NA TATU MAKAME, ZANZIBAR @@@@
MAMLAKA ya mapato Tanzania (TRA) Tanzania imesema itaimarisha mazingira mazuri kwa wafanyabiashara kuondosha vikwazo kwao.
Kamisha mkuu wa Mamlaka hiyo Salehe Juma Mwenda alisema hayo wakati wa kikao cha pamoja kilichowashirikisha watendaji wa mamlaka za kodi Tanzania pamoja na wafa nyabiashara hao kilichofanyika huko hoteli ya Madinat Al bahri Mbweni Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja wenye lengo kusikiliza changamoto za wafanyabiashara.
Alisema miongoni mwa mikakati hiyo kuondosha vikwazo kwa wafanyabiashara kwa kutoa ushirikiano kwa wafanyabiashara kila kunapotokuwa vikwazo kwenye uingizaji wa biashara hapa nchini.
Mwenda alitumia nafasi hiyo kueleza kuwa mkakati mwengine kuziruhusu bandari za Fumba Unguja na Mkoani Pemba kushusha mizigo inayotoka moja kwa moja nje ya nchi kinyume ilivyo sasa mizigo hiyo kushushwa Mombasa Kenya.
Alisema ujenzi wa bandari hizo unakwenda kwa kasi na zitakapokamilika bandari hiyo zitafanya kazi kama bandari nyengine.
"Ujenzi wa bandari hizi unakwenda kwa kasi tuwapongeze viongozi wetu wakuu akiwemo Rais wa Jamuhuri ya Muumgano wa Tanzanzi Dk Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Hussein Ali Mwinyi kwa kujenga miundombinu bora ya kufanyia biashara.
Mwenda alisisitiza kuwa serikali itaondosha vikwazo vyote kwa wafabyabiashara pamoja kusikiliza changamoto zao ili wafanye kazi zao bila usumbufu.
Alisema kuwa lengo kuona taasisi za kodi zinaongeza mapato ili kwenda sambamba na matakwa ya serikali ya kuongeza ukusanyaji wa kodi.
Aliongeza kuwa kuondosha vikwazo ni njia bora ya kuongeza mapato na kueleza kuwa kwa mwaka wa fedha 2025/2026 makusanyo kwenye mamlaka yaliongezeka na kufikia asilimia 36.
"Kwa mwaka wa fedha 2025/2026 Mamlaka hiyo ilikusanya bilioni 828 sawa na asilimia 99 na tulikusudia kukusanya bilioni 825 na kiwango hili tulivuka malengo tuliyojipangia", alisema.
Nae Naibu Kamishna wa mamlaka ya Mapato Tanzania upande wa Zanzibar Saleh Haji Pandu aliwahakikishia wafanyabiashara kuwa mamlaka hiyo itazifanyia kazi changamoto zilizotolewa na wafanyabiashara ili kuona vikwazo vyote vinaondoka kwenye usafirishaji wa bidhaa.
Kwa upande wake Kamishna wa Kodi za ndani Michael Muhoja alisema mamlaka zitahakikisha kila mfanyabiashara analipa kodi kwa wakati ili kuona serikali inakusanya kodi pamoja na kulinda biashara za wafanyabiashara hao.
Nae kamishna wa kodi za ndani Tanzania Juma Bakar aliwataka wafanyabiashara kulipa kodi kwa wakati ili kuondosha vikwazo kwa wafanyabiashara.
Aidha alisema wataboresha mifumo kurahisisha usimamizi wa kodi na kutimiza wajibu wa kusimamia kodi kwa wafanyabiashara wote.
Aidha alisema mamlaka inawajengea uwezo watendaji wa mamlaka hiyo ili kutoa huduma bora kwa wafanyabiashara.
Nao wafanyabiashara waliitaka mamlaka hiyo kuruhusi wafanyabiashara kulipa kodi kodi sehemu moja ili kupunguza utitiri wa kodi kwa wafanyabiashara.
Hata hivyo waliomba kuruhusu meli za mizigo kushusha Zanzibar kinyume na zinavyoshusha mizigo bandari ya Mombasa kwa sasa hali inayochelewesha mizigo kuingia nchini kwa wafanyabiashara.
Comments
Post a Comment