Skip to main content

Posts

Showing posts from May 15, 2022

AMINA SHAABAN: MLENGWA WA TASAF PEMBA ANAYEUSHANGAAZA UMMA

  NA HAJI NASSOR,  PEMBA “KABLA ya kuja kwa mpango wa kunusuru kaya maskini, hali yangu ya maisha ilikuwa ya kubahatisha hasa kujipatia mlo walau wa siku, ilikua kazi,’’ Ni maneno ya mwanzo ya mlengwa huyo wa TASAF, Amina Shaaban Shamte, alipokuwa akizungumza nami, kwenye eno lake la malisho ya wanyama kijijini kwake Mgogoni wilaya ya Wete Pemba. Amina kabla ya kutuliwa na TASAF mikononi mwake, ilikuwa jambo la kawaida, kutimiza siku tatu bila ya mlo hata ule wa kumuwezesha kuishi.   “Kwanza niwashukuru viongozi ambao walileta huu mpango wa kaya maskini, mfumo huu umekuwa ni mkombozi mkubwa     kwetu sisi ambao tuna hali ngumu za maisha”, anasema. Bi Amina anasema, kabla ya kuja kwa mpango huo wa kunusuru kaya maskini, hakuwa na shughuli yoyote ya kujipatia kipato lakini baada ya kufikiwa na TASAF aliweza kujishuhulisha na biashara ya kuuza nazi na ndio safari yake ya kuona mwanga ilianzia. Katika kipindi hicho ambacho TASAF haijamfikia, watoto wake kwenye suala la kuso

MALAWITI ATUPWA CHUO CHA MAFUNZO MIAKA 14 PEMBA

  NA HASSAN MSELLEM, PEMBA MAHKAMA ya Mkoa Chake Chake, imemuhukumu kutumikia Chuo Cha Mafunzo kwa muda wa miaka 14, mshitakiwa  Omar Songoro Hamad mwenye miaka 38 mkaazi wa Vikunguni wilaya ya Chake chake, baada ya kupatikana na kosa la kumlawiti mtoto menye miaka 11. Hukumu hiyo imetolewa jana Mei 18, mwaka 2022 na hakim Muumin Ali Juma wa mahakama ya maalum ya makosa udhalilishaji katika Mahakama ya mkoa Chake Chake. Awali ilitajwa mahakamani hapo na Mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka ofiai ya Mkurugenzi wa Mashtaka Mohamed Said Mohamed kuwa, mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo siku na tarehe isiyofahamika majira ya 1:30 usiku. Ambapo alitenda kosa hilo, eneo la Vikunguni Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, akijua kuwa analofanya ni kosa. Mashahidi wa nne wa upande wa mashtaka waliwasilishwa mahakamani hapo, akiwemo mtoto mwenyewe,  mamzazi wa mtoto, Askari wa ,mpelelezi pamoja Daktari ambapo amekiri kuwa mtoto huyo alifanyiwa ulawiti. Hakukuwa na mashahidi kwa upande wa ms

DAKTARI ANAYEDAIWA KUMBAKA MTOTO MARA TATU PEMBA AANZA MAISHA YA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MAHAKAMA ya Mkoa Wete, imelazimika kumlaza rumande kwa muda wa wiki mbili, daktari Is-haka Rashid Hadid, akidaiwa kutenda makosa manne kwa mtoto mmoja mwenye miaka 16, likiwemo la kumbaka mara tatu. Akisoma hati ya mashtaka, Mwendesha Mashtaka kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Juma Mussa , alidai kuwa, mtuhumiwa huyo alimbaka mtoto huyo ambae yuko chini ya uangalizi wa wazazi wake. Alidai kuwa, baina ya Aprili 21, mwaka huu mtuhumiwa huyo alimtorosha mtoto huyo, kutoka nyumbani kwao Gombani wilaya ya Chake chake mkoa wa kusini Pemba na kumpeleka nyumbani kwake Kangagani wilaya ya Wete. Ambapo baada ya kumtorosha, usiku wake alianza kumbaka na kuendelea kumfanyia kitendo hicho kwa siku tatu tofauti. ‘’Mtuhumiwa umetenda makosa manne, kwa mtoto mwenye miaka 16, moja ni kumtorosha na pili ulimbaka mara tatu, wakati ukiwa nyumbani kwako, eneo la Kangagani wilaya ya Wete mkoa wa kaskazini Pemba,’’alidai. Mara baada ya kusomewa mashtaka yake, mtuhumi

MCT LATANGAAZA MAJINA WASHINDI TUZO ZA WANAHABARI: ZANZIBAR LEO PEMBA WAUPIGA MWINGI

  TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI   Dar es Salaam, Alhamisi, Mei 19, 2022 Jopo la majaji saba lililokaa kwa siku tisa, kuanzia Mei 7 hadi 15, 2022 kupitia jumla ya kazi 598 za waandishi zilizokuwa katika makundi 20 ya kushindaniwa katika Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) 2021, limemaliza kazi yake, Mei 15, 2022.   Jopo hilo lilitumia siku tisa badala ya nane kutokana na ongezeko la kazi 202 kutoka Tuzo za EJAT 2020, ambapo jumla ya kazi 396 ziliwasilishwa ukilinganisha na kazi 598 za sasa. Hapa niwapongeze na kuwashukuru majaji kwa kazi kubwa waliyoifanya usiku na mchana yakupitia kazi hizo.   Jopo liliongozwa na mwenyekiti, Mkumbwa Ally. Wajumbe wengine walikuwa Mwanzo Millinga (Katibu), Aboubakar Famau, Mbaraka Islam, Imane Duwe, Beatrice Bandawe, na Rose Haji, ambao waliapishwa Mei 6, 2022 na Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Baraza la Habari Tanzania (MCT), Jaji Robert Makaramba.   Majaji hao wameteua jumla ya waandishi 60 ambao kazi zao zimeoneka