Skip to main content

Posts

Showing posts from November 23, 2025

WADAU ZANZIBAR WAUNGANA KUADHIMISHA SIKU 16 ZA KUPINGA UDHALILISHAJI

                                                                                                                                                                                                                                27/11/2025 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI     Taasisi za kutetea haki za wanawake, vijana, watu wenye ulemavu na watoto Zanzibar,  zinaungana kwa pamoja kuadhimisha Siku 16 za Kupinga udhalilis...

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

  NA FATMA HAMAD, PEMBA@@@@ UTELEKEZAJI ni ile hali ya wazazi kukwepa majukumu yao ya kutoa matunzo kwa familia zao. Wengi wa wananchi wanadai kwamba, sababu kubwa inayopelekea utelekezaji ni baadhi ya akinababa wanapoamua kuoa mke zaidi ya mmoja, maranyi huwa hawatimizi wajibu wao. Ingawa wapo wengine, hudai kukumbwa na sababu, ya kutafuta maisha kutoka sehemu moja kwenda nyingine, mfano wa wavuvi au wafanyabiashara. Hayo yakifanyika, mafundisho ya dini yanafundisha kuwa, mzazi wa kiume ndio mwenye jukumu kubwa la kutoa matunzo kwa familia yake. Lakini ulimwengu wetu wa leo, kumeibuka wimbi kubwa la baadhi ya wanaume kukwepa majukumu   yao na kuwabebesha mzigo wa malezi wanawake peke yao. Hali hiyo ya wanaume kutokushughulikia familia zao, inasababisha watoto kuishi kwa simanzi na huzuni, kana kwamba wamefiwa na wazazi wao na kukosa familia ya kuwatunza. Kiongozi wa Kanisa Katoliki lililopo Mkungu Malofa Chakechake, Robert Miguwa Ndalami, anasema dini imeeleke...

SHEHA CHUMBAGENI LEO KUWAONGOZA WANANCHI KIDUTANI UPITISHWAJI KANUNI ZA KIJIJI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SHEHA wa Chumbageni wilaya ya Mkoani, Mgeni Othman Shaame, jioni ya leo anatarajiwa kuwaongoza wanachi wa kijiji cha Kidutani, kuzipitisha sheria ndogondogo, zitakazowaongoza wananchi hao, ili kujenga tabia njema . Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Katibu wa kamati ya elimu na maadali ya kijiji hicho Machano Ali Makame, alisema jioni ya leo, kijijini hapo watakuwa na ugeni wa shehia yao. Alisema kuwa, sheha huyo pamoja na ujumbe wake akiwemo askari wa shehia, watakutana na wananchi hao, na kuzijadili kwa mara ya mwisho kanuni, hizo kabla ya kuzipitisha rasmi. Alieleza kuwa, kijiji hicho kimeamua kuanzisha kanuni hizo, ili kuwasawaidia vijana kuwaelekeza kwenye maadili mema, ili wawe raia bora wa taifa hili. ‘’Ni kweli jioni ya leo, Sheha wa Chumbageni ataungana na wananchi wa kijiji cha Kiduatani, ili kuzipitisha kanuni, ambazo zilianzishwa na wananchi wenyewe,’’alisema. Mwenyekiti wa kamati hiyo Mwalimu Saleh Abdalla Mohamed, alisem...

WAANDIKISHENI WATOTO WENYE ULEMAVU SKULI "MDHAMINI ELIMU"

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA WAZAZI na walezi wenye watoto wenye ulemavu wametakiwa kuwaandikisha watoto hao skuli kwa mwaka wa masomo unaotarajiwa kuanza 2026, ili kuhakikisha upatikanaji wa haki ya msingi ya elimu kwa watoto hao. Wito huo umetolewa na Afisa mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali   Pemba Mohamed Nassor Salim wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi, alisema zoezi la uandikishaji wanafunzi wapya kwa mwaka wa masomo 2026 linaendelea kwa watoto wote waliofikia umri wakiwemo wenye ulemavu. Alisema wakati umefika kwa wazazi, walezi jamii na serikali za shehia kuhakikisha watoto wenye ulemavu wanapata haki yao ya msingi ya elimu, kwa kuhakikisha wanandikishwa skuli bila kujali mahala wanapoishi au aina ya ulemavu walionao. Aliongeza serikali kupitia wizara ya elimu imeandaa mazingira rafiki kwa watoto wenye ulemavu ambao wanaishi katika mazingira magumu, kwa kuwajengea skuli maalumu inayotoa elimu mjumuisho ili kuhakikisha wanapata haki yao ya msing...