Skip to main content

Posts

Showing posts from September 4, 2022

SHERIA ZIZINGATIE UWIYANO WA KIJINSIA ILI KUWAWEZESHA WANAWAKE KIUONGOZI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::: MAPUNGUFU yaliyopo katika sheria mbali mbali Zanzibar, zimetajwa kuwa zinachangia kutokuwepo kwa uwiano wa usawa wa kijinsia, kati ya wanawake na wanaume katika ngazi mbali mbali za uongozi.   Mapungufu ya sheria hizo yameibuliwa na wanajamii kufuatia mikutano 41 iliyofanyika katika shehia 44 kisiwani Pemba, iliyoandaliwa na wahamasishaji jamii kwa  kushirikiana na asasi za kiraia kisiwani hapa, juu ya ushiriki wa wanawake katika kushika  nafasi za uongozi na demokrasi. Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari juu ya mapungufu yaliyobainika kwenye sheria kukwaza ushiriki wa wanawake kwenye nafasi za uongozi, Mkurugenzi wa Jumuiya ya utetezi wa Jinsia na Mazingira Pemba (PEGAO) Hafidh Abdi August 8, mwaka 2022, alisema miongoni mwa Asasi zilizoshirikiana kuchambua mapungufu hayo ni pamoja na taasisi ya Tumaini Jipya Pemba (TUJIPE), Nihurumie Foundation, KOK Foundation, PRADO, PACSO, Jumuiya ya Wanawake wa Kiislamu, pamoja na Kituo cha hudum

IMPROVED COOKING TECHNOLOGIES TO REDUCE THE USE OF FIREWOOD IN RURAL HOUSEHOLDS

  Zawadi Ali Mjaka (30) has been suffering from eye disease for five years now.  According to doctors the source of her disease is smoke due to frequent uses of firewood for cooking. Despite all her efforts to seek treatment in various hospitals, Mwanaisha, a mother of two children and a resident of Unguja Ukuu Unguja South District, is yet to be cured. She complains of swelling eyes with tears whenever she uses firewood for cooking.  Because of her poverty and inability to afford the costs of gas or electricity for cooking she is compelled to use firewood as source of energy. "I have been suffering from eye infections for more than five years now, I have visited various hospitals to seek treatment but I have not yet recovered,” she said.   Zawadi is not the only rural woman who continues to suffer from the disease due to the use of firewood for cooking. Unlike Zwadi who has been suffering from eye problems, other women who use clean energy for cooking have never

WEMA PEMBA YAWAJENGEA UWEZO WASHAURI WA MASOMO

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA:::: WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar imewajengea uwezo washauri wa masomo, ili kuboresha zaidi katika kufanya ufuatiliaji, ushauri katika ufundishaji pamoja na upimaji kwa wanafunzi. Akifungua mkutano kwa washauri hao, leo August 8, 2022 Kaimu Mratibu Idara ya Mafunzo ya Ualimu WEMA Pemba, Mzee Ali Abdalla alisema mafunzo hayo yatasaidia kuboresha kiwango cha ufaulu kwa wananfunzi. Alisema kuwa, katika ufuatiliaji imeonekana kuwa kuna changamoto kwenyea kutunga maswali yenye umahiri katika pimaji na mitihani, hivyo Wizara imeona kwamba ipo haja ya kuliomba Baraza la Mitihani Tanzania kuwapa mafunzo washauri wa masomo, ili na wao waweze kuwajengea uwezo walimu. ‘’Kutokana na changamoto hiyo, tumeona kwamba tutumie fursa hii, kwani Baraza la mitihali limekuwa likitoa mafunzo haya kwa maafisa mitihani katika halmashauri na skuli mbali mbali’’, alisema Kaimu huyo. Alieleza kuwa, lengo la mafunzo hayo ni kwamba baada ya mafunzo wawe na uwezo wa

MEIYE HAMAD: MJASIRIAMALI WA PEMBA ALIYEANZA KAMA MCHICHA SASA NI MBUYU

  NA MARYAM SALUM, PEMBA   WATU wa zamani walishasema kuwa, maisha ni kutafuta na sio kutafutana. Wengine wakaibuka wakisema kuwa, mtafutaji hachoki na mgagaa na upwa hali ugali mkavu. Hapa walilenga mbali kuwa, mtafutaji hachoki na mafanikio yanahitaji juhudi binafsi na wala hayashuki tu kama mvua mawinguni. Misemo hii sasa yamesadifu kwa vitendo kwa mjasiriamali Meiye Hamad Juma (47), akiishi kijiji cha Mavungwa shehia ya Mbuzini nje kidogo na mji wa Chake Chake Pemba. ALIPOANZIA UJASIRIAMALI Mwaka 2016, ndio bisummillah, mjasiriamali huyo alipofunuka macho yake mawili, na kuanza kama mchicha kwenye ujasiriamali wake. Kwa wakati huo akiwa ni mmoja wa wanachama wa ushirika wa “Tupate Sote” na kujiunza shughuli mbali mbali za utengenezaji bidhaa. Lakini 2018, Meiye alipoamua kuanzisha kikundi chake, kwa kutengeneza bidhaa mbali mbali ambazo kwa sasa zimemkomboa kimaisha. ‘’Bidhaa ambazo kwa sasa natengeneza baadhi ni zile nilizoziona kule kwenye ushirika wangu wa awal

KATIBU TAWALA MKOANI AWAPA NENO WAKULIMA WA KARAFUU

                NA HAJI NASSOR, PEMBA::::: KATIBU Tawala Wilaya ya Mkoani Pemba Miza Hassan Faki amewakumbusha wakulima wa zao la karafuu Wilayani humo kutokuzichanganya karafuu zao na takataka nyengine ikiwemo makonyo kwani kufanya hivyo kunaweza kulipoteza ubora zao hilo. Alisema karafuu za Zanzibar zina ubora wa aina yake kuliko maeneo yote Duniani hivyo, ni wajibu kwa wakulima hao kulifahamu hilo na kuenzi ili liweze kubakia katika ubora wake. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake Mkoani alisema, ubora wa zao hilo ni vyema ukaanzia kwa wakulima iwe katika kulianika kwenye vyombo vinavostahiki. Alieleza kuwa, uwanikaji wa karafuu katika saruji, lami, bati na katika vyombo sehemu inayoanza kupoteza ubora na kuanza kuingia takataka nyengine. Katibu Tawala huyo alieleza kuwa, ubora wa zao hilo baada ya kuvunwa kwake hutakiwa kuanikwa katika vyombo maalumu kama vile majamvi na mikeka ili kudhibiti mafuta ya karafuu hizo yasipotee kabla ya kufikishwa kituoni kwa