Skip to main content

Posts

Showing posts from January 22, 2023

TAMWA-ZNZ YAENDELEA KUWAONESHA NJIA WANAHABARI WACHANGA

  Na Muhammed Khamis,TAMWA-ZNZ   CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA - Zanzibar  kimesema  ili wanawakwe wengi zaidi waweze kushika nafasi za uongozi waandishi wa habari wanawajibu wa kuripoti  habari zitakazowaibua wanawake katika shughuli mbali mbali  zitakazowawezesha wanawake  kushika nafasi hizo.   Kauli hiyo umetolewa na Mkurugenzi wa Chama hicho Dkt,Mzuri Issa alipokua akizungumza na baadhi ya waandishi wa habari vijana kutoka Unguja na Pemba ambao wanaendelea kupatiwa mafunzo maalumu ya kujengewa uwezo juu ya kuripoti habari za wanawake kushika nafasi za uongozi sambamba na kuchochea uwajibikaji kwa maslahi ya Umma.   Alisema kwa muda mrefu wanawake wengi wamekua wakishindwa kufikia malengo ya kushika nafasi za uongozi katika ngalizi mbalimbali kutokana na dhana potofu  ya kuamini wanaume pekee ndio wanapaswa kuwa viongozi jambo ambalo linapingwa na mikataba yote ya kikanda na kimataifa.   ‘’Nyinyi waandishi wa habari vijana muna nafasi kubwa kuibadili hali hi

MRATIBU BARAZA LA WATU WENYE ULEMAVU PEMBA: AWAPA NENO WANAKIKUNDI PANDANI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: WANAKIKUNDI cha watu wenye ulemavu, kiitwacho ‘USHAURI’ kilichopo shehia ya Pandani wilaya ya Wete Pemba, wanaojishughulisha na kilimo cha njugu, wameshauriwa kujitenga mbali na migogoro, kwani ndio sumu inayoweza kuwagawa na kurudi tena, kwenye umaskini. Ushauri huo umetolewa leo Januari 26, 2023 na Mratibu wa Baraza la Taifa la watu wenye ulemavu Zanzibar ofisi ya Pemba, Mashavu Juma Mabrouk, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kumaliza ziara maalum, ya kukitembelea kikundi hicho. Alisema, vikundi vingi huanzishwa kwa furaha na malengo, mikakati mikubwa, lakini mwisho wa siku wanachama hufarakana kwa kuingia kwenye migogoro. Alieleza kuwa, suala la migogoro ni jambo lisiloepukika, lakini suala la kuitatua ni jambo la lazima, ili kutimiza ndoto na azma ya kuanzisha umoja wao. ‘’Niwatake wenzetu hawa wenye ulemavu kuwa, kikundi chao hichi kisijekikaparaganyika, kwa kule kuikaribisha migogoro, kwani, mnaweza kurudi tena kwen

TAMWA-ZANZIBAR, WAANDISHI WAZIJADILI SHERIA ZENYE MAPUNGUFU KATIKA KUPINGA UDHALILISHAJI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:: MRATIBU wa Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, amesema sheria zenye mapungufu katika mapambano dhidi ya ukatili na udhalilishaji, ni changamoto nyingine inayohitaji kufanyiwa kazi. Alisema kwa mfano, sheria Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, kwenye vifungu vyake vya 108 na 109 vilipotaja kosa la ubakaji na dhabu, hakuna adhabu sawa kwa washitakiwa wa kosa la aina moja. Mratibu huyo aliyasema hayo Januari 24, mwaka 2023 ofisi ya TAMWA Chake chake Pemba, wakati akiyafunga mafunzo ya siku mbili, kwa waandishi wa habari, kwenye mradi wa Kuhamasisha hatua za kitaifa, dhidi ya kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji, unaoendeshwa na tasisi za TAMWA, KUKHAWA, TUJIPE, ZAFELA na ZAMWASO. Alisema, bado sheria zinaendelea kuwaweka njia panda wananchi, kwa kule washtakiwa wa makosa ya ubakaji, kupewa adhabu tofauti, na sio iliyotajwa kwenye sheria husika. ‘’Kwa mfano, wapo wanaotiwa hatiani kwa ubak

