Skip to main content

Posts

Showing posts from May 8, 2022

RC KUSINI PEMBA 'KADA YA SHERIA ITABAKI NGUZO MUHIMU KWA JAMII'

    MKUU wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, amesema kada ya sheria itaendelea kuwa eneo muhimu katika jamii. Alisema, kwa kulitambua hilo Serikali, iliamua kutunga sheria mahusisi ya msaada wa kisheria nambari 13 ya mwaka 2018, na kuanzishwa Idara ya Katiba na Masada wa Kisheria, ili kuwafia wananchi kuwapa elimu, ushauri na msaada wa kisheria.   Alisema idara hiyo imekua ikifanya kazi kubwa katika masuala mbali mbali ya msada wa kisheria Zanzibar, ili kuona wananchi wasio na uwezo wanapata haki zao za kisheria. Mkuu huyo aliyasema hayo Mei 12, mwaka 2022 wakati akiyafungua mafunzo ya kwanza ya siku 15 kwa wasaidizi wa sheria 15 wa majimbo yote kisiwani, yanayoendelea Gombani Chake chake. Alisema kada ya wasaidizi wa sheria, inasaidia kwa kiasi kikubwa  kuwafahamisha wananchi hususani wa ngazi za chini katika jamii, juu ya haki zao za kisheria na namna ya kufuatilia. “Mafunzo haya ni muhimu kwenu washiriki, ili mukitoka hapa muweze kwenda kutekeleza majukumu yenu kwa uweledi

CHAMA CHA MADEREVA KUSINI PEMBA CHANG'AKA NAULI MPYA YA DALADALA

  NA HANIFA SALIM, PEMBA CHAMA cha Wamiliki wa gari za abiria na mizigo Mkoa wa Kusini Pemba ‘PESTA’ kimesema hakitambui uwepo wa nauli mpya wa gari za abiria, katika Mkoa huo kama wanavyofanya baadhi ya madereva na makondakta. Kimesema, kwa sasa madereva wanapaswa kuendelea kuwatoza abiria wao nauli kongwe, na sio mpya kama ambavyo wanafanya baadhi yao. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu, Katibu wa chama hicho Pemba, Hafidh Mbarka Salim amesema, hana taarifa ya kuwepo kwa nauli mpya, kwa gari za abiria. Alieleza kuwa, anachofahamu ni kuwa tayari ‘PESTA’ imeshapeleka maombi ya mchanganuo wa nauli mpya, kufuatia wamiliki wa gari hizo kukumbwa na changamoto kadhaa, ikiwemo kupanda bei ya mafuta. ‘’Kwa sasa hakuna mmiliki wa gari wala dereva, aliyeruhusiwa kupandisha nauli mpya, na badala yake zitumike nauli kongwe hadi pale tangazo litakapotolewa,’’ alisema. Hafidh alifafanua kuwa, katika muongozo huo wa maombi walioutuma serikalini, pamoja na upandaji w

MASHEHA PEMBA WAKUMBUSHWA JAMBO KUHUSU UVIKO 19

  NA JAFFAR ABDALLA, PEMBA MASHEHA Kisiwani Pemba, wamehimizwa kuendeleza juhudi za kuwahamasisha wananchi, kujitokeza kuchanja chanjo ya kujikinga dhidi ya ugonjwa wa Uviko19, ili kujiepusha na maambukizi ya maradhi hayo. Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Kitengo cha elimu ya Afya Zanzibar, Bakar Hamad Magarawa, wakati akifungua mafunzo ya siku moja, yaliyowashirikisha masheha na watendaji wa Wizara ya Afya, mkutano uliofanyika Samail Chahe chake Kisiwani Pemba. Alisema, bado zipo baadhi ya shehia  idadi ya wananchi wanaojitokeza kupata chanjo hiyo ni ndogo, hivyo ipo haja kwa masheha, kuwaelimisha wananchi wao kuchukua tahadhari kwa kupata chanjo hiyo. Aidha Bakari amewatoa hofu wananchi kuwa, chanjo hiyo ni salama na haina madhara yoyote, ambayo yananaweza kuathiri afya zao, wanapopatiwa chanjo hiyo na kuacha dhana yakuwa chanjo hizo zinamadhara. ‘’Nawasihi masheha muendelee kuhamasisha wananchi wenu kuchanja chanjo hii, kwani kuna baadhi ya shehia idadi ya walio chanja iko

