Skip to main content

Posts

Showing posts from August 7, 2022

WAFANYAKAZI ZECO KUTIMULIWA KAZI IKIWA.............

  NA SALMA LUSANGI, ZANZIBAR WAFANYAKAZI wa Shirika la Umeme Zanzibar 'ZECO' wameahidiwa kuwa watafukuzwa kazi, endapo uchuguzi unaoendelea ukibaini wameshiriki katika kuwaunganishia umeme watu waliyokamatwa kwa kosa la kujiunganishia, umeme kinyume na sheria Zanzibar. Kauli hiyo imeitowa na Katibu Mkuu wizara ya Maji, Nishati na Madini Joseph Kilangi wakati akizungumza na watendaji wa ZECO, katika ofisi ya shirika hilo jana. mjini Zanzibar. Alisema mwananchi wa kawaida aliyekuwa hajasoma fani ya umeme, hawezi kuchezea umeme lazima alishirikiana na mtaalamu wa umeme kutoka ZECO au nje ya ZECO hivyo ripoti ya uchunguzi ikionesha mtendaji wa Shirika amehusika atamfukuza kazi. “Mimi ninavyofahamu nguzo ya umeme haikai ndani ya fensi, kuna mtu hapo amecheza aidha kuungana na mfanyakazi wa ZECO na mfanyakazi yeyote aliyeshiriki kuungana na kishoka hatakuwa salama nitamchomoa,''alieleza. Aliwanasihi wafanyakazi hao, wakati huu ni vizuri ajitokeze mwenyewe ili ajulikane  aliye

WATAALAMU WA AFYA PEMBA WAPIGIA CHAPUO MAZIWA YA MAMA KWA WATOTO

NA HAJI NASSOR, PEMBA::::: WATAALAMU wa afya ya mama na mtoto kisiwani Pemba, wamewakumbusha wanawake, kuhakikisha hawawalishi chakula au aina yoyote ya kimiminika, watoto wao wachanga, kama bado hawajatimiza miezi miezi sita, kwani kufanya hivyo, huwapa ukuaji bora na wenye afya. Walisema ukuaji bora na wenye afya kwa mtoto, na hasa baada ya kuzaliwa, huchangiwa na mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na wazazi kuacha kuwalisha watoto wao chakula au aina ya yoyote ya maji. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, wataalamu hao walisema, kumlisha chakula hata laini au aina yoyote ya maji mtoto ambae hajatimiza miezi sita, ni kuilazimisha mishipa na mashine ya kusagia kufanya kazi isiyoimudu. Mmoja kati ya wataalamu ambae ni muuguzi wa mama na mtoto wa Hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani, Rabia Mohamed Ussi, alisema hali hiyo, hupelekea kuzuka kwa magonjwa ikiwa ni pamoja na utampia mlo. ‘’Hata kama mtoto analia kwa ishara ya njaa, lakini hakuna namna ya kumpa chakula au

ASILIMIA 97 YA WATOTO WANAOZALIWA HUNYONYESHWA MAZIWA YA MAMA

  Joyce Joliga, Songea   Asilimia 97 ya watoto wanaozaliwa hunyonyeshwa maziwa ya mama, ikiwa asilimia 92 ya watoto hunyonyeshwa kwa kipindi cha mwaka mmoja na kuendelea.   Hayo yamebainishwa leo na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu Mhe. Mwanaidi Khamis wakati akimwakilisha Waziri wa Afya Mhe Ummy Mwalimu kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji maziwa ya mama kwa watoto kitaifa yanayofanyika kwenye halmashauri ya Ikungi Mkoani Singida.   Mhe. Mwanaidi ameendelea kusema kuwa 43% tu ya watoto  ndio hunyonyeshwa hadi kipindi cha miaka miwili na kuendelea huku takwimu zikionesha 57% tu ya watoto ndiyo hunyonyeshwa maziwa ya mama pekee bila kuchanganya na chakula kingine wala maji ndani ya kipindi cha miezi 6.   "Tafiti zinaeleza kuwa mtoto akizaliwa na kuanza kunyonyeshwa maziwa ya mama ndani ya saa moja kunaweza kuokoa uhai wake kwani kuchelewa kumnyonyesha mtoto kuna changia kwa kiwango kikubwa vifo vya watoto

