Skip to main content

Posts

Showing posts from April 10, 2022

DK. MWINYI AKIWA PEMBA AWAPA FUTARI WANANCHI

           NA HANIFA SALIM, PEMBA  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema kila mwenye uwezo anawajibu wa kutoa sadaka kwa kuwasaidia ambao hawana uwezo hususani katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani. Alisema katika mwezi huu mtukufu wafadhili wengi wamejitoa katika kuwasaidia watu ambao wana hali duni za kimaisha, hivyo aliwataka wananchi wenye uwezo kujitolea kutoa sadaka kwa wenzao ambao wako katika mazingira magumu. Aliyasema hayo kwa nyakati tofauti, katika hafla ya kukabidhi msaada wa futari kwa wazee, mayatima, wajane na watu wenye ulemavu kwa Mkoa wa Kusini Pemba, iliyofanyika ofisi ya Mkuu wa wilaya Mkoani na Tibirinzi Chake chake. "Ni kweli wanaopata ni wachache na wanaohitaji ni wengi, lakini hii ni taasisi moja tu zipo na taasisi nyengine ambazo zimesaidia, ikiwemo kampuni ya Olympic na mashirika mengi yamesaidia kwa Wilaya ya Micheweni na Wete", alisema. Dk. Mwinyi alisema, kwa niaba ya serikali ya Mapinduzi

WANAWAKE KISIWA CHA FUNDO PEMBA WATAKA KITUO CHA POLISI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA WANAWAKE wa kisiwa kidogo cha Fundo wilaya ya Wete Pemba, wamesema umbali wa kilomita zaidi ya 60 kwa usafiri wa baharini kutoka kisiwani hapo, hadi kilipo kituo cha Polisi Wete, ni moja ya changamoto zainazowafanya wasiyaripoti mara kwa mara, matukio ya kihafalifu wanayofanyiwa. Wamesema wamekuwa wakifanyiwa vitendo viovu kama vile kuharibiwa mitego yao, kilimo chao cha mwani na kisha kutukanwa, ingawa wamekuwa na uzito kukifuata kituo cha Polisi Wete. Walisema, suluhushi la wao kuyaripoti matendo wanayofanyiwa na vijana wa kisiwa hicho, ni kujengewa kituo kidogo cha Polisi ili karibu yao. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kisiwani hapo, walisema hawaishi kwa amani na utulivu kama walivyo wanawake wengine vijiji vyengine, kutokana na kutishiwa hata usalama wao. Mmoja kati ya wanawake hao Mwajuma Rashid Salmin, alisema wanapoharibiwa mashamba yao ya mwani na vijana kisha hurejea kuwatukana. Alieleza kuwa, pamoja na hivyo, wamekuwa wakiwatishia