Skip to main content

Posts

Showing posts from March 10, 2024

PP AMSOTESHA RUMANDE ANAYEDAIWA KUUA KWA MAKSUDI

    NA MARYAM NASSOR, ZANZIBAR@@@@ MTUHUMIWA   wa kesi ya kuua kwa makusudi, inayosikilizwa mahakama kuu Tunguu Zanzibar, inayomkabili Omar Mahmoud Abdallah (36) mkaazi   wa Jang’ombe Unguja, ameendelea kusota rumande, baada ya upande wa mashtaka,   kushindwa   kukamilisha   upelelezi wa shauri hilo kwa wakati.   Mara baada ya kufika mahakamani hapo, mtuhumiwa huyo akitokea rumande, Mwendesha mashtaka kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka Zanzibar Said Ali Said, alimueleza  Jaji wa mahakama kuu Zanzibar kuwa, kesi iyo ipo kwa ajili ya kuanza kusikilizwa   maelezo ya awali, lakini   bado upelelezi wa shauri hilo haujakamilika. “Mheshimiwa Jaji leo, kesi hii ipo kwa ajili ya kusikilizwa, lakini bado hatujakamilisha   upelelezi wa kesi na mashahidi, hivyo tunaomba utupangie tarehe nyingine, kwa ajili ya kusikilizwa,’’ alidai.   Baada ya maelezo hayo, Jaji wa mahakama kuu Zanzibar   Ali Mohamed Ali,   aliwauliza mawakili wa upande wa utetezi uliokuwa ukiongozwa na Ali Rashid Ali n

'TUSHIRIKIANE KUDHIBITI UHALIFU': INSPEKTA KHALFAN

NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ MKAGUZI wa shehia ya Mlindo Wilaya ya Wete, Inspekta wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Khalfan Ali Ussi amewataka wanajamii kushirikiana pamoja katika kuhakikisha wanapambana na wizi wa mifugo pamoja na mazao. Aliyasema hayo wakati wa kampeni ya nyumba kwa nyumba kutoa elimu ya kupambana na matendo ya kihalifu katika jamii, kupitia mradi wa 'familia yangu haina uhalifu' ambao husikiliza changamoto za wananchi na kutafuta mbinu mbadala ya kuzitatua. Alisema kuwa, iwapo wanajamii watashirikiana katika kukomesha vitendo vya kihalifu, watafanikiwa kudhibiti wizi wa mazao na mifugo ambao kwa sasa umeshamiri katika shehia hiyo, hali ambayo inarudisha nyuma juhudi za wananchi ambao wanapambana na hali duni ya maisha. "Lengo la ziara yetu hii ni kuendeleza kufanyia kazi miradi ya Polisi jamii, kusikiliza kero za wananchi na kizitafutia ufumbuzi," alisema Mkaguzi huyo. Alifahamisha kuwa, anaamini kwamba kampeni hiyo ya nyumba kwa nyumba itale

DK.MWINYI: 'SERIKALI ZINATAMBUA, KULINDA MCHANGO WA WANAWAKE'

  Serikali zote mbili zinatambua umuhimu na mchango mkubwa unaotolewa na wanawake hapa nchini na zimekuwa zikichukua hatua mbali mbali za kumlinda na kuwawezesha katika hatua za kimaendeleo.   Hayo yamesemwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar. HEMED SULEIMAN ABDULLA katika Kongamano la Uwezeshaji wanawake Kiuchumi Zanzibar linaloenda sambamba Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililofanyika katika Ukumbi wa Hotel ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar leo.   Amesema kuwa   kwa kutambua mchango wa wanawake nchini serikali imeongeza nafasi za wanawake katika vyombo vya maamuzi kutokana na marekebisho ya katiba ya mwaka 2010 kwa kuongeza asilimia ya viti maalum vya wanawake katika Baraza la Wawakilishi kutoka asilimia 30 hadi asilimia 40.   Rais Dkt. Mwinyi amesema kuwa Serikali kupitia Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi imetoa mafunzo mbal

