Skip to main content

Posts

Showing posts from April 17, 2022

KAMATI MTEGA WAWI YATOA ONYO LA MWISHO WACHIMBA MCHANGA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMATI ya Maendeleo ya kijiji cha Mtega shehia ya Wawi wilaya ya Chake Chake, imeahidi kuwachukulia hatua za kisheria, wananchi wote wenye tabia ya kuchimba mchanga kwenye barabara yao, iliyoingia kijijini kwao. Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa kamati hiyo Khamis Haji, alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, juu ya tabia iliyojitokeza ya uchimbaji mchanga na kusababisha mashimo kwenye barabara hiyo. Alisema, waligundua hilo baada ya kuitembelea barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 2.5, ambapo alisema waligundua mashimo yenye kina kirefu, ambayo yanaweza kuhatarisha uimara na uendelevu wa barabara hiyo. Mwenyekiti huyo alisema, lazima wawachukuliwe hatua za sheria, ambao watawakamata wakiichimba barabara hiyo kwa kuchukua mchanga, kwa ajili ya ujenzi. “Baada ya hivi karibuni kuitembelea barabara hii nikiwa na wajumbe wa kamati hii, tulikuta vishungu vya mchanga pembezoni mwa barabara yetu, na kwamba wapo wanaoichimba kwa maslahi yao,’’a

WATU WENYE ULEMAVU PEMBA WATOA NENO UKODISHWAJI VISIWA ZANZIBAR

IMEANDIKWA   NA HAJI NASSOR, PEMBA WATU wenye ulamavu kisiwani Pemba, wamepongeza hatua ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kutaka kuvikodisha visiwa vinane vidogo vidogo, kwa dola za Marekani milioni 271.5 wastani wa shilingi bilioni 600.357. Wamesema hatua hiyo inaonesha, nia ya dhati ya serikali ya kutaka kuwainua wananchi kiuchumi, jambo ambalo walisema ni vyema nao, wakaangaliwa kunufaika na uwekezaji huo. Walieleza kuwa, hatua hiyo ya serikali inayoongozwa na Dk. Mwinyi, wameifurahia mno, na sasa kilichobakia kwa watendaji sekta ya utalii, kuweka mazingira rafik kwa ajili yao. Wakizungumza na mwandishi wa habari, kufuatia kusambaa kwa taarifa ya uwekezaji ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar ‘ZIPA’ Sharif Ali Sharif, walisema hofu yao, ni kusahauliwa katika uwekezaji huo. Mmoja kati ya hao Hidaya Mjaka Ali, alisema uwekezaji huo ikiwa watashirikishwa kikamilifu, unaweza kuwa na maana pana kwao, ikiwa ni pamoja na ajira za kudumu. “Sisi watu wenye ulemavu mara z

Bobay’ kipimo cha kisayansi cha uzalishaji chumvi -Ukikikosea chumvi hugeuka sumu kali

  NA HAJI NASSOR, PEMBA “MAJI ya chumvi yakitoka baharini, huwa na ujoto sifuri au kisaynasi inaitwa ‘ zero Bobay’, hapo sasa lazima kuyaingiza kwenye bwawa ‘reserve’ ili kuyavumbika,’’ Ndivyo alivyoanza mtaalamu na mkulima wa bidhaa ya chumvi ya mawe, Bakari Shaaban Bakari aliyeko bahari ya mjini Kiungoni Wete Pemba, wakati akizungumza na mwandishi wa makala haya.   CHUMVI NI NINI? Chumvi  kwa maana ya  kemia  ni  kampaundi  inayofanywa na ‘ ion ’ yaani  anioni  yenye  chaji hasi  na ‘ Calcium  yenye  chaji chanya  baada ya  bezi  kuunganika na aside au metali yoyote. Lakini, kuna aina nyingi za chumvi kutokana na  elementi  mbalimbali na hizi kwa jumla haziwezi kuliwa, na bindamu, kwa mfano chumvi ya aside, chumvi ya muungano . Kwa bahati mbaya, chumvi inayotumiwa na watu wengi haina madini ya kutosha ya sodium na chloride kutokana na kutengenezwa upya viwandani kwa kusafishwa (refined ).   Utumiaji wa chumvi sahihi na kwa kiwango kinachotakiwa, una faida nyingi m

DUNIA ILIANZIA HAPA NA SASA IKO HAPA KUPIGANIA HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU

  IMEANDIKWA NA HAJI NASSOR, PEMBA KWA miaka mingi, suala la haki za watu wenye ulemavu halikuwa likoenekana na umuhimu wake, kuanzia hapa Zanzibar na duniani kote. Dunia wakati inasonga mbele, hadi kufikia miaka ya 80, ambapo Umoja wa Mataifa UN, jumuiya za watu wenye ulemavu zilianza kutetea upatikanaji wa haki za binadamu kwa watu wenye ulemavu. Suala ka kutetea haki za watu wenye ulemavu, lilijotokeza hata kwenye vita vya kwanza vya duniani vya mwaka 1914 na vile vya pili vya mwaka 1918, baada ya kujitokeza kwa majeruhi kadhaa. Mitandao ya kijamii inahabarisha kuwa, kwa wakati huo waliotetea na kupata haki zao za matibabu na huduma nyingine ni wale, waliopkumbwa na madhila kwenye vita hivyo pekee. Katika eneo jengine mwaka 2006, Umoja wa Mataifa ulianzisha mkataba wa kimataifa kuhusu haki za watu wenye ulemavu (UN -Convention on the Rights of Persons with Disabilities- UNCRPD). Shabaha kubwa ya mkataba huo ilikuwa ni kulinda na kuboresha hali ya watu wenye walemavu d