SHEHA WAWI: 'TUTASHIRIKIANA NA MSAIDIZI WA SHERIA WETU'

  NA AMINA AMHED, PEMBA UONGOZI wa  Shehia ya Wawi Jimbo la Wawi wilaya ya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba,  umesema utatoa kila aina ya ushirikiano  na msaidizi wao mpya wa sheria, katika kutatua changamoto mbali mbali za jamii zikiwemo matukio ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia, ambazo kwa muda mrefu zilikuwa zikikosa ufumbuzi, kwa kutokuwepo msaidizi wa sheria makini.  Hayo yalielezwa Januari 22, 2023 na Sheha wa Shehia ya Wawi Sharifa Ramadhan Abdalla, alipokuwa akifungua mkutano maalum wa kutoa Elimu  kwa wajumbe wa sheha wa shehia hiyo, kutoka kwa Msaidizi moya wa sheria Kutoka Jumuia ya Wasaidizi wa Sheria wilaya ya Chake Chake Pemba 'CHAPO'.   Alisema anaamini kuwa Idara ya Katiba na Masaada wa Kisheria kumuwezesha Msaidizi huyo wa sheria, haikukosea, kwani amemuwa mtendaji mzuri na mfuatuliaji hata kabal ya kupata mafuanzo ya awali ya sheria na sasa kuijiunga na CHAPO  na kuwa katika shehi hayo. Alisema kwa anavyomfahamu Msaidizi huyo wa sheria, naamini zile chha

TAMWA-ZANZIBAR: VYOMBO VYA HABARI BADO NI JUKWAA PEKEE LA MABADILIKO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:: MKURUGENZI Mtendaji wa Chama Cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, amesema, bado vyombo vya habari vitaendelea kuwa tegemeo kwa jamii, katika kuwabadilisha kutoka mtazamo finyu na kwenda wenye tija. Dk. Mzuru aliyasema hayo leo Januari 23, 2023 wakati akifungua mafunzo pacha, kati ya waandishi wa habari wa Unguja na Pemba, kwa njia ya kielektronik, kwenye mafunzoi ya siku mbili, chini ya mradi wa Kuhamasisha hatua za kitaifa dhidi ya kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji, unaoendeshwa na tasisi zaTAMWA, KUKHAWA, TUJIPE, ZAFELA na ZAMWASO. Alisema, vyombo vya habari ni jukwaa muhimu na limeshafanya magauzi kadhaa, ikiwa ni pamoja na kusababisha kupatikana kwa sheria mbali mbali zikiwemo za kupinga udhalilishaji na adhabu zake. Alieleza kuwa, ndio maana TAMWA katika kutekeleza kazi zote, lazima kuwashirikisha waandishi wa habari, ili kuhakikisha wanachotaka kukifanya, iwe rahisi kupata matokeo. ‘’Bado vyom

SMZ KUJENGA MJI WA KISASA WA SERIKALI

                                           Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar Dkt Mngereza Mzee Miraji amesema wizara yake imeshakamilisha ramani ya   mji wa Serikali kiutendaji kwa awamu ya kwanza ambapo maeneo sita yameshaainishwa kwaajili ya kujenga mji huo. Akizungumza   mara baada ya kumaliza kikao baina ya wizara yake na Taasisi ya Rais ufuatiliaji na Usimamizi wa utendaji Serikalini (PDB), kilichofanyika mwisho wa wiki katika hoteli ya Golden Tulip Kiembesamaki, Unguja, alisema ramani ya Mji wa Serikali imekamilika   na muda sio mrefu Serikali itaamua wapi ujengwe mji huo. Dkt Mngereza aliyataja baadhi ya maeneo ambayo wizara yake imependekeza kujenga mji wa Serikali ikiwemo, Fumba, Kisakasaka, Dunga na Tunguu ambapo maeneo hayo kwa unguja yameonekana yanafaa kujengwa Mji wa Serikali kutokana vigezo vinavyohitajika katika Mji wa Serikali. “Ni kweli mwezi mmoja   uliyopita tuliwaita watendaji wa wizara zote za Serikali tuliwaita wizarani watupe