Skip to main content

Posts

Showing posts from February 19, 2023

DK. MWINYI LEO KUKABIDHI TUNZO WASHINDI WAANDISHI WA HABARI ZA WANAWAKE ZANZIBAR

  TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Washindi wa tunzo za umahiri wa uandishi wa habari wa takwimu za wanawake na uongozi kujulikana  leo usiku wa  25 Febuari, 2023. Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA, ZNZ), kwa kushirikiana na Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) na Jumuiya ya Mazingira, Jinsia na Utetezi Pemba (PEGAO) leo  Jumamosi tarehe 25 Febuari, 2023 zimeandaa hafla          ya utoaji tunzo maalum za umahiri wa uandishi wa habari za takwimu zinazohusu masuala ya wanawake na uongozi Zanzibar ambayo itafanyika katika ukumbi wa Sheikh Idriss Abdul Wakil  – Kikwajuni kuanzia saa 1: 00 usiku.   Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Hussein Ali Mwinyi katika hafla hiyo ambayo inategemewa kuhusisha zaidi ya watu 150.   Kauli mbiu ya tunzo hizo ni “KALAMU YANGU MCHANGO WANGU KWA WANAWAKE” na ina lengo la

WADAU, WAANDISHI, WAMILIKI WATAJA SABABU KUTAKA SHERIA MPYA YA HABARI ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: KWA zaidi ya miaka 10 sasa wadau wa habari wamekuwa wakipaza sauti zao kutaka sheria mpya na bora ya habari Zanzibar. Wadau mfano Baraza la Habari, TAMWA-Zanzibar na hata Shirika la Internews Tanzania ofisi ya Zanzibar wamekuwa wakiungana na waandishi kuhakikisha sheria moja ya habari inapatikana. Mratibu wa Internews ofisi ya Zanzinar Zaina Mzee, anasema moja ya sababu ya kutaka sheria mpya ya habari Zanzibar, ni kuona zile mbili zilizopo zinafutwa. ‘’Ipo sheria ya Tume ya Utangaazaji Zanzibar nambari 7 ya mwaka 1997, pamoja na marekebisho yake, pamoja na ile ya s heria nambari 5 ya Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu ya mwaka 1988, ambayo imefanyiwa marekebisho mwaka 1997.   Anasema sheria hizo, zimekuwa na vifungu ambavyo sio rafiki kwa kuimarisha uhuru wa habari pamoja na uhuru wa kujieleza katika jamii.   Anaeleza kuwa, pamoja na ukongwe wake sheria hizo mbili kuu zinazosimamia vyombo vya habari, lakini kubwa zimekuwa zikiwabana waandish

JINSI VIFUNGU VYA SHERIA YA MAGAZETI ZANZIBAR VINAVYOUWEKA CHINI YA ULINZI UHURU WA HABARI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA:::   SHERIA nambari 5 ya Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu ya mwaka 1988, ambayo imefanyiwa marekebisho mwaka 1997, inavyo vifungu 81, vilivyobebwa na sehemu 1O.   Pamoja na marekebisho hayo yaliyofanywa miaka 9, baada ya sheria hiyo kupita na sasa ikielekea kuwa na umri wa miaka 21, lakini bado kuna vifungu vinatajwa kuuweka chini ya ulinzi uhuru wa habari Zanzibar.   Ndivyo ilivyo kuwa sheria hiyo, kwa wakati huo na miaka hiyo ilitungwa na kisha kusainiwa na rasi wa wakati huo wa Zanzibar kwa nia nzuri, ingawa kwa sasa uzuri huo haupo tena. WADAU WATAKA SHERIA MPYA Ndio maana, kwa mfano Shirika la Internews Tanzania kwa kushirikiana kwa karibu na TAMWA-Zanzibar na wakati mkubwa na Baraza la Habari Tanzania MCT, wamekuwa wakita sheria bora na fariki Zanzibar.   Kwani Mratibu wa Internews Tanzania ofisi ya Zanzibar, Zaina Mzee, anasema sheria hiyo kwa sasa, inakinzana pakubwa na dhana ya demokrasia na utawala bora unaochapuzwa na uh

SIKU 180, ZABEBA MATUKIO 610 YA UDHALILISHAJI ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: MATUKIO 610 ya ukatili na udhalilishaji kwa wanawake na watoto, yameripotiwa kutokea  Zanzibar, kwa kipindi cha miezi mitatu mitatu ya mwaka 2021 na 2022, taarifa za ofisi ya   Mtakwimu Mkuu wa serikali Zanzibar, zinaeleza. Kwa miezi ya Januari hadi Machi mwaka 2021, Ofisi hiyo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Zanzibar, ilikusanya matukio 363, ingawa kwa mwaka jana, katika kipindi hicho matukio hayo yaliripotiwa 247, upunguzu wa matukio 116. Takwimu hizo zinafafanua kuwa, kwa mwaka 2021 kwa miezi mitatu ya mwanzo, mwezi ulioongoza ni mwezi wa Machi ulioripoti matukio 141, ukifuatiwa na mwezi wa Januari matukio 122 na Febuari matukio 100. Kwa mwaka 2022, mwezi uliokihiri kwa matukio mengi ni mwezi Febuari, ulioripoti matukio 100, huku mwezi Machi ukiripoti matukio 82, wakati mwezi wa Januari yakishuka kwa 17, na kuripoti matukio 65 pekee. Taarifa hiyo ikeleza kuwa, mwezi wa Febuari kwa miaka yote miwili, iliripoti matukio sawa ya 100 kwa wanawake

SHERIA YA TUME YA UTANGAAZAJI ILIVYOBEBA MANENO YENYE UKAKASI KWA UHURU WA HABARI ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: ZANZIBAR kama ilivyo eneo jingine lolote ulimwenguni, nayo inavyo vyombo vya habari, ambavyo maudhui yake ni sawa na vile vya mataifa mengine. Nikukumbushe tu kuwa, kazi za msingi za vyombo vya habari ni kuelemisha, kuburudisha na kuhabarisha ingawa kwa pia ni kukosoa, kupongeza na kuhoji. Kazi hii hasa ni haki ya kikatiba, katika mataifa mbali mbali, kwa mfano Zanzibar katiba yake ya mwaka 1984 kifungu cha 18 na ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ibara 18 imeelezea haki hii. Kama hivyo ndivyo, unaweza kushangaa kuwa suala la kutoa, kupata na kusambaaza habari ni haki ya kikatiba, sasa iweje kutungwe sheria yenye vifungu au maneno, yenye ukakasi kwa waandishi wa habari. SHERIA YA TUME YA UTANGAAZAJI ZANZIBAR NO 7 YA MWAKA 1997 Sheria hii ambayo sasa inatimiza umri wa miaka 26, tokea pele ilipotiwa saini na Rais wa wakati huo wa Zanzibar Dk. Salmin Amour Juma, licha ya kufanyiwamarekebisho. Kwa hakika, lengo kuu la sheria hii,