Skip to main content

Posts

Showing posts from June 2, 2024

ANAYEDAIWA KUMUUA MKE WAKE KWA MAKSUDI AREJESHWA RUMANDE

    NA MARYAM NASSOR, ZANZIBAR@@@@ MTUHUMIWA    wa kesi ya mauwaji, Khalfan Ali Abdallah( 26) amepandishwa katika kizimba cha mahkama kuu Tunguu   Zanzibar ,kwa tuhuma za kuua kwa makusudi chanzo kikitajwa ni wivu wa mapenzi. Akisomewa shitaka lake hilo na Mwendesha mashtka kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka Zanzibar, Ali Amour Makame, mshitakiwa huyo alikana shitaka hilo.  Mara baada ya kufika mahakamani hapo, mtuhumiwa huyo akitokea rumande, Mwendesha mashtaka kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka Zanzibar Ali Amour Makame Alimueleza, Jaji wa mahakama kuu Zanzibar kuwa, kesi iyo ipo kwa ajili ya kuanza kutajwa maelezo ya awali, lakini bado upelelezi wa shauri hilo haujakamilika na kumpa muda mtuhumiwa kutafuta wakili wa kesi yake. “Mheshimiwa Jaji leo (jana), kesi hii ipo kwa ajili ya kutajwa, lakini tunaomba uihairishe na kuipanga tarehe nyengine, ili kumpa muda   mtuhumiwa kutafuta   au kutafutiwa wakili, kwa ajili ya kumsimamia kesi yake,” alidai. Baada ya maelezo

MASHEHA WESHA, WAWI: 'TUNAZO ARDHI TAYARI KWA UJENZI WA OFISI'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MASHEHA wa shehia za Wawi na Wesha wilaya ya Chake chake Pemba, wamesema tayari wameshapata maeneo, kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za masheha, kama agizo la serikali kuu, lilivyowataka kutafuta ardhi kwa kazi hiyo. Walisema, kwa sasa wanachosubiri ni serikali kuanza upelekaji vifaa kwa ajili ya ujenzi wa ofisi hizo, hasa baada ya maeneo hayo, kuyamiliki kisheria. Wakizungumza na mwandishi habari hizi Juni 8, 2024 kwa nyakati tofauti, walisema tayari maeneo hayo yameshapimwa na taasisi husika, na sasa yako tayari kwa ajili ya ujenzi wa ofisi hizo. Sheha wa shehia ya Wesha Haji Mohamed Ali, alisema eneo ambalo wameshakubaliana na wananchi kwamba lijengwe ofisi, ni milki ya serikali tokea asili. Alisema, eneo hilo kwa muda mrefu, wananchi waliamua kulihifadhi kwa upandaji wa miti mbali mbali, hivyo wakati wowote likitakiwa kutumika litasafishwa. ‘’Sisi wananchi wa shehia Wesha, eneo la kujenga ofisi kwa ajili ya sheha tunalo, kilichobakia tunaisubir

MDHAMINI FEDHA PEMBA: USIMAMIZI MALI ZA UMMA KUFIKIA MALENGO YA SERIKALI’

    NA HASINA KHAMIS, OUT- PEMBA@@@@ AFISA Mdhamini wa Wizara ya Fedha na Mipango Pemba Abdull-wahbi Said Abuu-bakar, amesema usimamizi bora wa mali za umma itasadia kwa serikali, kufikia malengo yaliyokusudia.   Aliyasema hayo leo Juni 6, 2024 katika kikao cha kupokea maoni ya wadau, kwa muongozo wa uondoaji wa mali za umma na usimamizi, udhibiti wa matumizi ya vyombo vya moto vya serikali, ukumbi wa wizara hiyo Gombani Chake chake Pemba.   Alisema changamoto zilizopo katika wizara, taasisi za umma na mashirika, ni kushidwa kusimamia kutunza na kutumia vyema mali za umma kama sheria inavyotaka.   "Hatufanyi vyema katika kusimamia mali za umma, ambapo inasababisha kushidwa kufikia lengo la mali hizo, jambo ambalo sio sahihi,’’alieleza Afisa Mdhamini huyo.   Aidha aliwataka washiriki hao kutoka mashirika ya umma na taasisi za serikali, kutoa ushirikiano na ofisi ya usajili wa hazina, pamoja na kutumia fursa hiyo kwa kutoa elimu na maoni kwa jamii.   Nae Msaj

UVCCM KUSINI PEMBA, SKULI ZA MTANGANI, MAUWANI ZAPANDA MITI

  ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@    WANAFUNZI wa skuli ya msingi ya Mtangani na wenzao wa skuli ya sekondari ya Mauwani, wilaya ya Mkoani Pemba, wametakiwa kushiriki kikamilifu katika  kupanda miti na kuyatunza mazingira, ili kuendeleza urithi wa kijani katika visiwa vya  Zanzibar.   Hayo yameelezwa Juni 4, 2024 na Mjumbe wa Baraza kuu Taifa la Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapindizi ‘UVCCM’ anaeshughulikia mkoa wa kusini Pemba, Amriya Seif Saleh, wakti alipokua akishiriki katika zoezi la upandaji miti, eneo la Mtangani na Mauwani, ikiwa ni kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya mazingira duniani.   Alisema kuwa, ipohaja kwa walimu kujitahidi katika suala la kuwaelimisha wanafunzi, juu ya umuhimu wakupanda miti, ili  kuyahifadhi na kuyatunza mazingira yao na taifa kwa ujumla.   "Niwaombe walimu, mujitahidi sana kuwapa elimu wanafunzi hawa, ili wajue nini lengo hasa la upandaji wa miti na kuhifadhi mazingira, waweze kunufaika katika maisha yao ya kila siku",aliel

WAZAZI CHANZO KUZIMA NDOTO ZA WASICHANA KUWA WANAMICHEZO

  NA NIHIFADHI ABDULLA, ZANZIBAR@@@@ “SIKUJUA kinachoendela nilimuona tu baba kavimba nikamsalimia hakutikia vizuri mimi nikaingia ndani kukoga na mambo mengine”   Amesimulia   Wafaa akiwa kwenye upenu wa Nyumba na kuwacha kumlisha mtoto kwa muda wa sekunde 5 huku akionesha     huzuni usoni mwake. Jina lake halisi Wafaa Makame Hassan miaka 26 anakumbuka yaliyomtokea na namna alivyokatishwa ndoto za kuwa mwanamichezo miaka 12 iliyopita wakati anasoma skuli ya Muyuni iliyopo Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja. Amesema alikuwa na ndoto za kuwa mchezaji mkubwa wa mpira wa Nyavu ( Net Ball ) na tayari ali sha anza mashindano ya Skuli kwa skuli ya Elimu bila ya malipo. Ameendelea kusema baada ya kupumzika alipata habari kutoka kwa Shangazi yake ambae kwa sasa ameshatangulia mbele ya haki   kwamba baba yake kapiga marufuku kwenda kwenye michezo kwa madai kufanyika   uhuni. “Kuna mtu kampigia simu baba yako kuwa mnachanganyika na wanaume na kushikana hivyo amekasirika na laz