Skip to main content

Posts

Showing posts from August 6, 2023

PACSO YAWAONESHA NJIA YA MALEZI WAZAZI, WALEZI PEMBA

  NA MWANDISHI WETU, PEMBA JAMII kisiwani Pemba, imetakiwa kufahamu changamoto na viashiria vya udhalilishaji kwa watoto, ili kuwalinda na vitendo hivyo.   Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Mtandao wa Asasi za Kiraia Pemba ‘PACSO’ Mohamed Ali Khamis, mara baada ya kuutambulisha mradi wa kujadili changamoto zinazowakabili watoto, katika ukumbi wa kiwanda cha Makonyo Wawi Chake chake Pemba.   Alisema, jamii inapaswa kuwa karibu mno na watoto wao, ili kujua haraka viashiria vya kudhalilishwa, na sio kusubiri hadi janga liwakumbe.   Mwenyekiti huyo alieleza kuwa, hilo litakuwa rahisi ikiwa wazazi na walezi watatenga muda wa kuwa karibu na watoto wao.   ‘’Kama tunajiona tuko na harakati nyingi za maisha na kusahau kukaa na watoto wetu, wanaweza kukumbwa na janga kama la udhalilishaji na tukachelewa kufahamu,’’alieleza.   Akielezea lengo la mradi huo Mwenyekiti huyo wa PACSO, alisema ni kuwazindua wazazi, kufahamu viashiria na changamoto na namna ya kuwasaidia watoto was

WAKULIMA, WAFUGAJI KOJANI VIDOLE MACHONI

  NA MOZA SHAABAN, ZU WAKULIMA katika Shehia ya Kojani Wilaya ndogo ya Kojani mkoa wa Kaskazini Pemba, wamewalalamikia wafugaji kutodhibiti mifugo yao, jambo ambalo hupelekea uharibifu wa mazao yao.   Akizungumza na Zanzibar leo, mkulima wa Viazi vitamu Saada Ali Faki kijijini hapo, alisema wamekua wakijishughulisha na kilimo ili kujikwamua kiuchumi, ingawa wafugaji hurejesha nyuma jitihada zao.   Alisema wamekuwa wakitumia nguvu na gharama kubwa, kupanda mazao ili yawasaidie kiuchumi, ingawa malengo yao hayafikiwi kwani wafugaji hushindwa kudhibiti mifugo yao na kufanya uharibifu mkubwa. "Sisi tunatumia nguvu kupanda mazao, ili yatusaidie na familia zetu, ingawa wafugaji wanaturejesha nyuma kwa kuachia huru mifugo yao na kutuharibia mazao yetu,”alisema. Nae mkulima wa zao la Mtama Bikombo Said Hamad alisema, wamekua wakichukua hatua kadhaa, ili kudhibiti suala hilo ikiwemo kuripoti matukio hayo kwa uongozi wa shehia na hatua stahiki kuchukuliwa, ingawa bado suala hilo

WEMA: ‘CHANGAMOTO ZA MAISHA MICHEWENI ZISIWE CHAKA LA UTORO WANAFUNZI'

  NA ABUU BAKAR, ZU@@@@ WANAFUNZI wa skuli za Micheweni kisiwani Pemba, wametakiwa kuacha utoro na kuhudhuria masomoni kikamilifu, na hali ngumu ya maisha inowakabili, isiwe chanzo cha katitisha masomo. Kauli imetolewa na Afisa Elimu Sekondar i wa Wilayani humo, Rishad Kombo Faki, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii, ofisini kwake Micheweni, juu ya utoro kwa baadhi ya wanafunzi, kwa kisingizio cha hali ngumu ya maisha. Ali sema hali ya kimazingira iliyopo Micheweni, isiwe chanzo kwa wanafunzi hao kukatisha masomo yao, kwani elimu ni haki yao ya msingi. Alieleza kuwa, wazazi wamekuwa wakipambana, ili kuhakikisha wanawapatia watoto wao huduma za kila siku na za lazima, hivyo ni wajibu kwa wanafunzi hao kuthamini jambo hilo. “Ni kweli mazingira yaliyopo Micheweni yana vivutizi vingi vinavyo sababisha wanafunzi kuwa watoro, na hii inatokana na wanafunzi kupata marafiki wasio kuwa wazuri kitabia,”alifafanua. Akizungumzia athari ya wanafunzi kuwa watoro masomoni, alis

MPAMBANI WETE WAWAPA TANO POLISI JAMII YAO

  NA TATU NAHODA, ZU@@@@ WANAKIJIJI wa kisiwa cha Kojani shehia ya Mpambani wilaya ya Wete Pemba, wameishukuru polisi jamii yao, kwa kudhibiti na kukabiliana na vitendo vya kihalifu kijijini hapo. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kijijini hapo, wananchi hao walisema, tokea kuanzishwa kwa ulinzi shirikishi shehiani hapo, vitendo kadhaa vya kihalifu vimepungua. Walisema kuwa, ulinzi shirikishi umekuwa muarubaini tosha katika kijiji chao, kwa kupunguza matendo maovu, jambo ambalo kabla ya hapo halikuwepo. Wananchi hao walieleza kuwa, umoja na mshikamano uliopo, umesaidia kudhibiti vitendo viovu, kama vile wizi wa mazao na mifugo, na kupelekea kuishi kwa amani na utulivu.   Mmoja kati ya wananchi hao Said Haji Said alisema, kwa sasa mifugo na vipando vyao vinanawiri, kutokana na kuimarika kwa ulinzi shirikishi, kijijini kwao. Alisema kwa sasa wafugaji, na wakulima wanavuna wanachokipanda kwa wakati, kutokana na kuimarika kwa ulinzi shirikishi, jambo ambalo halikuwepo

