Skip to main content

Posts

Showing posts from September 14, 2025

Dk. SAMIA AAHIDI MAKUBWA BANDARI YA WETE, UWANJA WA NDEGE PEMBA UMO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MGOMBEA Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi ‘CCM’ Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema kama atapata ridhaa ya kutetea nafasi hiyo, ataijenga bandari ya Wete ili, iwe ya kisasa. Mgombea huyo wa Urais, aliyasema hayo jana, uwanja wa Gomabani ya kale, wilaya ya Chake chake Pemba, kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni, kuelekea uchaguzi mkuu mwezi Oktoba, mwaka huu. Alisema, ili kuifungua Pemba hakuna budi suala la miundombinu ya bandari, ni lazim kupanuliwa, ili kurahisisha usafirishaji wa wananchi na mizigo yao. Alisema, tayari fedha zake zipo, ambazo ni mkopo kutoka Korea, na anachosubiri ni kupata tena ridhaa ya wananchi ifikapo Oktoba 29, mwaka huu, aanze kazi. ‘’Niwahakikishie kuwa, mini na Dk. Mwinyi kama mtatupa ridhaa, basi moja ya eneo ambalo kwa Pemba, tutaliangalia, ni ujenzi wa bandari ya kisasa ya Wete,’’alisema. Ahadi nyingine, ambayo Mgombea huyo wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. S...

NRA KUWALIPA WAALIMU MSHARAHA SHILINGI MILIONI 1.5 IKIINGIA IKULU

  NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ MGOMBEA Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha NRA, Khamis Faki Mgau amesema, pindi akipata ridhaa ya kuongoza nchi, atahakikisha kila mwalimu wa skuli ngazi ya cheti, atamlipa mshahara wa shilingi 1.5. Ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara, akifungua kampeni kwa chama hicho, uliofanyika Kangagani wilaya ya Wete Pemba. Alisema kuwa kila mwalimu wa skuli kwa ngazi ya cheti, atamlipa kima hicho, ingawa wale wenye elimu ya juu watavuuka kima hicho.   "Walimu wa skuli wamekuwa wakifanya kazi kubwa ya kuwafundisha watoto wetu, ingawa wamekuwa wakipokea mishahara midogo, nikiiingia madarakani, nitarekebisha fedha za wafanyakazi hao,"alifafanua. Ahadi nyingine Mgombea huyo aliotoa ni kuweka mazingira laini, ili kila mmoja aliyefikia uamuzi wa kufunga ndoa, iwe rahisi. Alisema kuwa ifikapo mwisho wa mwezi kila kijana anahakikisha kumlipa shilingi laki 900,000, ili kumuwezesha kumudu mke ...

OTHMAN ATAJA MAMBO MANNE YA KUIFUNGUA PEMBA KIUCHUMI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MGOMBEA urais wa Zanzibar kwa tiketi ya ACT- Wazalendo Othman Massoud Othman, amesema kama akipata ridhaa ya kuingoza Zanzibar, atasimamisha utawala wa sheria na haki, ikiwa ni njia moja wapo ya kukuza uchumi. Alisema, haiwezekani wananchi kupata maendeleo endelevu, kama hakuna utawala wa sheria, ambao utawahakikishia wananchi kubaki na mali zao ikiwemo ardhi. Mgombea huyo wa urais wa aliyasema hayo jana Septemba 18, 2025, uwanja wa mpira wa Mpika tango Mkoani, wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa chama hicho, wa kampeni. Alisema, utawala huo wa sheria, utakuwa na mambo kadhaa, ikiwemo kila mmoja kupata heshima ya kufanya shughuli zake, kwa mujibu wa sheria. Alieleza kuwa, kufanya hivyo ni kuifungua Zanzibar kiuchumi, kutokana na watu kuheshimiana na kutunza amani na utulivu miongoni mwao. ‘’Kama nikiingia mdarakani, nitahakikisha, kwanza tunakuwa na utawala wa kuheshimiana, ambao ndani yake utamuhakikishia kila mmoja ma...

ADA-TADEA: YAAHIDI KUWAANZISHIA MFUKO WA MASOMO VIJANA

NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ MGOMBEA urais wa Zanziba kwa tiketi ya Chama ADA-TEDEA Juma Ali Khatib, amesema pindi wazanzibari wakimpa ridhaa ya kuwa Rais, atahakikisha anaanzisha mfuko maalumu utakaowsaadia, kuwawezesha vijana kusoma bila ya malipo. Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni, kwa chama hicho, uliofanyika Kangagani wilaya ya Wete Pemba. Alisema kuwa makundi hayo watayazingatia sana kwa sababu ni watu muhimu kutokana na uhitaji wao wa kimaisha, huku akiamini elimu ndio mwarubaini wa changamoto zao.   Alisema, mfuko huo hautokuwa na ubaguzi, na kubwa zaidi ni kuwapatia vijana gharama za masomo, ili kuhakikisha wanafinikisha ndoto zao.   Mgombea huyo alisema, inaonekana vijana waliowengi wanahamu wa kujiendeleza kielimu, ingawa changamoto ni kukosa mfuko wao maalum. ‘’Niwahakikishie vijana, pindi nikipata ridhaa ya kuwa rais wan chi hii, moja ya kipaumbele ni kuanzisha mfuko ambao utawasaidia vijana kielimu,’’alifa...

