Skip to main content

Posts

Showing posts from August 18, 2024

WANAFUNZI CONNECTING: 'ZITUMIENI WIKI ZILIZOBAKI KABLA YA MTIHANI WA TAIFA MTAFANIKIWA''

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MWALIMU Mkuu wa skuli ya sekondari ya Connecting Continent, iliyopo Mgogoni wilaya ya Chake chake Pemba, Mwache Juma Abdalla, amewataka wanafunzi wa darasa la kumi na mbaili skulini hapo, kuzitumia kwa maandalizi ya hali ya juu, wiki 11 zilizobaki, kabla ya kufanya mtihani wao wa taifa. Alisema, wiki hizo sio kidogo, kwa mwanafunzi kama ataweka pembeni uvivu, kudorora, kushughulikia anasa na kujikita kwenye masomo, hivyo anaweza kufanya vizuri, kwenye mtihani wa taifa. Mwalimu mkuu huyo, aliyasema hayo leo Augost 24, 2024 skulini hapo, kwenye kikao cha wazazi na wanafunzi hao, cha kutoa matokeo ya mitihani ya majaribio ya kimkoa ‘MOCK’ yaliofanyika hivi karibuni. Alisema, bado wanafunzi wanayonafasi ya kujiandaa na mitihani hayo, kwani waalimu wameshamaliza mtaala waliopangiwa, na sasa ni kazi wanafunzi wenyewe. Alieleza kuwa, waalimu wamekuwa wakitumia jitihada binafsi ili kuhakikisha wanamaliza mitaala mapema, na sasa ni kazi ya wanafunzi kuang

FOMU YA KUOMBA KUGOMBEA NAFASI YA MKURUGENZI CHAPO

                                                                             FOMU YA KUOMBEA NAFASI YA MKURUGENZI WA JUMUIA YA WASAIDIZI WA SHERIA CHAKE CHAKE – CHAPO   NB: MALIPO YA FOMU HII NI SHILINGI 2,500/. JINA LA MUOMBAJI: …………………………………………………………………………………                                                                    UMRI ……….. JINSI ………… SHEHIA ……………………………………. JIMBO …………………………….. TAREHE YA KUZALIWA …………/……………./……..………. PAHALA …………………………………………………. TAREHE YA KUCHUKUA FOMU ……………………….……./………….... .............../……………………………… NAFASI UNAYOSHIKA KWA SASA NI……………………………………………..KWA MUDA GANI…………… NAMBARI YA UWANACHAMA………………………………MWAKA ULIOJIUNGA ………………………………     UDHAMINI KATIKA KUOMBA NAFASI HII a)        Jina la Mdhamini wako………………………………………………………………Jinsi………………………………. b)       Nambari ya simu…………………………………………….. c)        Shehia anayoishi………………………………………………………Jimbo…………………………………………….. d)       Saini………………………………………………………

‘UWT’ KUSINI PEMBA: '‘ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WETU ILIKUWA YA KISAYANSI’

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ UONGOZI wa Umoja wa wanawake wa CCM ‘UWT’ mkoa wa kusini Pemba, umesema ziara iliyofanywa hivi karibuni na Makamu Mwenyekiti wa umoja huo taifa Zainab Khamis Shomari, imekuwa ni darsa tosha, kuelekea ushindi wa CCM hapo mwakani.   Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa umoja huo mkoani humo, Zuwena Khamis Abdalla, alipokuwa akizungumza hivi karibuni, kufuatia kumalizika kwa ziara ya Makamu Mwenyekiti huyo, mkoani mwake.   Alisema ujio wake, umewaamsha na kuendeleza mbele umoja huo na chama kwa ujumla, kwani ametoa maagizo ambayo kama yakifanyiwa kazi, CCM itaendelea kuweka historia ya ushindi katika kila uchaguzi.   Alieleza kuwa, moja ambalo wanalikumbuka ni kuwataka viongozi wa UWT mkoa, wilaya na hadi shina kuhakikisha wanaongeza idadi ya wanachama wa CCM.   Alifahamisha kuwa, hilo ni jambo la msingi ndani ya UWT, na hivyo ni lazima viongozo wote hadi ngazi ya mkoa, kulitekeleza kwa vitendo agizo la Makamu Mwenyekiti huyo. ‘’Ni kweli zia