WAKULIMA WA KARAFUU KUENDELEA KUPOKEA MALIPO KUPITIA SIMU

  NA ABDI SULEIMAN, PEMBA@@@@ MKURUGENZI wa Mfuko wa Maendeleo ya Karafuu Zanzibar Ali Suleiman Mussa amesema, kutokana na kuongezeka kwa utapeli katika jamii ni vyema wakulima wa karafuu kuendelea kutumiwa fedha zao kwenye akaunti ya TigoPesa, ili zibaki kuwa salama. Alisema, njia hiyo itaweza kuwasaidia wakulima wa zao la karafuu, fedha zao kuendelea kuwa katika hali ya usalama muda wote na sio kuchukua mkononi, kwani inahatarisha maisha yao. Mkurugenzi huyo aliyaeleza hayo wakati akifungua mkutano wa wakulima wa karafuu Mkoa wa Kaskazini Pemba, juu ya kuhamasisha kutumia mtandao wa simu ya Tigo Pesa katika kutumiwa malipo yao baada ya kuiuzia Serikali  karafuu zao. Aliwataka wakulima hao katika msimu wa karafuu ulioanza Agosti 3 mwaka huu, kuhakikisha wanatumia mitandao ya simu kuweka fedha zao, huku Shirika la ZSTC likiendelea na mchakato wa kuwasajili wakulima wote. “Kutumia mitandao katika kuhifadhi fedha ni sehemu salama, kuliko kuondoka na fedha mkononi, wengi wanakumbana na ch

WANANCHI MLETENI: 'MARUFUKU MGENI KUINGIA PASI NA TAARIFA'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa kijiji cha Mleteni, shehia ya Kisiwani wilaya ya Wete Pemba, katika kukabiliana na dawa za kulevy na wizi, wameendelea kupiga marufuku kwa mgeni yeyote, kuingia kijijini hapo, pasi na taarifa kwa uongozi wa kijiji. Walisema, hawatomvumilia mgeni wala mwenyeji aliyefuatana naye, ikiwa watabainika ameingia kinyemela kijijini hapo na hakuna taarifa rasmi. Walieleza kuwa, kwa sasa kijiji chao cha Mleteni, kiko salama kiasi, kwa dawa za kulevya na hata wizi, ndio maana wanawasisitiza wenyeji wanaotembelewa na jamaa zao, kutoa taarifa rasmi, kwa uongozi wa kijiji. Mmoja kati ya wananchi hao Salim Mussa Ali, alisema ingawa utumiaji wa dawa za kulevya bado uko chini, lakini wanaendelea kuwataka wenyeji, wanaoingia na wageni wao, kutoa taarifa rasmi. ‘’Tumeshagundua kuwa, wapo wageni wengine wanakuja na nia mbaya katika kijiji chetu, sasa tukigundua na ikawa ana mwenyeji wake wa kijiji cha Mleteni, tutamfikisha mbele ya vyombo vya sheria,’’ali

MKAGUZI WA POLISI JAMII AMWAGA VIFAA KWA WANAFUNZI WANAOJITAYARISHA NA MITIHANI

  NA SAID ABDULRAHMAN, PEMBA@@@@   WANAFUNZI wa skuli ya msingi na sekondari Pandani pamoja na sekondari Wete ambao wanajitayarisha na mitihani yao ya taifa, wamepatiwa msaada wa tochi na bablbu vyenye thamani ya shilingi 23,5000 kwa ajili ya kuwasaidia wakati umeme unapozimwa.     Msaada huo umetolewa na Mkaguzi wa Polisi Jamii shehia ya Pandani, Inspector Khalfan Ali Ussi baada kutembelea kambi ya wanafunzi hao na kuona hali halisi ilivyo wakati unapozima umeme, jambo ambalo linawapa usumbufu wakati wanapopitia masomo yao.   Akizungumza baada ya kukabidhi vifaa hivyo alieleza kuwa, vitaweza kuwasaidia wanafunzi hao katika kujisomea wakati umeme unapokata kwenye mabweni yao.   Inspector Khalfan aliwataka wanafunzi hao kujitahidi katika masomo yao, ili waweze   kufaulu vizuri na kuwa wakombozi katika familia zao na taifa kwa ujumla.   Aidha alieleza kuwa, wako tayari kufuatilia nyenendo za wanafunzi hao na yeyote ambae atapatikana na hatia ya kutohudhuria kwenye masom