Skip to main content

WAZIRI WA FEDHA TANZANIA ''TRA' KUKUSANYA SH/= 42 TRILIONI MWAKA 2026/2027

 


NA TATU MAKAME, ZANZIBAR@@@@

WAZIRI wa fedha Tanzania Balozi Khamis Mussa Omar amesema Mamlaka hiyo inatarajia kukusanya shilingi trilioni 42 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 katika maeneo mbalimbali ya Tanzania ili kuimarisha ukuaji wa uchumi hapa nchini.

Alisema hayo Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja kwenye hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) ikiwa ni muendelezo wa tamasha la Kizimkazi fastival. 

Alisema mapato hayo kutoka vyanzo vya ndani kwa robo tatu ikiwemo ulipaji kodi kwa wafanyabiashara na kueleza kuwa kwa mwezi ulioanzia Julai mwaka huu mamlaka hiyo ilikusanya zaidi ya bilioni 800 sawa na ongezeko la asilimia 21 ya makusanyo.

Alisema ukusanyaji mapato unaimarika kila mwaka kwani mwaka wa fedha 2024,2025 Mamlaka ilifikia asilimia 1003 huku mwaka 2025_2026 kiwango cha mapato kilifikia asilimia 1005 kwa Tanzania nzima katika maeneo yote ya yanayokusanywa kodi.

Aidha aliwataka wafanyabiashara kulipa kodi kwa hiari kwani ukusanyaji huo wa kodi ni mzunguuko wa uchumi ambao utawezesha ujenzi wa miundombinu katika maeneo mbalimbali ya Tanzanzia.

"Tumejipanga kuimarisha mifumo na huduma kila mikoa kurahisisha ulipaji kodi kwa wafanyabiashara", alisema.

Alieleza kuwa katika kikao cha bajeti cha kuu ya serikali mwaka huu kilichofanyika Bungeni Dodoma serikali iliamua kutenga mfuko maalum ambao utakaotumika kwa ujenzi wa miundombinu kama ujenzi wa barabara,skuli,maji,afya na huduma nyengine za jamii ikiwemo majengo ya Ofisi za serikali na kueleza kuwa fedha zitakazokusanywa na TRA asilimia 70 zitumike kwa ujenzi wa shuhuli hizo za kijamii.



 Sambamba na hayo alisema kati ya fedha zitakazokusanywa shilingi bilioni 5  60 zitatumika kwa ujenzi wa nyumba za watendaji wa mamlaka hiyo sehemu za mipakani lengo kurahisisha ukusanyaji wa mapato pamoja na kuongeza ufanisi kwa watendaji hao.

Alisema kazi inayofanywa na mamlaka hiyo ya kuwahimiza wafanyabiashara kulipa kodi kwa hiari imelenga kuendelea ujenzi kwani ukuaji huo ni ishara ya kukua kwa uchumi wa Tanzania.

Alitumia nafasi hiyo kueleza kuwa ukuaji wa uchumi umechangia ujenzi wa miradi ya maendeleo katika sekta mbalimba hasa ujenzi wa skuli,barabara ,afya na huduma nyengine za jamii.

Nae Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA )Yusuph Juma Mwenda akitoa taarifa ya ujenzi wa jengo la Ofisi ya TRA Kizimkazi alisema ujenzi huo wa ghorofa moja utatoa huduma kwa wakaazi wa Kizimkazi na Paje pamoja na maeneo mengine ili kusogeza huduma za ulipaji kodi kwa wafanyabiashara.

Alisema ofisi hiyo itagharimu shilingi bilioni 3,6,000,000 hadi kukamilika kwake na kueleza kuwa ofisi kama hizo zimejengwa katika mikoa zaidi ya 33 ya Tanzania na kueleza kuwa kila wilaya ujezni wa Ofisi hizo utaendelea.
 
Sambamba na hayo aliwapongeza wakandarasi wa ujenzi kwa jengo hilo linalokwenda kwa kasi na kueleza kuwa kumalizika kwake kutarahisisha utoaji huduma.

Nae mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja Othman Ali Maulid akimuwakilisha mkuu wa mkoa wa mkoa wa kusini Unguja Hamida Mussa Khamis alisema mkoa huo uko salama katika kuimarisha ulinzi na usalama.

Aliwapongeza viongozi wakuu wa nchi kwa kuimarisha miundombinu ya sekta mbalimbali ikiwemo ya ujenzi wa barabara na sekta nyengine za kijamii.

MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...