POLISI LATAJA SABABU KUMPA DHAMANA DAKTARI MTUHUMIWA UBAKAJI PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA JESHI la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, limekiri kumpa dhamana ya kipolisi daktari wa kituo cha afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, ambae ni anatuhumiwa kwa kumtorosha na kisha kumbaka mgonjwa wake, ambae ni mtoto. Kamanda wa Polisi mkoani humo, Juma Sadi Khamis, wakati akitoa taarifa hiyo kwa vyombo vya habari, alisema sababu za kumpa dhamana, ni kufuatia mtoto huyo kutaja watu wawili tofauti. Alisema, mtoto huyo alimtaja daktari huyo na mtu mwengine ambae kwa sasa, wanaendelea kumtafuta, hivyo wameona wampe dhama mtuhumiwa huyo hadi wote wawili watakapopatikana. Alieleza kuwa, mtoto huyo alimtaja daktari kwa sababu alikwenda kupata huduma, ingawa yuko mtu mwengine aliyemfanyia kitendo hicho. ‘’Kwa sasa baada ya kuona mtoto huyo anafanya ubabaifu, daktari ambae tulikuwa tunamshikilia tumeshampa dhamana kwa muda,’’alifafanua Kamanda huyo. Aidha Kamanda huyo, alieleza kuwa kwa sasa suala hilo linaendelea kupelelezwa kwa kina, na kisha Jeshi hilo litat

TUME YA UTANGAZAJI ZANZIBAR YAOTA MENO KWA VYOMBO VYA HABARI

  NA RAHIMA MOHAMED TUME ya Utangazaji Zanzibar imesitisha leseni za utangazaji kwa muda wa miezi sita kwa vituo vitatu vya redio na kuvifungia vituo viwili vya televisheni kwa muda usiojulikana  baada ya kukiuka masharti yaliyowekwa na tume hiyo. Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale, Kikwajuni mjini Zanzibar, Katibu Mtendaji wa tume hiyo, Suleiman Abdulla Salim, alisema wamefikia uamuzi huo baada ya kugundua ukiukwaji wa leseni ya utangazaji kwa vituo hivyo. Alieleza kuwa tume inafuatilia kwa ukaribu kabisa vituo vyote vya utangazaji na haitosita kuchukua hatua za kisheria kwa wale watakaotoa huduma ya utangazaji bila ya kuwa na leseni inayotambulika kisheria. Akivitaja vituo vilivyofungiwa kwa muda wa miezi sita ni redia ya Bomba fm  ambayo imekwenda kinyume na masharti yaliyowekwa kwa kurusha matangazo tofauti baina ya Zanzibar  na Dar essaalam, Assalam FM  pamoja na AM 24 FM ambazo  zimebadili muundo wa hisa ya kampuni bila ya kuridhiwa

HII HAPA HAKI ILIYOJIFICHA YA WATUMISHI WA UMMA WANAUME ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, PEMBA AMA kweli, ukitaka kukificha kitu, kitie kwenye maandishi. Wengi wamekuwa wakiyasema hayo, wakiwa na maana kuwa, ule utamaduni wa kusoma, sasa umeondoka. Kumbe kwenye maandishi kama ya sheria, kanuni na sera zilizotungwa kwa ajili ya kundi fulani, hukosa kutekelezwa kwa waliotungiwa, kwa kutosoma. Aliwahi kuwapa chagamoto wananchi Mkoani Pemba, aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Zanzibar Jaji Mashibe Ali Bakari, alipotakiwa kujibu juu ya sheria za Zanzibar kuwa lugha ya kigeni. ‘’Sheria za Zanzibar tunatungiwa sisi wananchi ambao lugha yetu mama ni Kiswahili, lakini zipo kwa lugha ya kugeni, hapa si mnataka kutufunga,’’alihoji Mohamed Abass sheha mstafu wa Kinyasini. Jaji Mshibe akawambia kuwa, utamaduni wa kusoma hata kwa nyaraka zilizoandikwa kwa lugha ya kiswahili sasa haupo, na ukitaka kukificha kitu kitie kwenye nyaraka. SHERIA NA KANUNI YA UTUMISHI WA UMMA 2014 Sasa ni miaka 19 imeshapita, tokea serikali ya Mapinduzi ya Za

