Skip to main content

TRA: 'TUNAENDELEA KUIMARISHA MAZINGIRA RAFIKI KWA WAFANYABIASHARA WAOTE'

 


NA TATU MAKAME, ZANZIBAR @@@@

 MAMLAKA ya mapato Tanzania (TRA) Tanzania imesema itaimarisha mazingira mazuri kwa wafanyabiashara kuondosha vikwazo kwao. 

Kamisha mkuu wa Mamlaka hiyo Salehe Juma Mwenda alisema hayo wakati wa kikao cha pamoja kilichowashirikisha watendaji wa mamlaka za kodi Tanzania pamoja na wafa nyabiashara hao kilichofanyika huko hoteli ya Madinat Al bahri Mbweni Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja wenye lengo kusikiliza changamoto za wafanyabiashara.

 Alisema miongoni mwa mikakati hiyo kuondosha vikwazo kwa wafanyabiashara kwa kutoa ushirikiano kwa wafanyabiashara kila kunapotokuwa vikwazo kwenye uingizaji wa biashara hapa nchini.

Mwenda alitumia nafasi hiyo kueleza kuwa mkakati mwengine kuziruhusu bandari za Fumba Unguja na Mkoani Pemba kushusha mizigo inayotoka moja kwa moja nje ya nchi kinyume ilivyo sasa mizigo hiyo kushushwa Mombasa Kenya.

Alisema ujenzi wa bandari hizo unakwenda kwa kasi na zitakapokamilika bandari hiyo zitafanya kazi kama bandari nyengine.

"Ujenzi wa bandari hizi unakwenda kwa kasi tuwapongeze viongozi wetu wakuu akiwemo Rais wa Jamuhuri ya Muumgano wa Tanzanzi Dk Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Hussein Ali Mwinyi kwa kujenga miundombinu bora ya kufanyia biashara.

Mwenda alisisitiza kuwa serikali itaondosha vikwazo vyote kwa wafabyabiashara pamoja kusikiliza changamoto zao ili wafanye kazi zao bila usumbufu.

Alisema kuwa lengo kuona taasisi za kodi zinaongeza mapato ili kwenda sambamba na matakwa ya serikali ya kuongeza ukusanyaji wa kodi.





Aliongeza kuwa kuondosha vikwazo ni njia bora ya kuongeza mapato na kueleza kuwa kwa mwaka wa fedha 2025/2026 makusanyo kwenye mamlaka yaliongezeka na kufikia asilimia 36.

"Kwa mwaka wa fedha 2025/2026 Mamlaka hiyo ilikusanya bilioni 828 sawa na asilimia 99 na tulikusudia kukusanya bilioni 825 na kiwango hili tulivuka malengo tuliyojipangia", alisema.

Nae Naibu Kamishna wa mamlaka ya Mapato Tanzania upande wa Zanzibar Saleh Haji Pandu aliwahakikishia wafanyabiashara kuwa mamlaka hiyo itazifanyia kazi changamoto zilizotolewa na wafanyabiashara ili kuona vikwazo vyote vinaondoka kwenye usafirishaji wa bidhaa.

Kwa upande wake Kamishna wa Kodi za ndani Michael Muhoja alisema mamlaka zitahakikisha kila mfanyabiashara analipa kodi kwa wakati ili kuona serikali inakusanya kodi pamoja na kulinda biashara za wafanyabiashara hao.

Nae kamishna wa kodi za ndani Tanzania Juma Bakar aliwataka wafanyabiashara kulipa kodi kwa wakati ili kuondosha vikwazo kwa wafanyabiashara.

Aidha alisema wataboresha mifumo kurahisisha usimamizi wa kodi na kutimiza wajibu wa kusimamia kodi kwa wafanyabiashara wote.



Aidha alisema mamlaka inawajengea uwezo watendaji wa mamlaka hiyo ili kutoa huduma bora kwa wafanyabiashara.
 
Nao wafanyabiashara waliitaka mamlaka hiyo kuruhusi wafanyabiashara kulipa kodi kodi sehemu moja ili kupunguza utitiri wa kodi kwa wafanyabiashara.



Hata hivyo waliomba kuruhusu meli za mizigo kushusha Zanzibar kinyume na zinavyoshusha mizigo bandari ya Mombasa kwa sasa hali inayochelewesha mizigo kuingia nchini kwa wafanyabiashara.

MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...