Skip to main content

Posts

Showing posts from April 30, 2023

MZEE MIAKA 70, AFARIKI AKIWA KWENYE FOLENI KUTAKA MAJI YA TIBA MSUKA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ABRAHMAN Juma Abdalla miaka 70, mkaazi wa kijiji cha Kuyuni wilaya ya Mkoani, ameanguka ghafla na kufariki dunia papo hapo, akiwa kwenye foleni ya kuchukua maji ya kiimani katika bahari ya Msuka, wilaya ya Micheweni kisiwani Pemba. Itakumbukuwa kua, eneo hilo lilishafukiwa na kupigwa marufuku na serikali, kuwataka wananchi wasiyatumie maji hayo, kwa kutokuwa salama kiafya. Pamoja na marufuku hiyo, imeabainika kuwa wapo baadhi ya wananchi, wamekuwa wakilitumia eneo hilo na kuchota maji ya kiimani, yanayodaiwa kuponyesha magonjwa na maradhi sugu. Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, walisema mpatwa na mauti, alifika shehia ya Msuka mashariki leo Mei 6, mwaka huu majira ya saa 3:00 asubuhi, akitokea kijijini kwao Kuyuni wilaya ya Mkoani. Walisema, mzee huyo alifika eneo hilo, akikabiliwa na magonjwa sugu, ili kuchukua maji hayo, ambayo alikuwa anaamini, yanaweza kumponyesha magonjwa yake. Mmoja kati ya mashuda hao Omar Kije Omar alisema, mzee huyo

WANANCHI MTEGA WAWI WAKARABATI BARABARA YAO KWA MATOFALI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA @@@@ WANANCHI wa kijiji cha Mtega, shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake Pemba, wameamua kuikarabati barabara yao yenye urefu wa kilomita 2.5, kwa kutumia matofali ya fuuwe na mawe, baada ya kuharibika kwa mvua, inayoendelea kunyesha. Mwandishi wa habari hizi, aliwashuhudia wananchi hao, wakiwa kwenye eneo la barabara hiyo, wakiikarabati barabara hiyo, kwa kutumia vipande vya matofali na mawe, ili iweze kupitika. Wananchi hao walisema, uamuzi huo umekuja kufuatia kukosa misaada kutoka mamla husika, hali iliyopekea mvua kuathiri barabara yao. Mwenyekiti wa kamati ya maendeleo ya kijiji hicho, Khamis Haji, alisema barabara hiyo imeharibika mno, kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha nchini kote. Alieleza kuwa, juzi Mei 4, kamati iliikagua barabara hiyo, na kufikia uamuzi wa kutafuta matofali na mawe, ili kuikarabati katika maeneo, yalioathiriwa zaidi na mvua. ‘’Hivi sasa, kama atatokezea mgonjwa ama mzazi anataka kwenda hospitali, inabidi tutumie gari za Ng

MAABARA YA AFYA YA JAMII PEMBA YAONGEZEWA UWEZO KUGUNDUA MAGONJWA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ WAZIRI wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui amesema, Maabara ya Afya ya Jamii Pemba sasa ina uwezo wa kuchunguza maambukizi mapya na kufanya ufuatiliaji wa magonjwa yenye umuhimu wa afya ya jamii kwa kutumia njia ya kisasa ya kugundua maradhi 'Next General Sequencing (NGS). Akizungumza mara ya kufungua maabara ya kisasa Wawi Chake Chake Pemba Waziri huyo alisema kuwa, kuwepo maabara hiyo itasaidia kuchunguza maradhi mbali mbali ndani ya kisiwa cha Pemba, jambo ambalo ni faraja kubwa. Alisema kuwa, awali Wizara ya Afya ilikuwa ikisafirisha sampuli za maradhi nje ya kisiwa cha Pemba jambo ambalo ilikuwa likiwapa usumbufu kwani majibu yalikuwa yanachelewa na kushindwa kugundua kwa haraka maradhi anayougua mgonjwa. ‘’Kwa kweli tupepata faraja kubwa sana kwa sababu sasa maradhi kama Uviko 19, Ebola na magonjwa mengine yatachunguzwa katika mabara hii ya Wawi Chake Chake Pemba, hivyo wataalamu na watendaji wazilinde na kuzitunza mashine kwa kuweka mazin