KESI YA ANAYEDAIWA KUMLAWITI KIJANA MWENYE ULEMAVU WA AKILI PEMBA KUENDELEA LEO

   NA FATMA HAMAD, PEMBA WAKILI wa serikali Juma Mussa Juma, ameiomba Mahkama ya mkoa ‘B’ Wete, kulighairisha shauri la ulawiti la kijana mwenye ulemavu wa akili, linalomkabili Nuhu Kombo Nuhu, hadi hapo atakapofanyiwa uchunguuzi, baada ya wiki iliyopita kujifanya kiziwa mahakamani hapo. Awali mtuhumiwa huyo, aliwashangaaza watendaji wa mahkama na wengine waliokuwepo mahkamani, hapo baada ya ghafla kuonekana kiziwi na kushindwa kujibu maswali, hali iliyopelekea Mahakama kuagizwa kufanyiwa uchunguuzi.   Hivyo Mwakili huyo wa serikali, ameleza mahkamani hapo, kwamba tarehe iliyopita upande wao uliomba mahakama   kumpeleka Hospital mtuhumiwa huyo, na mahkama kukubaliana na hilo. ‘’Nilitarajia leo Mheshimiwa hakimu, awepo mtaalamu mwenye majibu ya mtuhumiwa, maana wiki iliyopita alikuwa hawezi kuzungumza ‘bubu’ na agizo lako likawa ni kufikishwa hospitali kwa uchunguuzi,’’alihoji Wakili huyo. Hata hivyo Wakili huyo, alioneshwa kushangaazwa kwake hadi kufikia tarehe ya shauri hilo

DK. MWINYI AWAFURAHISHA WATUMISHI WA UMMA ZANZIBAR

    NA MWANDISHI WETU, IKULU RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema kwa mwaka wa fedha 2022/2023, serikali itaongeza mshahara kwa kutumia utaratibu wa kuwapanga watumishi katika madaraja na vyeo kwa mujibu wa miundo ya utumishi kwa kuzingatia elimu zao pamoja na uzoefu wa kazi. Rais Dk. Mwinyi aliyasema hayo huko katika viwanja vya Maisara kwenye hotuba yake aliyoitoa ya kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), ambapo kwa Zanzibar sherehe hizi zimefanyika hivi jana, hii ni kufuatia kuwapa wananchi wa Zanzibar muda wa matayarisho ya skukuu ya Idd el Fitr. Rais Dk. Mwinyi alisema kuwa ana imani kwamba ongezeko la mishahara litakalofanywa litakuwa na mchango katika kuimarisha uwezo wa watumishi wa umma kujikimu kimaisha pamoja na kuondoa kilio cha muda mrefu kwa watumishi wa umma ambapo elimu na uzoefu wao wa kazi haukuwa ukijitokeza wazi wazi katika marekebisho ya mshahara yaliyofanywa vipindi vilivyopita.

WATAHINIWA 95,955 KUANZA MITIHANI KIDATO CHA SITA LEO TANZANIA

  NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM JUMLA ya watahiniwa 95,955 kutoka shule za sekondari 841 na vituo vya kujitegemea 250 wanatarajia kuanza mitihani yao ya kumaliza kidato ya sita leo Tanzania bara na Zanzibar. Hayo yameelezwa leo na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), Dk. Charles Msonde wakati akizungumza na waandishi wa Habari na kueleza kuwa pia watahiniwa 9,670 kutoka vyuo 70 wamesajiliwa kufanya mitihani ya mwisho ya mafunzo ya ualimu katika ngazi ya stashahada na cheti. Dk. Msonde alisema kati ya watahiniwa wa kidato cha sita, 85,531 ni waliopo skuli na 10,424 ni wa kujitegemea. “Kati ya hao wanaume ni 47,859 ni sawa na asilimia 55.96 na wasichana ni 37,672 sawa na asilimia 44.04. Pia wapo watahiniwa wenye mahitaji maalumu 151, kati yao 136 ni wenye uoni hafifu na 15 ni wasioona kabisa,” alisema Dk. Msonde. Alifafanua kwamba kati ya watahiniwa wa kujitegemea 10,424 waliojisajili, wanaume ni 6,546 sawa na asilimia 62.80 na wanawake ni 3,878 sawa ana silimia 37.