Skip to main content

Posts

Showing posts from November 16, 2025

WIZARA YA AFYA KUIMARISHA UTOAJI HUDUMA KWA WATU WENYE ULEMAVU

NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ WIZARA ya Afya Pemba imesema, itaendelea kuboresha mifumo ya utoaji huduma na upatikanaji wa huduma za afya kwa watu wenye ulemavu, kama sheria zinavyo elekeza. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Afisa mdhamini wa wizara hiyo Pemba Khamis Bilali Ali alisema, ili kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata huduma bora kama ilivyo kwa wengine, wizara i ta hakikisha hospitali zinawekwa njia za kupitia watu wenye ulemavu (Ramp) ili kupita kwa urahisi  pale wanapofika kufuata huduma. Alisema jambo jengine linalotekelezwa ni kutoa maelekezo kwa watoa huduma za afya kuhakikisha wanatoa kipaombele kwa watu wenye ulemavu wanapofika hospitalini, kama kanuni zinavyo eleza ili kuhakikisha watu hao wanapata haki yao ya msingi ya afya bila ya usumbufu. “Tumeweka (Ramp) pia kuna kanuni zinazo wataka watoa huduma kutoa kipaombele kwa wenye ulemavu na wizara inasimamia kwakaribu suala hili na linafanyika”, alieleza. Alisema ingawa kuna changamoto ya wakalimani ...

WATU WENYE ULEMAVU NA USHIRIKI WA MICHEZO, BADO KIZUNGUMKUTI, WIZARA YAJITUTUMUA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘’WATU wenye ulemavu wanastahiki haki zote za msingi za binaadamu, sawa na watu wingine, ikiwemo michezo na burudani,’’inaeleza sheria yao. Sheria hiyo nambari 8 ya mwaka 2022, ikazidi kufafanua kwenye kifungu cha 28 (1) (f), kwamba kundi hilo linastahiki haki zote za msingi, bila ya ubaguzi.   Tena uzuri zaidi kifungu cha 29 (1), kikamtamka kuwa, Baraza la Taifa la Watu wenye ulemavu, katika kuiendea haki hiyo, litahakikisha ufikiaji wa maeneo hayo. Kikafafanua kuwa, lazima pawepo na miundombinu rafiki ya kuyafikia majengo ama maeneo kwa watu wenye ulemevu, wanapoziendea haki zao michezo na burudani. Kifungu cha 30, kikasisitiza kuwa, kila mmoja anawajibu wa kutekeleza, kulinda na kutetea haki za watu wenye ulemavu, kwa kutoa taarifa za uvujifu wa haki hizo. Eneo jingine sera ya maendeleo ya taifa ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2004, Ibara yake 3.15 ikazitaka nchi, kuhakikisha wanawekewa utaratibu utakaohakikisha watu wenye ulemavu, wan...

'THBUB' WAPIGWA MSASA MIFUMO UTENDAJI KAZI

  NA MWASHAMBA JUMA, THBUB@@@@ NAIBU Katibu Mtendaji Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Bw. Juma Msafiri Karibona amepongeza juhudi za watumishi wa tume hiyo kujengeana uwezo na kubadilishana uzoefu katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku. Karibona aliyasema hayo alipofungua mafunzo ya Mifumo ya Utendaji kazi kwa tume hiyo ya kujengeana uwezo baina ya watumishi wa tume hiyo yaliyofanyika ofisini kwao Mombasa, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini Magharibi, Novemba 19, 2025. Aidha, alisifu hatua ya watumishi hao kujijengea uthubutu na kujiongezea uelewa mpana hasa katika kufuatilia na kuyafanyia kazi matumizi ya mifumo katika utendaji kazi wao za kila siku ili kuendana sambamba na mabadiliko ya teknolojia. Akiuzungumzia mfumo wa Utumishi wa utendaji wa “ESS” moduli ya “PEPMIS” Naibu Karibona aliwahimiza watumishi hao kuendelea kuufanyia kazi mfumo huo kwa wakati ili kuendana sambamba na majukumu yao ya kila siku huku akiwatanabahisha watumishi hao ku...

HUDUMA ZA AFYA KWA WATU WENYE ULEMAVU SIO NGUMU WALA LAINI

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA DUNIA inapaswa ielewe kuwa, watu wenye ulemavu ni sawa na watu   wingine katika jamii. Wana haki ya kunufaika na kupata haki zote za msingi ikiwemo ya afya. Haki ya afya kwa watu wenye ulemavu imetamkwa na kuelezwa kwenye sera na sheria za kimataifa, kikanda na kitaifa. Hapa Mkataba wa Kimataifa wa Haki za watu wenye ulemavu wa mwaka 2006, ibara ya 25, imesisitiza watu wenye ulemavu wana haki ya kupata huduma za afya bila ubaguzi. Huku Sheria ya Watu wenye Ulemavu ya Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022 nayo kwenye kifungu cha 28, kikisisitiza watu wenye ulemavu wanastahiki kupata haki zote za msingi ikiwemo ya afya. “Watu wenye ulemavu wanastahiki kupata huduma za afya kama matibabu, matengenezo na marekebisho yanayohusiana na ulemavu,” kinafafanua kifungu hicho. Hii inaonyesha, jinsi gani ulimwengu umewazingatia   watu wenye ulemavu katika upatikanaji wa haki zote za msingi ambao ndio haki za kibinaadamu. Kwani watu wenye ulemavu n...