Skip to main content

Posts

Showing posts from October 9, 2022

UN WAGUSWA UTENDAJI KAZI TAMWA-ZANZIBAR

  Na Muhammed Khamis,TAMWA-ZNZ   Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya Wanawake (UN Women) Bi. Sima Sami Bahous amesema kazi inayofanywa na  Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA-ZNZ) kuhamasisha wanawake wengi zaidi kushiriki kwenye nafasi za uongozi ni ya kupongezwa na kuthaminiwa na kila mmoja kwa lengo la kufikia usawa wa kijinsia baina ya wanaume na wanawake.    Bi Sima, ameyasaema hayo katika ofisi za TAMWA-ZNZ zilizopo Tunguu Wilaya ya kati Unguja aipofanya ziara maalumu kuzungumza na uongozi wa chama hicho pamoja na baadhi ya wawakilishi wa asasi za kiraia,viongozi wa dini na wawakilishi wa vyama vya siasa kufuatia utekelezaji mradi wa wanawake na uongozi.    Amesema amefurahishwa na mbinu mbalimbali zilizotumiwa na TAMWA-ZNZ katika kutekeleza mradi huo kwa kushirikisha makundi mbalimbali yaliyopo katika jamii ikiwemo viongozi wa dini ambao wamefafanua misingi ya di

MWALIMU SKULI YA MADUNGU KUSUKA AU KUNYOA LEO MAHKAMANI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: MWALIMU wa skuli ya Madungu msingi Ali Makame Khatib miaka 25, anayetuhumiwa kumbaka mwanafunzi wake, mwenye miaka 11, leo Oktoba 17 mwaka huu, anatarajiwa kuanza kujitetea, katika mahkama ya makosa ya udhalilishi mkoa wa kusini Pemba.   Mtuhmiwa huyo anayesimamiwa na wakili wake Suleiman Omar Suleiman, Oktoba 12, mwaka huu waliiahidi mahkama hiyo kuwa, leo Oktoba 17, watawasilisha mashahidi wanne mahakamani hapo.   Walidai kuwa, mashahidi hao wanne wanakuja kupinga juu ya tuhma zinazomkabili, ambazo walidai kuwa hazina mashiko na nizakupangwa, ili kumchafulia jina lake.   ‘’Mheshimiwa hakimu baada ya kushauriana na mteja wangu, tumeamua kuwa leo hii, tutawasilisha mashahidi wanne, ambao watawasilisha ushahidi wao, na kisha kuiachia mahakama iendelee na utaratibu mwengine,’’alidai wakili huyo.   Upande huo wa utetezi, uliamua kuwa leo hii, watajitetea kwa mtuhumiwa na mashahidi wao kwa njia ya kiapo, ili ushahidi wao uweze kukidhi viwango vi

NAIBU WAZIRI NISHATI AWAAHIDI JAMBO WANANCHI KIBOJE

NA SALMA LUSANGI,   NAIBU waziri wa Maji, Nishati na Madini, Shabaan Ali Othman amewaahidi  wakaazi wa eneo la Kinooni, Shehia ya Kiboje, Unguja kuwa ndani ya wiki moja Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) litafikisha umeme katika eneo hilo ili waondokane na  gharama za kupandisha maji kwa kutumia umeme wa jenereta. Kauli hiyo ameitoa alipofanya ziara ya  kikazi katika jimbo la Uzini, Unguja  kufuatia malalamiko ya Mwakilishi wa jimbo hilo kwamba waakazi wa eneo hilo hawana huduma ya umeme  wala maji safi na salama. Shabaani alisema atahakikisha kuanzi tarehe 13 hadi tarehe 19, mwezi huu umeme utafikishwa katika maeneo hayo ili waakaazi wa eneo hilo waandokane na gharama za kutia mafuta kwenye jenereta kwa ajili ya kupandisha maji kutoka kwenye kisima hadi  tangi la maji la juu. Alisema wizara yake kupitia ZECO inatoa nguzo za umeme bure ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi hivyo atahakikisha Shirika hilo linafikisha

''MWALIMU SKULI YA MADUNGU ANA KESI YA KUJIBU'' MAHKAMA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::  M AHKAMA ya maalum ya makosa ya udhalilishaji ya mkoa wa kusini Pemba, iliyopo Chake chake imesema, mwalimu wa skuli ya Madungu msingi Ali Makame Khatib miaka 25, anayetuhumiwa kumbaka mwanafunzi wake, anayo kesi ya kujibu juu ya tuhma hizo.   Hakimu wa mahakama hiyo Muumin Ali Juma, alisema kilichobakia mbele yamtuhmiwa huyo, ni kujitayarisha kwa ajili ya kujitetea, hasa baada ya upande wa mashtaka, kufunga ushahidi wake.   Aliyasema hayo Oktoba 12, mwaka huu wakati mtuhumiwa huyo anayewakilishwa na mawakili wawili, juu ya tuhma za kumbaka mtoto wa miaka 11, akiwa juu ya kizimba cha mahkama hiyo.   Hakimu huyo, aliuuliza upande wa utetezi, juu njia watakayoitumia kufanya utetezi, ikiwa ni ya kiapo ama bila ya kiapo, ambapo ukaeleza utatumia njia ya kiapo siku hiyo.   ‘’Upande wa mashataka tokea Oktoba 11, mwaka huu ulishafunga ushahidi wake, baada ya kumskiliza shahidi wake wa mwisho, askari mpelelezi, hivyo mahkama imeona mtuhumiwa anayo