INSPEKTA KHALFAN: ATOA SOMO KUWAPATA VIJANA WENYE MAADILI

  N A ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ VIJANA wa shehia ya Pandani Wilaya ya Wete Pemba,  wametakiwa kuendelea kushikamana pamoja na kuwasimamia vijana wadogo, ili wakue katika maadili mema, hali itakayosaidia kujenga jamii yenye heshima.   Akizungumza Machi 12, 2024 mara baada ya kukabidhi mipira ya kufanyia mazoezi kwa vijana wa vijiji vya Masipa, Kijuki na Kidutani, Inspekta wa Jeshi la Polisi na Mkaguzi wa shehia ya Pandani Khalfan Ali Ussi alisema, ili kujenga jamii iliyobora ni lazima vijana wafuate maadili mema na kuacha kufanya mambo yasiyofaa.  Alisema kuwa, ushirikiano na mshikamano ni muhimu katika kuelekezana kufuata maadili mema, hivyo ni vyema kuendeleza ili  kujenga jamii iliyobora na yenye heshima.  "Nawapongeza sana kwa juhudi mnayoichukua kuhakikisha vijiji hivi vinakuwa salama na kuwataka waendelee, kwani jukumu la ulinzi wa mali zao ni la kila mwanajamii," alisema Inspekta huyo.  Inspekta huyo aliwaasa vijana hao kuacha muhali kwa vijana wanaojihusisha na matendo ma

MRADI WA VIUNGO ZANZIBAR WAONYESHA NJIA WANAWAKE, VIJANA

  Na Nafda Hindi, Zanzibar@@@@ Ikiwa   dunia inaadhimisha siku ya wanawake, ambayo husherehekewa kila mwaka ifikapo tarehe 08 March yenye mnasaba ya kuonesha mafanikio ya kijamii, kiuchumi, kiutamaduni na kisiasa huku ikitetea usawa wa kijinsia. Katika siku hii ya wanawake, ikiwa na kauli mbiu ya mwaka huu “Wekeza kwa wanawake, harakisha maendeleo”.   Kwa muktadha huo ikiwa na maana pana kuwekeza nguvu kwa mwanamke kunaharakisha maendeleo kwa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa Ujumla, na kwa kukazia kauli hiyo, hata Viongozi wa dini ya Kiislam katika hadithi za Mtume Muhammad (S W) inasema “Ukifundisha mwanamke mmoja ni sawa na kufundisha wanawake kumi. Kufuatia siku hii hiyo adhimu kwa wanawake TAMWA, ZANZIBAR hawako nyuma katika kuhakikisha wanatumia nafasi hiyo ili kumkombowa mwanamke kiuchumi kwa kuwa na uwezo wa kujitegemea na kutunza familia. Kupitia MRADI wa VIUNGO wenye lengo la kuwainuwa wanawake kiuchumi TAMWA, ZANZIBAR walifanya ziara ya siku moja kutembelea wanufaik

WALIOEKEZA SHILINGI 55,000 MISOONI UPANDAJI MIGOMBA KUCHEKELEA MAVUNO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ USHIRIKA wa ‘tudumishe maendeleo’ uliopo Misooni shehia ya Shungi wilaya ya Chake chake, umesema kama migomba yao 50 walioipanda mwaka jana, itazaa kwa pamoja, watajipatia faida ya shilingi 195,000. Kwani ushirika huo umetumia shilingi 25,000 kwa ununuzi wa miche 50 ya migomba aina ya mkono wa tembo, mtwike, kipukusa kwa wastani wa shilingi 500 kila mche mmoja na shilingi 30,000 kwa kulimishia shamba loa kwa hatua ya awali. Mwenyekiti wa ushirika huo Mbarouk Idrissa Omar, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi kijijini hapo alisema, waliamua kujikusanya pamoja na kuendesha kilimo hico, ikiwa ni njia moja yapo ya kujikwamua na umaskini. Alisema, walichagua kilimo cha migomba, kutokana na eneo walilo linakukubali vyema hasa kwa aina ya ardhi yao ilivyo, kilimo hicho ndio kilichoonekana kunawiri vyema, ilikinganishwa na mazao mingine. Alieleza kuwa, matumiani yao ni kuwa, kama migomba hiyo 50 walioipanda mwezi Januari mwaka jana, na kuzaa kw

