Skip to main content

Posts

Showing posts from May 29, 2022

LEO NI SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI, UNANAFASI GANI HAPO ULIPO?

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- MAZINGIRA ni vitu vyote vinavyotunzunguka vyenye uhai na visivyo na uhai.  Vitu vyenye uhai, ni pamoja na mimea na wanyama, lakini visivyo na uhai ni pamoja na hewa, maji na ardhi.  Maisha ya viumbe hai wa kizazi kilichopo na kijacho, hutegemea mahusiano mazuri kati ya watu na mazingira . KWANINI TUYAHIFADHI MAZINGIRA? Hifadhi ya mazingira  ni juhudi zinazofanywa na binadamu, ili kuhakikisha dunia anamoishi usiharibiwe na utendaji wake, bali uweze kuwafaa watu wa vizazi vijavyo. Tunatakiwa tutunze mazingira, kwani tukiyachafua tutapata magonjwa ya mlipuko kama vile kipindu pindu na mengine mengi. SABABU ZA MATOKEO YA UCHAFUZI WA MAZINGIRA Binadamu ndiye anayehusika na uchafuzi wa mazingira, na maendeleo yake ya viwanda na teknolojia na ukuaji wa idadi ya watu ni sababu zingine, zilizo wazi za kuongezeka kwa uchafuzi wa mazingira. Katika miaka ya hivi karibuni, kwa njia hii uzalishaji wa gesi zinazochafua mazingira, uzalishaj

PEGAO, TAMWA, ZAFELA WAUPIGA MWINGI PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: FAMILIA tatu zenye watu wa makundi tofauti wakiwemo wenye ulemavu, na wananchi 82 wamejiunga na elimu ya watu wazima miezi mitano iliyopita, baada ya taasisi za ZAFELA, PEGAO na TAMWA kuibua changamoto hizo. Tasisi hizo kwa sasa, zinaendelea na utekelezaji wa mradi wa miaka minne, wa Ku wawezesha Wanawake Kudai haki zao za uongozi, demokrasia na siasa ‘SWIL’ chini ya ufadhili wa      Ubalozi wa Norway. Akizungumza na waandishi wa habari ofis za PEGAO leo Juni 2, 2022, Mkurugenzi wa Jumuiya hiyo, Hafidh Abdi Said, alisema jengine ambalo limeibuliwa na kufanyiwa kazi, ni kujitokeza wanawake 40 wanaotarajia kuingia kwenye uchaguzi mkuu. Alieleza kuwa, wanawake hao wamedhamiria kuingia kwenye uchaguzi mkuu mwaka 2025, na PEGAO wamejiandaa kuwapa mafunzo, ya kuwajengea uwezo. Hafidhi, alieleza kuwa jengine kwa sasa wameshawafikia wananchi 3,222 kuwapa elimu ya umuhimu wa uongozi kwa wanawake. Kati ya wananchi hao, wanawake waliofikiwa ni 1,971 na wan

MTANGAZAJI ITV AIBUKA MSHINDI WA JUMLA 'EJAT' 2021/2022

  Masekepa Natisa Asangama  wa  Kituo cha Runinga  cha  ITV ameibuka Mshindi wa Jumla wa Tuzo za Umahiri wa Uandishi Habari Tanzania (EJAT) kwa mwaka 2021. Aliwashinda wanahabari wengine watatu  – Nusra Kichongapishi  wa runinga ya mtndaoni ya TIFU , Sanula Athanas  wa  Nipashe  Herieth Makweta  wa Mwananchi. Ansangama  alishinda tuzo mbili  – Tuzo ya Wazi na Utalii na Uhifadhi  kwa runinga. Alitangazwa Mshindi wa Jumla wa EJAT na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye katika kilele cha tuzo hizo kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam Mei 28,2021. Waziri  alimkabidhi  Mshindi huyo wa Jumla Tuzo, cheti  na hundi ya mfano ya kiasi cha sh. Milioni 3. Fedha hizo zimetolewa na mshiriki kiongozi wa EJAT , Baraza la Habari  Tanzania, kumwezesha  mshindi huyo kujiendeleza kwa masomo. Kushinda Tuzo ya Wazi  aliwashinda watangazaji wawili wa kituo cha runinga cha Star – Naishook Alais Makaseni  na  Sudi Shaaban  Ally  na kwa Tuzo ya Uhifadhi na Uhifadhi alikuwa

