Skip to main content

Posts

Showing posts from July 3, 2022

WATAALAMU ‘ECD’ WATAJA MBINU UJENZI WA UBONGO WA MTOTO MCHANGA

  NA HAJI NASSOR, DODOMA WAZAZI na walezi, wametakiwa kuzungumza na watoto wao wachanga kwa lugha rasmi, zinazozungumzwa na jamii yao, kwani kufaya hivyo, ni sehemu ya kuongeza makuzi, ufahamu na utanuzi wa ubongo wao. Kwani, tafiti zimegundua kuwa, watoto hata wanapokuwa tumboni, wanauwezo mkubwa wa kusikia mazungumzo ya lugha yoyote, hivyo mara wanapozaliwa wazazi wawe nao karibu. Muwezeshaji kwenye mafunzo ya Kitaifa ya Sayansi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto ‘SECD’ kutoka Mombasa Kenya Everlyne Okeyo, aliyaeleza hayo mjini Dodoma. Alisema, watoto wanakosa ukuaji mzuri wa kutengeneza ubongo wao, kwa kule wazazi kutowashughulika kuzungumza nao, wakidhani hawana uwezo wa kufahama lugha zao. Alieleza kuwa, makuzi mazuri ya awali ya mtoto, ni baina ya siku moja baada ya kuzaliwa hadi miaka minane, ambapo hapo huwa rahisi kwa wazazi na walezi, kuweke mwelekeo wa maisha ya mtoto. ‘’Wazazi waliowengi wamekua wanaanza kuweka nguvu zaidi za watoto wao, mara wan

MAUZO YA MADINI YAPAA ZANZIBAR

      NA  HAJI MTUMWA, ZANZIBAR ::: SERIKALI ya Mapinduzi  Zanzibar  (SMZ) kupitia Wizara ya Maji, Nishati na Madini imeingiza mapato ya sh. bilioni tatu na milioni hamsini na sita kwa kipindi cha miezi mitatu ikiwa ni mauzo ya maliasili zisizorejesheka ikiwemo kifusi, mchanga  mawe, kokoto na vumbi. Hayo yameelezwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizaya hiyo ambaye amehamishiwa katika Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi, Dkt Mngereza Mzee Miraji wakati akimkabidhi ofisi Katibu Mkuu mpya wa wizara  hiyo  Joseph John Kilangi aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi. Dkt. Mngereza amesema kutokana na changamoto za upotevu wa maliasili kwa kushirikiana na watendaji wake waliamua kuchukua hatua za makusudi kuazisha mfumo wa kuombea maliasili zisizorejesheka ili kuzuia upotevu mali hizo. Hivyo April hadi Juni wizara hiyo imeweza kuingiza fedha hizo  ambapo  mwezi wa Juni pekee uliingiza shilingi bilioni moja na nusu. “Mfumo huu ni mzuri sana kwani unaweza kuo

WADAU WA HABARI ZANZIBAR WATAKA SHERIA ISIYOUMIZA

                                 NA SALUM VUAI, ZANZIBAR; KWA miaka mingi sasa, sekta ya habari visiwani Zanzibar, licha ya kupata mafanikio kadhaa, lakini imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali zinazobana uhuru wa waandishi kutoa na wananchi kupata habari.   Ingawa uhuru umeongezeka kwa kiasi fulani, lakini bado baadhi ya watu wamejenga dhana kwamba waandishi wa habari ni maadui wanaopasa kuogopwa kama nyoka mwenye sum kali.   Mara kwa mara, waandishi wa vyombo vya habari ama wameripoti kunyimwa taarifa au kuamriwa kutozitangaza hasa pale kunapokuwa na matukio yanayoshtua umma ambayo yana chembechembe za uzembe wa viongozi na watendaji wakuu wa serikali.   Hali inakuwa mbaya zaidi pale ambapo hata viongozi wa serikali na taasisi zake wanapokataa kutoa ushirikiano kwa waandishi endapo watabaini wanatafuta ukweli juu ya taarifa zinazogusa maslahi yao binafsi.   Hata hivyo, viongozi kama hao wanakuwa marafiki wakubwa kwa waandishi wanapotaka kutangazwa vizuri na k