Skip to main content

Posts

Showing posts from November 19, 2023

LFS, YAWAONESHA NJIA MAAFISA MAWASILIANO WA JUMUIYA ZA WASAIDIZI WA SHERIA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAAFISA mawasiliano na habari wa Jumuia za wasaidizi wa sheria Tanzania zimetakiwa kujenga ushirikiano wa karibu na watendaji wenzao, ili kuhakikisha wanakuwa na mifumo sahihi ya utoaji wa taarifa za jumuia. Hayo yameelezwa na Mtaalamu wa masoko kutoka LSF Gilsant Mlaseko, wakati akizungumza na maafisa   hao kwenye mkutano wa kujengewa uwezo kwa njia ya kielektroniki. Alisema bidhaa ya mwasiliano sio haki ya Afisa Mawasiliano na Habari pekee kwenye jumuiya, bali anatakiwa kuwa karibu na wakurugenzi, waratibu na watendaji wengine. Alieleza kuwa, wakati mwingine ndani ya Jumuiya Afisa huyo anaweza kuwa mwisho katika utoaji wa taarifa na hasa baada ya kuidhinishwa na kuthibitishwa na kamati iliyoteuliwa. ‘’Suala la mawasiliano hasa ya kutoka nje ya Jumuiya, linapaswa watoa taarifa wawe makini na sio jukumu la mtendaji mmoja, bali iwe ni timu ya Jumuiya na kisha muhusika anateuliwa,’’alieleza. Akieleza umuhimu wa mawasiliano Mtaalamu huyo, alisema ni

MJASIRIAMALI WA MBAO PEMBA AKERWA KUCHELEWESHEWA KIBALI UKATAJI MITI

  NA KHADIJA OMAR, PEMBA@@@@ MJASIRIAMALI wa uchongaji na utengenezaji wa bidhaa za miti, Mohamed Hamza Khamis wa Kuyuni shehia ya Ngwachani wilaya ya Mkoani, ameziomba mamla husika kutoa ruhusa ya haraka ya ukataji miti, mara wanapokamilisha taratibu.   Alisema, inawezekana kufuata taratibu zote kuanzia kwa sheha hadi Idara ya misitu, kwa ajili ya kukata miti ya mbao ingawa changamoto ni ucheleweshaji wa utaji wa kibali husika.   Hayo yamelezwa na mjasiriamali huyo, wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizim kijijini hapo, juu ya changamoto anazopitia katika kazia yake.   Alisema, jambo hilo la kucheleweshwa kupewa kibali, humuwawia vigumu na kusababisha migogoro isiyokuwa ya lazima na wateja wake, kwani wanakuwa hawamuelewi.   Alieleza kuwa, kufanya hivyo wakati mwingine kunasababisha kumkimbizia wateja kwani, wengi wao hupenda kazi zao zifanywe kwa haraka mno.   ''Changamoto yangu kubwa ni kucheleweshwa kupewa kibali cha ukataji miti ya m

MIUNDOMBINU USHAHIDI WA KIELEKTRONIKI KAA LA MOTO MAHAKAMANI

  Na Mwandishi Wetu SHERIA ya ushahidi ya Zanzibar ya mwaka 2016 iliyoanza kutumika Januari 18, 2017, imeanzisha utaratibu maalum wa kisheria wa kupokea ushahidi wa kielektroniki. Sheria inatoa uhakika katika kupokea na kukubali ushahidi wa kielektroniki. Kifungu cha 71 hadi 73 vya sheria vinaeleza jinsi ushahidi wa kielektroniki unavyoweza kukusanywa na kushughulikiwa. Uwepo wa sheria hii ni dhahiri kwamba ushahidi wa kielektroniki unaweza kutumika wakati wa uchunguzi wa kesi za udhalilishaji wa kijinsia. Hata hivyo, utekelezaji unafanywa kwa kiwango kisichoridhisha sana, hali inayosababisha waathirika kutopata haki kwa wakati. Aidha, wakati sheria inaruhusu wapelelezi kukusanya ushahidi wa kielektroniki, polisi bado hawana ujuzi wa kutosha wa jinsi ya kukusanya ushahidi wa kielektroniki. Ofisa wa makosa ya mtandao kutoka Jeshi la Polisi Zanzibar, Issa Mohamed Salum, "Hatujapewa mafunzo ya kukusanya ushahidi wa kielektroniki. Bado tunaandika maelezo ya waathiriwa kwenye karatasi.

WAZAZI WENYE WATOTO THAMARAT NISSAI WAKUMBUSHWA JAMBO

  NA ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@ UONGOZI wa skuli ya kiislamu Thamaratu-nnisai iliyopo Machomane wilaya ya Chake chake Pemba, imewakumbusha wazazi na walezi, kulipa ada zao kwa wakati, ili kurahisisha ufanisi wa usomeshaji skulini hapo. Akizungumza na wazazi na walezi wenye wanafunzi skulini hapo, Mwalimu Mkuu wa skuli hiyo Bimkubwa Habibu, alisema wapo baadhi ya wazazi, bado wamenakuwa wazito kulipa ada za watoto wao.   Alieleza kuwa, hilo linachangia uzoroteshaji wa skuli hiyo, ikiwemo usomeshaji na hata malipo ya mishahara ya waalimu walipo skulini hapo, ambao wanazitegemeza ada hizo.   ‘’Nyinyi wazazi na walezi, ambao mmewaleta watoto wenu skulini hapa, jambo la kwanza mhakikishe suala la ada halichelewi, maana ndio tegemezi kuu, kwa maendeleo yote ya skuli hii,’’alieleza.   Aidha Mwalimu Mkuu huyo amewakumbusha wazazi na walezi hao kuwa, wakumbuke kuwa, skuli hiyo hina mfadhili, anaeiendesha bali inategemea mno ada watakazozilipa kwa ajili ya watoto wao.   Akizun

WAWAKILISHI WANAWAKE WAUPIGA MWINGINI MAJIMBONI, WATATUA CHANGAMOTO KWA 'MZO'

NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@   Katika majimbo mengi Unguja na Pemba ni kawaida kusikia malalamiko ya waliochaguliwa kuingia Baraza la Wawakilishi, Bunge na Udiwani nadra kuonekana, tafauti na walipohangaika kuchaguliwa.   Hii ilipelekea majimbo mengi kuzorota kimaendeleo kwa vile hapakuwepo watu waliohangaikia shida zao na kilichosikika ni wananchi kulalamika kwamba waliowachagua kupeleka mbele madai yao hawaifanyi kazi kama walivyotarajia.   Hali ilianza kubadilika hivi karibuni kutokana na kuibuka wanawake majasiri na wanaojituma kuhangaikia kero hizi baada ya kushika hatamu za uongozi katika ngazi mbali mbali.   Wapo watu waliodiriki kusema laiti zamani kungekuwa na wawakilishi wanawake kama hawa waliopo sasa, matatizo ya majimbo mengi yangepatiwa ufumbuzi na yangepungua.   Licha ya kuwepo viongozi wanawake wachache, lakini kazi waliyoifanya wengi wao ni kubwa na inathibitisha maelezo ya kwamba siku zote mama huwa na huruma na ndio maana wawakilishi wanawake wanatum