Skip to main content

Posts

Showing posts from June 28, 2026

Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa Ataka Wadau Kuongeza Weledi Katika Kutokomeza Ukatili

  Na Muandishi Wetu Zanzibar Mwenyekiti wa Kamati yaMapngo wa   Kitaifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto, ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman, amewataka wadau wanaojihusisha na masuala ya ukatili na udhalilishaji kufanya kazi kwa weledi na ushirikiano ili kutokomeza vitendo hivyo katika jamii. Mhe. Haroun alitoa wito huo jana wakati wa uzinduzi wa Kamati ya Kitaifa ya ngazi ya Mawaziri uliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Airport, Zanzibar. Alisema kuwa lengo la kuundwa kwa kamati hiyo ni kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi mbalimbali katika kupambana na vitendo vya ukatili na udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto, kwa lengo la kupunguza na hatimaye kuvimaliza kabisa. Aidha, aliitaka kamati hiyo kutekeleza majukumu yake kwa bidii, kuweka mikakati madhubuti na kuhakikisha sheria pamoja na sera zilizopo zinatekelezwa ipasavyo ili kulinda haki za wanawake na ...

KIZUNGUMKUTI TUHMA ZA UKATILI, UDHALILISHAJI KWA KIZIWI MICHEWENI

  SAIDA ALI, PEMBA MAMA mzazi ambae mwanawe mwenye ulemavu wa uziwi wa miaka 38, alifanyiwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji, ameviomba vyombo vya ulinzi na usalama, kuwa haki itendeke kufuatia unyama aliodai kufanyiwa, kijana wake. Aliyasema hayo, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, shehia ya Shumba vyamboni wilaya ya Micheweni, kufuatia sitofahamu ya majibu ya hospitali na athari aliyonayo kijana wao. Alisema kuwa kitendo alichodai kufanyiwa kijana wao huyo, ambacho alimshuhudia akiwa amefungwa mikono nyuma akiwa na tambara mdomoni, ni cha kikatili na udhalilishaji. Alieleza kuwa, muda wa saa 8:00 usiku baada ya kusikia kelele za kukorota kwa kijana wake, alikimbilia chumbani kwake, na kufika alijonea maajabu. ‘’Kwanza alikuwa amevungwa mwiili mzima nguo nyeusi mithili ya beibui, nilishuhudia vichupa vidogo viwili, kimoja kikiwa na majimaji, (dawa) nusu na chingine kikiwa kitupu,’’alifafanua. Aidha mzazi huyo alisema, jingine ambalo limemshitua kwa kij...