MCT: VYOMBO VYA HABARI KUFUATA MAADILI HAKUNA MBADALA

  NA HAJI NASSOR, ALIPOKUWA UNGUJA MWENYEKITI Kamati ya Maadili ya Baraza la Habari Tanzania MCT- Jaji mstaafu Robart Makaramba, amesema nguvu iliyonayo chombo cha habari ni kubwa, hivyo suala la kuzingatia na kufuata maadili kwa vitendo halina njia mbadala. Alisema, maadili ndio msingi mkuu kwa vyombo vya habari, kutekeleza wajibu wao vyema, na kinyume chake kikitumika vibaya nguvu zake, kinaweza kuleta madhara. Mwenyekiti huyo aliyaeleza hayo August 9, mwaka 2022 mjini Unguja, kwenye mkutano wa siku moja, wa waandishi wa habari, wahariri na wadau wa habari, katika mkutano maalum wa kujadili maadili ya wanahabari. Alisema, kila mwandishi akiamua kuyafuata kwa vitendo maadili ya kazi yake, jamii hawatakwazwa na vyombo vya habari, kama ilivyo sasa kwa baadhi ya vyombo kuyapa kisogo. ‘’Niwakumbushe sana suala la kufuata maadili yenu, maana nyinyi waandishi na wahariri mnanguvu kubwa mno, hata zadi ya bunduki na upanga,’’alieleza. Akizungumza kwenye mkutano huo, Katibu Mtendaj

NAIBU WAZIRI MADINI ATOA NENO RASILIMALI YA MCHANGA-ZANZIBAR

  NA SALMA LUSANGI, ZANZIBAR NAIBU Waziri wizara ya Maji, Nishati na Madini Zanzibar Shaaban Ali Othman, amesema Zanzibar hakuna biashara ya mchanga hivyo, eneo la Taveta na maeneo mengine ya hawarusiki mtu kufanya biashara hiyo.   Hayo aliyasema wakati akizungumza na waandishi wa habari wakati akikagua barabara ya ndani iliyojengwa na Wizara  yake, ili kurahisisha upatikanaji wa huduma ya hiyo huko Donge Pangatupu Mkoa wa Kaskazini Unguja. Alisema wizara ya kupitia Idara yake ya Nishati na Madini imeshatoa maelekezo, kwamba wananchi wanatakiwa waombe huduma hiyo moja kwa moja kupitia mfumo maalum. Alisema hakuna ugumu katika upatikanaji wa huduma ya mchanga kwa njia ya mfumo hadi  huduma hiyo kumfikia mtumiaji, hivyo maeneo Taveta na maeneo mengine sio rasmi kuuza mchanga na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, haiko tayari kuruhusu mtu yeyote  kufanya biashara hiyo. “Kumekua na ukaidi ambao sio walazima sana, hii inatusababisha sisi tuweze kutumia sheria zaidi, kwasababu mael

FOREST BURNING IS A BIG THREAT TO THE ENVIRONMENT IN ZANZIBAR

  BY, HAJI NASSOR-PEMBA   BURNING of forests is the biggest threat of environmental damage in the Jonzani national park located 35 kilometers south of the island of Unguja.   This park with an area of ​​5,000 hectares is the home of the rare natural resource Kima Punju (Zanzibar Red Colobus Monkey), animals that are not found anywhere else in the world.   In addition, it is one of the few natural forests with world status recognized by the United Nations Educational and Scientific Organization (UNESCO).   This damage is due to the increase of human activities in the reserve area, especially agriculture, beekeeping and grazing for animals.   Forest burning in this period is greater than it was six decades ago.   According to the Zanzibar Department of Forestry and Non-Renewable Natural Resources, the burning of forests in this reserve was three hectares on November 13, 2012 but the rate increased by 50 times on February 8, 2015, where 141 hectares of forests we

CHAPO YAWAFIKIA WANANCHI MFIKIWA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA /CHAPO IDARA ya utambuzi wa ardhi Pemba,  imesema ardhi  yenye eneo dogo iliyopangwa, kupimwa na kisha mmiliki kukabidhiwa hati ya matumizi, huwa na thamani mara mbili ya eneo kubwa ambalo halikupimwa. Hayo yameelezwa na Afisa wa Utambuzi wa ardhi Pemba Faki Ali, wakati akijibu maswali ya wananchi wa shehia ya Mfikiwa wilaya ya Chakechake, kwenye mkutano wa wazi ulioandaliwa na na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chakechake, CHAPO juu ya elimu ya utatuzi wa migogoro ya ardhi kwa njia ya amani. Alisema, kuna umuhimu mkubwa kwa wananchi, ardhi zao kuzirasmisha kwa kuzitambua na kupata hati maalum za matumizi, ili ziongezeke thamani wakati zinapohitajika kwa matumizi mengine. Alieleza kuwa, serikali ina nia ya kuipima ardhi yote ya Zanzibar, na kuwapa wananchi hati ya matumizi, bila ya malipo yoyote. Afisa huyo alifafanua kuwa, tayari shehia tano za Unguja na Pemba zimeshaanza mpango huo kwa majaribio. "Lazima wananchi waelewa kuwa, ardhi iliyopimwa