WANANCHI CHAKE CHAKE WAUMISHA VICHWA AJALI ZA BODA BODA

  NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ WANANCHI wa kijiji cha Ole Kianga wilaya ya Chake chake, wamesema ajali nyingi za barabarani zinasababishwa na waendeshaji wa  bodaboda kutokana na utumiaji mbaya wa  barabara wanapokuwa kwenye shughuli zao. Wameyasema hayo leo Septemba 19, 2025 walipokuwa wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, juu ya uwepo wa ajali nyingi zikisababishwa na waendeshaji wa bodaboda.   Wakieleza kuwa ajali hizo kwa sasa zimekuwa tishio na kuwaweka roho juu, wanaotumia usafiri wa bodaboda kupitia vyombo hivyo.   Mpanda bodaboda Aisha Ali Abdullah alisema ni usafiri unaorahisha kwa sasa, ingawa wamekuwa hawana amani, kutokana na waendeshaji kukosa umakini. Alisema kuwa ndani ya barabara kumekuwa na vyombo vya usafiri kila aina, ingawa kwa upande wa pikipiki aina ya bodaboda, zimekuwa zikihatarisha usalama wao. Alifafanua kuwa waendeshaji bodaboda hao, weingi wao wamekuwa ndio chanzo kikubwa cha kusababisha ajali barabarani, kwani wamek...

ZNCC: YAWAKUMBUSHA WAJASIRIAMALI KUZISAJILI BIDHAA ZAO

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAJASIRIAMALI kisiwani Pemba, ambao bado hawajazisajili biashara zao, wame kumbwa kufanya hivyo haraka, ili wawe na sifa wakati wanapoomba misaada ama kuingia, katika mashindani mbali mbali. Ushauri huo umetolewa leo Septemba 18, 2025 na Mkurugenzi mtendaji wa Jumuiya ya kitaifa ya wafanyabishara Zanzibar ‘ZNCC’ Hamad Hamad, alipokuwa akizungumza na wajasiriamali hao, wakati akiyafungua mafunzo, ya umuhimu wa usajili wa majina ya biashara na bidhaa zao, yaliyofanyika ukumbi wa Manispaa Chake chake. Alisema, njia moja kwa wajasiriamali hao kufikia ndoto zao, suala la kusajili bidhaa zao na majina ya biashara, haliepukiki, ikiwa wana malengo ya kufika mbali. Alisema, unapoisajili biashara na jina la biashara, huwa ni kuilinda na kujihakikishia kuipandisha hadhi, kama zilivyo kwa biashara nyingine za makampuni. ‘’Niwatake haraka sana, ambao hawajajisajili ‘BPRA’ kufanya hivyo, maana kinyume chake, jina la bidhaa zako ambazo zimeshakuwa maarufu ...

ACT- WAZALENDO KULIIMARISHA ZAO LA KARAFUU IKIINGIA IKILU

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT- Wazalendo, Othman Masoud Othman amesema, atahakikisha wananchi wa Pemba, wananufaika moja kwa moja na rasilimali ya zao la karafuu ambalo ni uti wa mgongo wa uchumi wa Zanzibar. Akiwahutubia wananchi kwenye viwanja vya Mchangamdogo Kambini Jimbo la Kojani, Mkoa wa Kaskazini Pemba Othman alisema, pamoja na karafuu kuwa ni zao la kimkakati, na lenye thamani kubwa duniani, bado linahitaji kufufuliwa ili kuleta tija zaidi kwa wananchi wa Zanzibar. Alisema kuwa, Zanzibar ina uwezo wa kuzalisha zaidi zao la karafuu, ili liendelee kuwa ni mwega wa uchumi wa nchi, hivyo atakapopewa ridhaa ya kuiongoza nchi,  atalifufua zao hilo pamoja na mazao mIngine ya viungo kwa ajili ya kuiinua Zanzibar kiuchumi. "Nitatafuta wawekezaji watakaokuja kununua karafuu hapa, hivyo zao hilo litaongezeka thamani na wananchi wataongeza vipato vyao," alisema mgombea huyo. Aidha alieleza kuwa, wamejipanga kuwawezesha wavuvi ili wao...

ADC YAAHIDI KUWALIPA MISHAHARA WAALIMU WA MADRASSA ZANZIBAR

  NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ MGOMBEA urais wa Zanzibar wa tiketi ya chama cha Alliance for Democtratic Change ‘ADC’ Hamad Rashid Mohamed, amsesema moja ya kipaumbele chake, kama atapata ridhaa ya kuwa Rais wa Zanzibar, atahakikisha walimu wa madrsa kuwalipa mishahara kama, walivyo wafanyakazi wingine. Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni za chama hicho, zilzofanyika uwanja wa Gombani kongwe Chake Chake Pemba. Alisema kuwa atahakikisha walimu wote wa madrassa, atawalipa mishahara kama wafanyakazi wingine, pamoja kuwapatia vifaa vya TEHAM. "Mukinipa ridhaa ya kuwa Rais wa Zanzibar, nitahakikisha walimu wote wa madrassa, nitawalipa mishahara kama wafanyakazi wengine wa utumishi wa umm," alisema. Aidha Mgombea huyo, alisema kama atapata ridhaa hiyo, ataimarisha kilimo cha mpunga, ili kuhakikisha hakuna mwananchi anayenunua mchele.   Alieleza, kwa ardhi ya Zanzibar ilivyo kubwa, na kwa uzoefu wake wakati alipokuwa Waziri wa Kilimo, ana ha...