Skip to main content

Posts

Showing posts from June 11, 2023

MTAMBWE KUSINI MAJI 'BWERERE', ZAWA YASEMA JAMBO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa shehia ya Mtambwe kusini wilaya ya Wete Pemba, wamesema kwa sasa huduma ya maji safi na salama katika vijij vyao, inapatikana kwa urahisi, tofauti na hapo zamani. Walisema, kwa sasa wamekuwa na wakati mzuri wa kujipangia shughuli zao mbali mbali za kimaisha, na wala upatikanaji wa huduma hiyo, sio changamoto inayowatengulia rataiba zao za kimaisha. Wakizungumza na waandishi wa habari waliofika kijijini hapo, walisema kwa sasa huduma hiyo, iko karibu vijiji vyote, tena bila ya mgao, jambo ambalo limechangia kufikia malengo yao. Walieleza kuwa, upatikanaji wa huduma hiyo kwa miaka minne mfululizo sasa, unawapa uhakika wa maisha yao, hasa kwa vile kila mmoja, anaendesha shughuli zake kwa urahisi. Salma Hamad mkaazi wa kijiji cha Kivumoni, alisema kwa sasa huduma hiyo iko vyema na haina shida kwao, ikilinganisha na miaka 20 iliyopita. ‘’Awali sisi wananchi wa kikijiji cha Kivumoni shehia ya Mtambwe kusini, tukifuata maji masafa ya mbali

MKAMA NDUME: MTAWALA MBABE PEMBA KIFO CHAKE KIZUNGUMKUTI HADI LEO

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ HAPO zamani Magofu ya Mkama Ndume yalikuwa makaazi ya waswahili, ya enzi za kati, ambayo yaliachwa na wakaazi wake katika karne ya 16.   Ambapo hapo, ilikuwa ni kabla ya Wareno Afrika Mashariki inajulikana kwa uimarishaji wake kwa kutumia mawe. Magofufu hayo yako wastani wa kilomita 10 kutoka katikati ya mji wa Chake chake, ambao ndio makao makuu kwa kisiwa cha Pemba.   Kwa wakati huo mji huo ulitawaliwa na kiongozi mmoja aitwaye Mohammed bin Abdul -Rahman, ambaye alijulikana sana kwa ukatili wake kwa raia wake. Na kwa wakati huo alipewa jina la utani la Mkama Ndume lenye maana ya  mkamua wanaume  kwa lugha ya kiswahili cha zamani. Ndio maana, hadi leo eneo hilo lililojaa historia sio kwa kisiwa cha Pemba pekee, bali baraza zima la Afrika na duniani, pakaitwa Mkama Ndume. Kwa kuwa mtawala alikuwa akifanya ibada, alijenga msikiti wa asili wa Ijumaa, miaka 700 iliyopita, ambao ulikuwa na nguzo tisa. Nguzo tatu mbele, tatu nyuma na kat

SKULI YA SEKONDARI CONECTING CONTINENT, ZAO LA MWEKEZAJI LINALOWANYIWA NA WAZALENDO

        NA MARYAM SALUM, PEMBA@@@@ SKULI ya sekondari ya Connecting Continent iliyopo nje kidogo ya mji wa Chake chake, ni miongoni mwa skuli 10 binfsi zilizopo kisiwani Pemba. Skuli hiyo ipo nje kidogo ya mji wa Chake Chake, imekuwa ikiwavutia zaidi na wanafunzi wasichana kutokana na upasishaji wake mzuri wa kila mwaka. Conecting ni miongoni mwa skuli 10 binafsi kisiwani Pemba, zilizobahatika kuruhusiwa kuwekeza katika elimu kwa ngazi ya sekondari. Skuli hiyo ilianzishwa mwaka 2006 ikimilikiwa na wawekezaji wajerumani, ikiendeshwa na michango midogo midogo ya wafadhili wenyewe na ada nyepesi zinatolewa na wazazi na walezi.     Skuli hiyo ilianza kufanya mitihani ya taifa mwaka 2008, na kufika mwaka 2022, wanafunzi 671 walihitimu.   Kati ya wanafunzi hao wanawake walikuwa 332 na wanaume walikuwa 339 kwa wakati huo, wakitokea skuli mbali mbali za msingi kisiwani Pemba. Mwandishi wa makala hii hakutaka hadithi za mdomo alitaka kujua kinaga ubaga historia japo fupi y