NDIMARA MWANDISHI NGULI TANZANIA AIBUKA MSHINDI

  Mhariri mkongwe, mchapishaji na mkufunzi,  Ndimara Tegambwage,  ametunukiwa tuzo ya Mafanikio ya Maisha ya Uandishi wa Habari (LAJA) kwa mwaka 2022.   Waziri Mkuu , Kassim Majaliwa, aliyemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kama Mgeni Rasmi wa sherehe za Tuzo  za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania   (EJAT) 2021  zilizofanyika  katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam alimkabdihi  Ndimara Tuzo ya LAJA . Pia  alimkabidhi hundi ya mfano ya sh. milioni  10  kama zawadi ya LAJA. Jina la Ndimara kama mshindi wa  LAJA  lilitangazwa na Waziri wa  Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye  baada ya  mtangazaji veterani  Rose  Haji  kusoma  wasifu wake. Ndimara  ana uzoefu mkubwa wa zaidi ya miaka 40 katika vyombo vya habari. Miongoni mwa michango yake katika tasnia ya habari alikuwa mmojawapo wa waliochagiza kuanzishwa  kwa Baraza la Habari la Tanzania (MCT) la wanahabari wenyewe  na kuanzisha ofisi ya  Taasisi ya Habari Kusini mwa Afr

SABABU YA KUFUNGWA JELA MAISHA HII HAPA

  Mahakama ya Wilaya Nkasi Mkoani Rukwa imemhukumu kifungo cha maisha jela Peter Malema (21) Mkazi wa Kijiji cha Nkundi Kata ya Kipande Wilayani Nkasi kwa kosa la kumbaka Mtoto wa miaka 4. Akitoa hukumu hiyo Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya Benedict Nkomola amesema Mahakama hiyo imefikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha na ushahidi uliotolewa pasipo shaka yoyote na kumtia hatiani kwa kosa hilo. Upande wa mashitaka ukiongozwa na Waendesha mashitaka Denis Chagike na Sedrick Mashauri wameieleza Mahakama hiyo kuwa Mtuhumiwa alitenda kosa hilo March 23, 2021 katika Kijiji cha Nkundi ambapo alimbaka Mtoto huyo wa miaka 4 na kumsababishia maumivu makali. "Mtuhumiwa hili ni kosa lake la pili la ubakaji na katika kosa la kwanza aliwai kuhukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na aliondolewa baada ya kushinda rufaa" (chanzo Milard Ayoo)

HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU ZAZIDI KUPIGIWA CHAPUO

                                    NA ZUHURA JUMA, PEMBA USHIRIKIANO unahitajika zaidi katika kuhakikisha kunakuwa na ukondoishwaji wa masuala ya watu wenye ulemavu, ili wapate haki zao za msingi. Akiwasilisha mada katika mkutano wa Mtandao wa Wilaya wa Mpango Jumuishi wa Maendeleo katika Jamii (CBID), Mshauri kutoka Shirika la watu wenye ulemavu la Norwey (NAD) Christine Cornick alisema, wamekuwa wakifanya kazi na mtandao huo, ili kuisaidia kuleta mabadiliko katika jamii. Alisema kuwa, ushirikiano wa pamoja ndio utakaoleta nguvu ya kufanya kazi na kuleta mabadiliko ya haraka katika ukondoishaji wa masuala ya watu wenye ulemavu katika nchi mbali mbali. "Katika mtandao huu tumeshirikisha watu mbali mbali, wanakuwa na sehemu ama mahala ambapo wanakutana na kubadilishana uzoefu katika ngazi mbali mbali na kutoa maamuzi ya kujenga jamii iliyobora", alisema Mshauri huyo. Alifahamisha kuwa, watu wenye ulemavu wamekuwa wakikosa huduma zao za msingi, jambo ambalo linasababisha kudha