Skip to main content

Posts

Showing posts from August 28, 2022

‘PPC’ KLABU ILIYOWATOA MAFICHONI WAANDISHI WA HABARI PEMBA KIMAFUNZO

  NA HANIFA SALIM, PEMBA WAANDISHI wa habari ni watu muhimu katika jamii yoyote ile ulimwenguni. Maana moja ya majumku yao ambayo sio rahisi kufanya na kundi jengine la watu ni kule, kuelimisha, kuburudisha na kuhabarisha iwe kijamii, kisiasa,kiutamaduni na kiuchumi. Licha ya changamoto ambazo wanakumbana nazo katika utekelezaji wa majukumu yao, bado wana dhima kubwa ya kuipatia jamii taarifa ambazo zinatokezea kila siku. Pamoja na kadhia hiyo taasisi kama hizo za vilabu vyao, ‘Press Club’ huwa zinasimama wima, kuwatetea waandishi hao wanaokumbwa na madhila kadha. Mei 3 ya kila mwaka duniani kote, kunaadhishwa siku ya uhuru wa vyombo vya habari, ni siku muhimu kwa waandishi wa habari. Waandishi wa habari wamekuwa wakifanya kazi zao kwa mujibu wa katiba zote mbili, ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na Zanzibar ya mwaka 1984 ambazo   zinahimiza upatikanaji wa habari na kutowa habari kwa wananchi. Kwa kawaida kila jambo ambalo linamaslahi na watu ili liw

HAYA NDIO MAAJABU YA MAZIWA YA MAMA KWA MTOTO

    KUTOKA, PEMBA::::: KILA mwanzoni mwa wiki ya mwezi wa Agosti, ya kila mwaka, dunia huwa na wiki ya unyonyeshaji wa maziwa ya mama.   Lengo la wiki hii, huwa ni kusisitiza umuhimu wa maziwa ya mama kwa watoto wachanga na wadogo, kiafya.   Afya ni kitu muhimu katika maisha ya mwanadamu na kinyume chake, ni kuzalisha maradhi kadhaa yanayodhoofisha mwili na kiakili.   Katika kuhakikisha afya ya mwanadamu inaimarika, msingi wake huanzia tokea mtoto anapokuwa tumboni na mara anapozaliwa, kwa kuhakikisha anapewa mahitaji ya msingi ikiwemo maziwa ya mama.   Maziwa ya mama yana kinga kamili ikiwemo ya vitameni A vya kutosha ambavyo huwa ni kinga ya maradhi mbalimbali kwa mtoto mchanga.   Ingawa wapo baadhi ya akina mama hawapendi kunyonyesha na huamuwa kumuachisha ziwa mtoto mara tu, anapojifunguwa, kwa sababu tofauti ikiwemo kuhofia maziwa yake kuanguka, kupoteza haiba na muonekano wake.   Katika hatuwa ya kumlisha mtoto chini ya miezi sita kunaweza kumsababis

MAKAMU WA PILI AKIWA PEMBA, AWAPA DARSA WAALIMU WAKUU

                                                  NA ZUHURA JUMA,  PEMBA   MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdullah amewataka walimu wakuu wa skuli zote kisiwani Pemba kusimamia uwajibikaji na nidhamu kwa walimu wao, ili wafanye kazi kwa ufanisi na kuleta maendeleo kwa wanafunzi.   Alisema kuwa, kuna baadhi ya walimu hawafundishi vizuri, wanaingia na kutoka kazini muda wanaotaka, jambo ambalo linasababisha kudumaza maendeleo ya wanafunzi na hatimae kuwa na ufaulu wa kiwango cha chini.   Akizungumzia mara baada ya kusikiliza changamoto za walimu Mkoa wa Kaskazini Pemba, Makamu huyo alisema, wasiende kuchafua mafaili yao kwa chuki binafsi, bali wawape miongozo inayotakiwa kwa mujibu wa Sheria, ili kufikia yale yanayoitaka Serikali.   "Nawasisitiza kutimiza wajibu wenu kisheria na sio kwa chuki, kwa sababu kuna walimu hawasomeshi vizuri, wanaingia na kutoka kazini muda wanaotaka lakini kwenye taarifa zao zote zinazotetwa ni nzuri kwenye mafaili yao&quo