Skip to main content

Posts

Showing posts from April 7, 2024

MWANI: ZAO LINALOWABEBA WANAWAKE KIUCHUMI, BIDHAA ZAKE ZAONGEZA MYORORO WA THAMANI

  NA MUZNAT KHAMIS, ZANZIBAR@@@@ TOFAUTI na vilimo vyengine tulivyovizoea ambapo mkulima hulazimika kuchimba ardhi kwa kutumia jembe ama zana nyengine, kuweka mbegu, mmea huanza kuota na tofauti na mwani ambao hulimwa kwenye maji ya bahari.   Kilimo cha mwani kilianza mwishoni mwa mwaka miaka ya 1980 hapa Zanzibar, ambapo wanaume wakiwa kwenye hatari za uvuvi wanawake walizana kuingia kwenye kilimo hicho.   Hata hivyo, wanawake wengi hapo awali waliokuwa wakijishughulisha na kilimo cha mwani ni wale waliokuwa kwenye mazingira magumu wakiwemo wajane, ambao ndio waliokiona kilimo hicho kuwa mkombozi.   Umaarufu wa kilimo hicho zaidi unatokana na faida zake kiuchumi na kwa sababu wakulima wengi wa zao hilo hapa Zanzibar ni wanawake, ina maanisha kwamba zao hilo limekuwa moja ya nguzo ya kiuchumi katika maisha ya akina mama Zanzibar.   Makala haya yanalenga kuangalia japo kwa ufupi sana namna zao hilo linavyowanufaisha kiuchumi akina mama na namna zao hilo lilivyobadilish

WAISLAM MTEMANI WAWI WAKUMBUSHWA JAMBO BAADA YA RAMADHAN

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAUMINI wa dini ya kiislamu kijiji cha Mtemani, shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake Pemba, wamekumbushwa kuyaendeleza mema yote waliyokuwa wakiyatenda katika mwezi mtukufu wa Ramadhan, kwani amri na makatazo hayo waliyokuwa wakiyatii, bado yanaendelea kuwepo. Hayo yameleezwa na khatibu wa msikiti wa Mtemani Wawi wilaya ya Chake chake Salim Nassor, wakati akitoa hutuba mbili za swala ya Edi-l Fitir, mara baada ya kukamilika kwa swala hiyo, iliyofanyika msikitini hapo leo April 10, 2024. Alisema, hipendezi na haingii akilini kuona waumini wa dini ya kiislamu waliokuwa wakifuata maamrisho ya Muumba, katika mwezi mtukufu wa Ramadhan na kisha sasa amri hizo, kuzipindua na kufanya watakavyo. Alieleza kuwa, Muumba aliyekuwepo katika mwezi uliomalizika, ndio yule yule aliyepo katika miezi mingine, hivyo ni wajibu wa waumini hao kuendelea kumtii, ili kupata radhi zake. Khatib huyo alifafanua kuwa, katika kipindi cha mfungo, kila mmoja alikuwa laini mbele ya

MKAGUZI WA POLISI AKERWA WANAOTUMIA BANDARI BUBU KUSAFIRISHIA BIDHAA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ WANANCHI wa shehia ya Mjananza Wilaya ya Wete Pemba wametakiwa kushirikiana pamoja kuhakikisha bandari zilizopo kwenye shehia yao hazitumiki vibaya. Akizungumza na wananchi wakati wa ziara ya kukagua bandari bubu, Mkaguzi wa shehia hiyo Inspekta wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Khalfan Ali Ussi alisema, ni vyema bandari hizo zikatumika vizuri ili zisiwaingize kwenye makosa. Alisema kuwa, siku zote bandari bubu hutumika vibaya kwa baadhi ya wananchi kusafirisha bidhaa kwa njia ya magendo, hivyo wananchi hao hawana budi kushirikiana pamoja kuhakikisha hawaruhusu kupitishwa bidhaa, kwani ni kosa kisheria. "Suala la ulinzi na usalama wa bandari hizi sio la watu maalumu bali ni la wananchi wote, hivyo kila mmoja kwa nafasi yake ana wajibu wa kuzilinda bandari hizo ili zisitumike vibaya," alisema Khalfan. Aidha aliwataka wanajamii hao kutoa taarifa kwa vyombo vya ulinzi pale tu watakapoona kuna bidhaa ama vitu vimeingizwa, kwani wanaofanya hivy

MaDC, MASHEHA, MADIWANI MKOANI WAPEWA DOZI KUHUSU MIPANGO MIJI

  NA ASHA ABDALLA, PEMBA @@@@ WAKUU wa wilaya, Masheha na Madiwani  wametakiwa kushirikiana kwa pamoja katika kuwaelimisha wananchi kuhusiana na mipango miji, ambayo itaweza kuwasaidia wananchi wote kuwa na makaazi yenye hadhi kisiwani Pemba.  Hayo yameelezwa na Salma Abdalla Ali kutoka Idara ya mipango miji na vijiji kamisheni ya Ardhi Pemba, kwanyakati tofauti, wakati walipokua wakitoa mafunzo ,huko wilayani  Mkoani Mkowa wa Kusini Pemba.  Alisema kua Mipango miji imekuja kwa ajili  ya kuwapimia Wananchi maeneo ambayo hajawahi kupimwa hususani yale ambayo hayajafanyiwa ujenzi, ili waweze kupunguza migogoro mbalimbali ambayo inajitokeza ndani ya jamii. Aidha alisema kuwa Idara ya Mipango miji wanakazi kubwa ya kuelimisha jamii, kupitia vipindi mbalimbali vya redio na tv, kwani wanachi bado wanauwelewa mdogo kuhusu mipango miji. Hata hivyo alisema kuwa, wanatarajia kupanga eneo kwa kila wilaya, ambalo litaweza kuimarisha mji ambalo litaweza kutumika kwa matumizi mbalimbali ya wananchi 

WANAOTUMIA BARA BARA MKOANI-CHAKE CHAKE WAIKUMBUSHA SERIKALI UJENZI

   NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wanaotumia barabara ya Mkoan-Chake chake, wameikumbusha serikali kuanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami, ili waitumie kwa utulivu wanapokuwa katika harakati zao za maendeleo. Walisema, kwa sasa barabara hiyo imekuwa kero kwao, kutokana na uwepo wa mashimo, misingi, na mipasuko mipana ambayo wakati mwingine husababisha ajali ambazo zinaweza kuepukika. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, baada ya kutokezea ajali hivi karibuni eneo la Ngezi, walisema, mashimo ambayo huongezeka kila mvua zinaponyesha, ndio chanzo cha ajali. Mmoja kati ya wananchi hao Anuwari Is-haka Omar wa Matuleni, alisema wakati umefika sasa kwa serikali kutimiza ahadi ya ujenzi wa barabara hiyo. ‘’Kwa muda mrefu tumekuwa tukiskia kuwa ujenzi wa barabara hii, utaanza wakati wowote, lakini hadi sasa imeshapita miaka hatuoni kinachofanyika,’’alisema. Kwa upande wake Mwanaisha Omar Haji wa Kipapo, alisema katika eneo la Chanjamjawiri, limekuwa maarufu kwa