RAMLA: MWANAMKE ANAYEPAMBANIA SOKA KWA WANAWAKE, APITIA CHANGAMOTO LUKUKI

  NA HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@ ‘MWANZO wa kuanza mchezo huu, nilipata changamoto kubwa na kuambiwa nacheza mchezo wa kiume, wa kihuni lakini sikuvunjika moyo’. Hayo ni maneno ya kocha wa mpira wa miguu timu ya Mkoani Qunes, Ramla Khamis Juma aliyenza kwa kutandaza soka hapo awali. Kocha Ramla   aliyasema maneno hayo wakati akizungumza na makala haya huko katika uwanja wa mpira wa miguu Mpikatango Mkoani kisiwani Pemba, wanapofanyia mazoezi. Akinisimulia sababu ya kupenda michezo ni pale alipokuwa skuli ya msingi Ngwachani, akiwa darasa la sita baada ya kuwaona wanafunzi wenzake wakishiriki michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa pete ‘netball’. Wakati akiingia skuli ya Sekondari Uweleni, alikuwa anachezea timu ya netball ya wilaya, ndipo hapo hapo alipoanza kujifunza kucheza mpira wa miguu. “Kwa vile mchezo wa mpira wa miguu kwa wanawake, ilikuwa haujazoeleka wilaya ya Mkoani na ni ajabu, ambapo wengi walishangaa na kunikataza lakini haikuwa lolote mimi niliendelea kujifunza,”al

AZAM YAFUNGUA OFISI PEMBA

  NA HASINA KHAMIS, PEMBA @@@@ MKUU wa wilaya ya Chake Chake Pemba, Rashid Abdalla Ali, alisema uwepo wa Azam Tv, utawezesha kuibua vipaji viliopo kisiwani Pemba kwa vijana.   Alisema hayo wakati akifungua duka la wakala wa Azam Tv huko, eneo la Sukita mjini Chake chake, kisiwani Pemba.   Alisema tegemeo kwa vijana wa Pemba, juu ya uwepo wa ofisi kuu ya Azam Tv, ni kuimarisha kutangaza na kuvumbua vipaji vya wasanii, mbali mbali ikiwemo kuonesha tamthilia zao.   Aidha mkuu wa wilaya alisema "wananchi hawatakuwa na haja ya kusafirisha visimbuzi vyao nje ya kisiwa cha Pemba, kwa matengenezo badala yake kutumia vyema ofisi hiyo iliyofuguliwa kwa ajili yao,"alisema.   Nae Meneja wa mauzo na usafirishaji wa bidhaa, Adam Ndimbo, aliwahakikishia wananchi kuwa huduma zitatolewa kwa sawa nchi nzima, pamoja na kutoa elimu kwa wananchi.   Alisema changamoto zote za visimbuzi zimetatuliwa na kuwataka kuwa na imani na wakala wa hao kwa huduma bora na matengenezo bure

WADAU WATAJA DARZENI YA CHANGAMOTO ZINAZOWAKWAMISHA WATOTO WA WAKIKE MICHEZONI

  HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@ MICHEZO ni sehemu muhimu katika utamaduni wa kila jamii ya binadamu kote duniani. Michezo iko ya aina nyingi, ambayo jamii ya makabila tofauti hushiriki kutokana na utamaduni walionao na kwa madhumuni tofauti. Pamoja na michezo kuwa na faida lukuki, ikiwemo kupata ajira,   kujenga afya ya mwili na akili, kuburudisha, kuelimisha, kutambulisha, kujenga ukakamavu, kuonesha vipaji na kujenga urafiki, lakini bado jamii iko nyuma kwa hilo. Ingawa hakuna tamko linaloonesha kuwa watoto wa kike hawapaswi kushiriki katika michezo, ingawa bado hali haijaridhisha. Sera ya maendeleo ya michezo 2018 imeonesha hali ya sasa tangu kuanzishwa kwa wizara yenye dhamana ya michezo na baraza la michezo la taifa, maendeleo katika maeneo mbalimbali ya michezo yamepatikana. Sera hiyo haikumbaguwa mtu yoyote kushiriki michezo na kuonesha kuwa, michezo mingi mipya imaenzishwa na kuleta mafanikio makubwa kulingana na vipaji na uwezo walionao wananchi. Ambapo nayo Katiba ya

DC.MJAJA: ‘UHURU WA KUJIELEZA UNAMIPAKA YAKE’

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MKUU wa wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja, amesema ni lazima waandishi wa habari, wanasiasa na wanaasasi za kiraia, kuutumia vyema uhuru wa kujieleza, ili kuepusha madhara yanaoweza kujitokeza. Kauli hiyo ameitoa, ukumbi wa Chuo cha Samail Gombani Chake chake Pemba, wakati akifungua semina ya kijamii, kuhusiana na uhuru wa kujieleza, iliyoandaliwa na Jumuiya ya Waandishi wa habari Pemba ‘PPC’ kwa kushirikiana na Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari Tanzania ‘UTPC’ na kuwashirikishi waandishi wa habari, wanasiasa, jamii na viongozi wa dini. Alisema, ni kweli uhuru wa kujieleza ni haki ya kikatiba, na nivigumu mtu kumzuia kutoitumia haki hiyo, ingawa suala la tahadhari ya kukiuka mipaka, ni jambo la kuzingatia. Alieleza kuwa, waandishi wa habari hutumia vyombo vya habari kama tv, redio, magazeti na vile vya mtandaoni, ili kufikisha ujumbe kwa jamii husika. ‘’Hapa kwa eneo hilo, la kuzingatia zaidi ni, ili kuepusha machafuko ni kuhakikisha habari hizo kwa