NAIBU Waziri wa Maendeleo wa Jamii Jinsia Wazee na Watoto Anna Athanas Paul amesema iwapo mtoto wa kike atasoma kwa bidii ataweza kuviepuka viashiria vya unyanyasaji ambavyo ndio vikwazo vikubwa vinavyowafanya kutokufikia malengo yao. Ameeleza jayo katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya mtoto wa kike huko katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) Kampas ya Maruhubi Unguja. Amesema watoto wa kike wakisoma kwa bidii itasaidia kutimiza malengo yao ya baadae hali ambayo itasaidia kujiepisha na vitendo viovu ikiwemo unyanyasaji wa kijinsia. “Iwapo mtoto wa kike atasoma kwa bidii ataweza kuviepuka viashiria vya unyanyasaji ambavyo ndio vikwazo vikubwa vinavyowafanya kutokufikia malengo yao ” Amesema Waziri huyo. Naibu Waziri huyo amefahamisha kuwa kwa mujibu takwimu kutoka Afisi ya Mtakwimu Mkuu mwaka 2023 matukio 1954 ya ukatili na udhalilishaji yaliripotiwa kati ya matukio hayo wasichana walikuwa 1263 sawa na aslimia 77.1 hiyo inaonesha bado watoto wa kike wanah