Skip to main content

Posts

Showing posts from November 23, 2025

SHEHA CHUMBAGENI LEO KUWAONGOZA WANANCHI KIDUTANI UPITISHWAJI KANUNI ZA KIJIJI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SHEHA wa Chumbageni wilaya ya Mkoani, Mgeni Othman Shaame, jioni ya leo anatarajiwa kuwaongoza wanachi wa kijiji cha Kidutani, kuzipitisha sheria ndogondogo, zitakazowaongoza wananchi hao, ili kujenga tabia njema . Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Katibu wa kamati ya elimu na maadali ya kijiji hicho Machano Ali Makame, alisema jioni ya leo, kijijini hapo watakuwa na ugeni wa shehia yao. Alisema kuwa, sheha huyo pamoja na ujumbe wake akiwemo askari wa shehia, watakutana na wananchi hao, na kuzijadili kwa mara ya mwisho kanuni, hizo kabla ya kuzipitisha rasmi. Alieleza kuwa, kijiji hicho kimeamua kuanzisha kanuni hizo, ili kuwasawaidia vijana kuwaelekeza kwenye maadili mema, ili wawe raia bora wa taifa hili. ‘’Ni kweli jioni ya leo, Sheha wa Chumbageni ataungana na wananchi wa kijiji cha Kiduatani, ili kuzipitisha kanuni, ambazo zilianzishwa na wananchi wenyewe,’’alisema. Mwenyekiti wa kamati hiyo Mwalimu Saleh Abdalla Mohamed, alisem...

WAANDIKISHENI WATOTO WENYE ULEMAVU SKULI "MDHAMINI ELIMU"

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA WAZAZI na walezi wenye watoto wenye ulemavu wametakiwa kuwaandikisha watoto hao skuli kwa mwaka wa masomo unaotarajiwa kuanza 2026, ili kuhakikisha upatikanaji wa haki ya msingi ya elimu kwa watoto hao. Wito huo umetolewa na Afisa mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali   Pemba Mohamed Nassor Salim wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi, alisema zoezi la uandikishaji wanafunzi wapya kwa mwaka wa masomo 2026 linaendelea kwa watoto wote waliofikia umri wakiwemo wenye ulemavu. Alisema wakati umefika kwa wazazi, walezi jamii na serikali za shehia kuhakikisha watoto wenye ulemavu wanapata haki yao ya msingi ya elimu, kwa kuhakikisha wanandikishwa skuli bila kujali mahala wanapoishi au aina ya ulemavu walionao. Aliongeza serikali kupitia wizara ya elimu imeandaa mazingira rafiki kwa watoto wenye ulemavu ambao wanaishi katika mazingira magumu, kwa kuwajengea skuli maalumu inayotoa elimu mjumuisho ili kuhakikisha wanapata haki yao ya msing...