Na Muandishi Wetu Zanzibar Mwenyekiti wa Kamati yaMapngo wa Kitaifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto, ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman, amewataka wadau wanaojihusisha na masuala ya ukatili na udhalilishaji kufanya kazi kwa weledi na ushirikiano ili kutokomeza vitendo hivyo katika jamii. Mhe. Haroun alitoa wito huo jana wakati wa uzinduzi wa Kamati ya Kitaifa ya ngazi ya Mawaziri uliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Airport, Zanzibar. Alisema kuwa lengo la kuundwa kwa kamati hiyo ni kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi mbalimbali katika kupambana na vitendo vya ukatili na udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto, kwa lengo la kupunguza na hatimaye kuvimaliza kabisa. Aidha, aliitaka kamati hiyo kutekeleza majukumu yake kwa bidii, kuweka mikakati madhubuti na kuhakikisha sheria pamoja na sera zilizopo zinatekelezwa ipasavyo ili kulinda haki za wanawake na ...