DC. MKOANI: SMZ ITAENDELEA KUYAPA HAKI MAKUNDI YOTE BILA YA UBAGUZI

  NA ASHA ABDALLA, PEMBA @@@@ SERIKALI ya Mapindunduzi ya Zanzibar ya awamu ya nane chini ya uongozi wa Dk.Hussein Ali Mwinyi, inaendelea kufanya harakati kwa makundi mbalimbali katika kuhakikisha kila mzanzibar anapata haki zote za msingi bila ubaguzi wa rangi, silka na  itikadi  yake . Ameyasema hayo Mkuu wa wilaya ya Mkowni Khatibu Juma Mjaja kwaniaba ya  Mkuu wa Mkowa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Masoud, wakati alipokua akigawa vifaa maalumu vya  watu wenye uUlemavu wa ngozi  kutoka katika mradi wa ZAHO  huko ukumbi wa Manis[paa ya Mji Chake chake Pemba Machi 9, 2024. Amesema kuwa serekali inaweza kuwawezesha zaidi watu wenyeulimavu wa ngozi kwa miundombinu mbalimbali kwakupatiwa elimu ,afya bora na hata kupatiwa  mikopo ambayo  itaweza kuwasaidia katika kufanya biashara ndogondogo nakuweza kujikwamua kimaisha. "Niwaleze wazazi  nawelezi kua nikosa kisheria kuwaficha watu wenye ulemavu au kumdalilisha kwani nawao ni watu kama  watu wengine duniani."alifafanua  Hata hivyo

''ITUMIENI MIKOPO KUENDELEZA BAISHARA ZENU': MKURUGENZI BADRU

Mkurugenzi Idara ya Jinsia kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Makundi Maalumu (SMT) ndugu Badru Abduln uru amewataka wajasiriamali wanawake kutumia vyema fursa ya mikopo ili kuendelea biashara zao. Akizungumza wakati alipofungua mafunzo kwa wajasiriamali hao juu ya namna ya kuomba mikopo isiyo na riba katika B enki ya CRDB, yaliyofanyika jana katika ukumnbi wa Sebleni kwa wazee ikiwa ni shamrashamra za kuadhimisha siku ya wanawake duniani,   ndugu badru amesema kufanya hivyo kutawasaidia kuweza kujikwamua na utegemezi. Amewataka wanawake hao kutambua kuwa katika mikopo hio ya CRDB S erikali nayo imechangia kwa kiasi kikubwa ili kuwasaidia wanawake kuwainua kiuchumi. Pia amewataka kuwa na nidhamu ya fedha wanazikopa kwa kufanya jambo walilolikusudia ili waweze kurejesha mikopo hiyo na kuwasaidia wengine. Aidha amewashauri kuyatumia majukwaa ya uwezeshaji kiuchumi ili kuweza kuwak ut anisha na wajasiriamali wengine Pamoja na kutanua wigo wa kibishara. Wakati huo huo

WAZIRI PEMBE ATAJA FAIDA YA UCHUNGUUZI WA AFYA KWA MAMA, MTOTO

  Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe.Riziki Pembe Juma amesema upimaji wa  afya  ni muhimu sana kwa wanamke na mtoto , kwani uchunguzi husaidia kutathmini hali ya afya na kusaidia kutambua matatizo yoyote yanayoweza kutokea. Pia a mesema hatua hiyo itawasaidia katika kuwakinga watoto na vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia. Mhe Riziki ameyasema hayo kwa niaba ya Mwenyekiti wa Taasisi ya Maisha bora Foundation mama Maryam Mwinyi, katika kampeni ya Afya bora maisha bora iliyofan y ika katika viwanja vya Kivunge Wilaya ya Kaskazini A Unguja. Amesema Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto imefanikiwa kuweka namba ya simu  inayotambulika 116 kwa kupiga bure, ikiwa lengo ni kutoa taarifa masuala yote ya udhalilishaji na kuweza kufuatiliwa na kuchukuliwa hatua.   A me toa wito kwa   wazazi na walezi kuwasaidia watoto wanapowapatia taarifa za vitendo hivyo, huku akiw a sihi kurejesha malezi ya pamoja ili kuwakinga watoto juu ya vitendo hivyo. Aidha