Skip to main content

Posts

Showing posts from October 13, 2024

ANNA ATAJA FAIDA LUKUKI ZA ELIMU KWA MTOTO WA KIKE

  NAIBU Waziri wa Maendeleo wa Jamii Jinsia Wazee na Watoto Anna Athanas Paul amesema iwapo mtoto wa kike atasoma kwa bidii ataweza kuviepuka viashiria vya unyanyasaji ambavyo ndio vikwazo vikubwa vinavyowafanya kutokufikia malengo yao. Ameeleza jayo katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya mtoto wa kike huko katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) Kampas ya Maruhubi Unguja. Amesema   watoto wa kike wakisoma kwa bidii itasaidia kutimiza malengo yao ya baadae hali ambayo itasaidia kujiepisha na vitendo viovu ikiwemo unyanyasaji wa kijinsia. “Iwapo mtoto wa kike atasoma kwa bidii ataweza kuviepuka viashiria vya unyanyasaji ambavyo ndio vikwazo vikubwa vinavyowafanya kutokufikia malengo yao ” Amesema Waziri huyo. Naibu Waziri huyo amefahamisha kuwa kwa mujibu takwimu kutoka Afisi ya Mtakwimu Mkuu mwaka 2023 matukio 1954 ya ukatili na udhalilishaji yaliripotiwa kati ya matukio hayo wasichana walikuwa 1263 sawa na aslimia 77.1 hiyo inaonesha bado watoto wa kike wanah

VOSHOKA WA UBAKAJI PEMBA KIKAANGONI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAMTANDAO wa kupambana na vitendo vya udhalilishaji kisiwani Pemba, wamelaani kitendo cha watu wazima, kukimbilia kwa watoto wachanga, kuwadhalilishaji, kwani husababisha athari zaidi kwao. Walisema, miongoni mwa athari hizo ni kuwasababisha kukosa kizazi, kuwatishia masomo, athari za kisaikolojia jambo ambalo linatajwa kuzima ndoto zao za maisha. Wakizungumza kwenye kikao cha kuwasilisha ripoti za kazi zao, kilichofanyika ofisi ya TAMWA Pemba, walisema, sasa vitendo hivyo wadhalilishaji wameelekeza nguvu zaidi kwa watoto wadogo. Walieleza kuwa, zipo kesi kadhaa zinazowahusu watoto wenye umri kati ya miaka mitano hadi 10, wakifanyiwa udhalilishaji na wanaume wenye umri kuanzia miaka 40 hadi 50. Mwanamtandao kutoka wilaya ya Mkoani Haji Shoka Khamis, alisema sasa wabakaji wameelekeza nguvu kwa watoto wadogo, jambo linalokuwa gumu wanapofika mahakamani. ‘’Wadhalilishaji sasa wamehamia kwa watoto wadogo, na kisha huwapa lugha za vitisho, kwamba