'JUMAWAKIPE' YAKANUSHA KUWATAFUTIA WAUME WA OMAN WANACHAMA WAO PEMBA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ JUMUIYA ya Maendeleo ya Wanawake wa Kiislamu Pemba (JUMAWAKIPE)imekanusha tangazo lililosambaa katika mitandao ya kijamii kwamba, Jumuiya hiyo inawataka Waomani wanaotaka kuoa, wafike kisiwani Pemba kwani wanawake wapo kuanzia miaka 18 hadi 35. Jumuiya hiyo imesema kwamba, tangazo hilo ni la kupuuzwa kwani waliosambaza ujumbe huo ilijiita ni Jumuiya ya Wanawake Pemba na sio Jumuiya ya Maendeleo ya Wanawake wa Kiislamu Pemba, jambo ambalo si katika akhlak za kiislamu kumnadisha mwanamke katika mtindo huo. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Amira wa Jumuiya hiyo Asya Amour Abdulrahman alisema kuwa, wanalaani kitendo hicho kilichofanywa na Jumuiya hiyo ya Wanawake Pemba, ambapo wao kama Jumuiya ya JUMAWAKIPE wanakanusha kusambaza ujumbe huo. Alisema kuwa, ujumbe uliosambaa mitandaoni ulisomeka kuwa ‘Jumuiya ya wanawake Pemba inapenda kuwajulisha Waomani wote wanaotaka kuoa yakwamba wapo wanawake kuanzia umri wa miaka 18 hadi 35 wakiwa bikira kwa gh

ELIMU YA CHANJO YA UVIKO19, KUNDI LA VIZIWI LALAMIKIA KUSAHAULIWA

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MKATABA wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu, ambao Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliusaini Machi mwaka 2007 na kuthibithisha mwaka 2009, unalazimisha huduma za afya kwa watu wenye ulemavu. Ibara ya 25, inasisitiza nchi wanawachama , watumbue kuwa, watu wenye ulemavu wanayo haki ya kunufaika kwa kiwango cha juu, huduma za afya tena bila ya ubaguzi wowote. Mkataba ukafafanua kuwa, nchi husika zitachukua hatua zinazostahiki, kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata huduma bora za afya. ‘’Nchi wanachama zitatoa huduma za afya, zinazohitajika kwa watu wenye ulemavu, hasa kutokana na aina ya ulemavu wao, yakiwemo maeneo ya vijijini,’’umefafanua Mkataba huo. Ukaongeza kuwa, nchi hizo zitawataka wataalamu wa afya, kutoa huduma za kiwango sawa kama watu wenye ulemavu, kama zinavyotolewa kwa watu wengine, ikiwa ni pamoja na misingi ya kutoa ridhaa kwa uhuru na ufahamu wa kutosha. Mwaka 1983 hadi 1992 hatua mbali mbali zilichukuliwa, iki

MWARUBAINI HUU HAPA WA KUMALIZA TABIA YA KUWAUWA WATUHUMIWA ZANZIBAR

    I NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘’ATAKAYE muua mwenzake, basi naye anyongwe, na kinga kuwa alikuwa na hasira isifanye kazi, yakifanyika hayo, kujichukulia sheria mikononi itakoma,’’wanasema wahanga wa matukio hayo. WAHANGA WANATOA RAI GANI? Mke ambaye muume wake aliuawa mwaka 2020 eneo la Micheweni kwa wananchi waliodaiwa kuwa na hasira, anasema njia pekee ya kuondoa utamaduni wa wananchi kujichukulia sheria mikononi, naye ni kuuliwa. Kijana Issa Haji Othman wa Mwanakwerekwe, anasema njia nyingine ya kukomesha wananchi kujichukulia sheria mikononi, ni kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria. Mayasa Haji Mzee wa Chake chake, anasema ili kukomesha wananchi kujichukulia sheria mikononi, ni wananchi kuelezwa mifumo ilivyo ya haki jinai. ‘’Wananchi hawaelewi kwa undani, mifumo ya haki jinai, kuanzia kesi inapokuwa Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka hadi Mahkamani pamoja na haki ya dhamana au rufaa,’’anasema. VYOMBO VYA KUSIMAMIA HAKI JINAI VINASEMAJE ?

SIKU YA URITHI AFRIKA YAADHIMISHWA PEMBA , RC KUSINI ASEMA JAMBO

  NA MARYAM SALUM, PEMBA@@@@ WANANCHI Kisiwani Pemba wametakiwa kuonesha ushirikiano kwa Serikali,   juu ya   jitihada zinazofanywa na viongozi wa nchi katika kusaidiana   kuenzi urithi, ili kizazi kilichopo na kijacho kiweze kufaidika. Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Massoud wakati akizungumza na wanachama wa jumuia ya Urithi Pemba   pamoja na wafanyakazi mbali mbali katika kilele cha maadhimisho ya siku ya Urithi duniani Afrika,ambapo kitaifa kwa pemba kilele kimefanyika tenis Chake Chake. Alisema kuwa Serikali ya Tanzania Bara na ya Zanzibar kupitia Viongozi wake ilifanya jitihada za makusudi kwa kuandaa kipindi maalum cha kutangaza utalii duniani kama urithi wa afrika. Alisema kuwa kutokana na jitihada zinazonywa na viongozi hao wananchi ipo haja kwa   kuunga mkono jitida hizo ili lego liweze kufikiwa.   “Viongozi wetu wakuu akiwemo Rais wa Jamuhuri ya Tanzania Dk. Samia na Dk. Huseein Mwinyi kwa kushirikiana wameandaa mpango maalum wa ku