Skip to main content

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......


 


NA HAJI NASSOR, PEMBA

MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao.

Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando.

Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo.

Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao.

“Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Mbunge huyo wa viti maalum wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asya Sharif Omar, alisema, viongozi wa CCM wataendelea kutekeleza ahadi kwa wananchi mbali mbali, bila ya kujali itakadi zao.



Kuhusu sensa ya watu na maakazi, zoezi linalotarajiwa kufanyika mwaka huu, aliwataka wananchi wasipuuze na kushiriki kikamilifu.

“Lengo kuu la sena hii, ni serikali kupata idadi halisi ya wananchi wake, ili sasa ipange mipango na mikakati ya kweli, maana kinyume chake, ni kufanya kazi kwa kubahatisha,’’alifafanua.

Hata hivyo, amewasisitiza wananchi hao wasisite kuchangia huduma ya maji safi na salama, ili Mamlaka ya Maji Zanzibar ‘ZAWA’ kwao iwe rahisi kurekebisha miundombinu inapoharibika.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Gando Salim Mussa Omar, alisema moja ya vipaumbele vyake ni kuona wananchi wote wanapata huduma za lazima.

Alieleza kuwa, huduma ya maji safi na salama ni moija wa msingi mkuu wa wananchi, katika kufanikisha mikakati yao ya maisha ya kila siku.

“Ni kweli, hapa kijiji cha Taifu shehia ya Kinyasini wakati napita kuomba kura, nililalamikiwa juu ya ukosefu wa huduma ya maji safi na salama, na nikawaahidi,’’alifafanua.

Alisema, alishirikiana na wananchi pamoja na ZAWA hadi kufanikisha mradi huo, ambao sasa wananchi kadhaa watafaidika na kusahau kero ya miaka 14.

Katika hatua nyingine, amesema atakuwa karibu mno na ZAWA, ili kuona mradi huo haufi, kwani kuwarejesha tena wananchi kwenye dhiki waliyokuwa nayo, ni hasara.

Hata hivyo Mbunge huyo amesema, bado Gando mpya aitakayo haijafikia, ingawa kwa sasa mipango na mikakati yake, ikiwemo ujenzi wa matangi ya kuhifadhia maji yameshaanza.



Mwananchi Hamad Nassor Hamad, alisema kazi iliyofanywa na Mbunge wao, lazima waithamini kwani, imewafanya wazaliwe upya kwenye huduma ya maji safi na salama.

Aisha Kombo Hassan, alisema sasa mikakati yao ya kujiletea maendeleo yamepungua changamoto, kwani awali walilazimika kutumia maji ya kuokota.

“Ilikuwa alfajiri kubwa, inatubidi tuamke na kufuata huduma hiyo mabondeni tunakoendesha kilimo, na wala hayako salama, lakini leo twamshukuru Mbunge wetu,’’alieleza.

Hata hivyo Kazija Hija Makame, alisema kazi iliyobakia sasa ni kuendelea kuilinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yadumu kwa muda mrefu.

Kijiji cha Taifu shehia ya Kinyasini, Jimbo laGando wilaya ya Wete mkoa wa kaskazini Pemba, chenye wakaazi 823, kilikosa huduma ya maji safi na salama kwa miaka 14, na kulazimika kutumia maji ya visima vya kata.

                                         Mwisho  

 

Comments

  1. Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na akaondoka kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki yangu aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu ili kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.

    Mwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwa ajili yangu - na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.

    Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.

    Lakini sio hivyo tu - Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyozunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.

    Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote - huzuni, bahati mbaya, au kuchanganyikiwa - usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.

    Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159

    dawnacuna314@gmail.com

    ReplyDelete
  2. Ukiwa umefanya kazi maisha yako yote kujenga familia na urithi, huwezi kuruhusu kivuli cha mtu wa tatu kiiharibu katika miezi michache tu. Niligundua kuwa mabadiliko ya ghafla ya tabia ya mume wangu yalikuwa kuingiliwa kiroho, si tu mgogoro wa katikati ya maisha.

    Niliwasiliana na Mystic Kakaa kwa ajili ya uingiliaji kati wa kibinafsi. Kazi yake ilikuwa ya upasuaji. Alitambua kivuli na kukiondoa kabisa bila drama yoyote ya umma. Ndani ya siku 5, umakini wa mume wangu ulirudi nyumbani kwetu na katika mustakabali wetu. Ikiwa unalinda maisha yenye thamani kubwa na unahitaji bwana anayeelewa busara, wasiliana naye kwa: dawnacuna314@gmail.com

    WhatsApp: +2349046229159

    Yeye ndiye kiwango cha dhahabu.
    Kwa uchawi wa upatanisho wa uhusiano/ndoa.

    Uchawi wa kumfanya mpenzi wako wa zamani/mwenzi wako aombe msamaha.

    Uchawi wa kumrudisha mpenzi wako/kumvutia mpenzi mpya.

    Uchawi wa kurejesha mali/pesa zilizoibiwa.

    Mabadiliko ya umbo/Uchawi wa kutoweka.

    Uchawi wa kushinda bahati nasibu/kesi ya mahakama. Na zaidi

    ReplyDelete

Post a Comment