao, katika shehia mbali mbali Zanzibar .   Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Siti Abass Ali, wakati akizungumza kwa nyakati tofauti, na wajasiriamali wanawake wa wilaya nne za Pemba.   Alisema pamoja na juhudi kubwa inayochukuliwa na Serikali katika kumuendeleza mwanamke, lakini bado imeonekana kuna baadhi ya maeneo yamekuwa ni kikwazo kufikia maendeleo yaliokusudiwa.   Alieleza kuwa, pamoja na hayo, anaamini uanzishwaji wamajukwaa hayo, inaweza kuwa endelevu, ili kuwainua kiuchumi wanawake na hatimae taifa kwa juma.   Mkurugenzi huyo alifahamisha kuwa, uwepo wa majukwaa hayo kutatoa fursa kwa akina mama, kupata chombo madhubuti cha kuzungumza pamoja na kuwa na sauti moja wanapotafuta dawa ya changamoto zao.   Mkurugenzi Siti aliwasisitiza akina mam