Skip to main content

Posts

Showing posts from March 24, 2024

MEYA JIJI LA CHAKE CHAKE: 'NJOONI MJIFUNZE KWA 'GOMBANI FITNESS CLUB'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MEYA wa jiji la Chake chake Hamad Abdalla Hamad, amevitaka vilabu vyingine vya mazoezi kisiwani Pemba, kuiga mfano unaofanywa na wenzao wa ‘Gombani Fitness club’ kwa kule kuwa karibu na jamii. Hayo aliyasema leo Machi 30, 2024 mara baada ya kumalizika kwa futari, iliyoandaliwa na klabu hiyo, iliyojumuisha wawakilishi wa vikundi vya mazoezi vya Pemba, watoto mayatima na waumini wengine na dini ya kiislamu na kufanyika ukumbi wa ZRA Gombani. Alisema, Gombani Fitness Club, imekuwa karibu mno na jamii, kwa kule kujumuika katika shughuli za umma kama za usafi, uchangiaji damu na futari ya kila mwaka. Alieleza kuwa, klabu hiyo haipo tu kwa ajili yakufanya mazoezi pekee, kama vilivyo vilabu vyingine, bali wanakwenda mbali zaidi, kwa kuwa karibu na jamii kivitendo. ‘’Mfano huu wa futari mlioiandaa, kuchangia kwenu damu kwenye shughuli mbali mbali za umma, kushiriki usafi ni mambo ya kuigwa na vilabu vyingine,’’alieleza. Aidha alieleza kuwa, ibada walioif

MANENO 'SHINANI, SHIMONI' YAWAWEKA HURU WALIODAIWA KUKUTWA NA BANGI PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHAKAMA kuu Zanzibar kanda ya Pemba, imewaachia huru Akida Mbega Bakari (33) na Rashid Rajab Ngoji (32), waliyokuwa wakikabiliwa na tuhma za kupatikana na misokoto 340 ya iliyodhaniwa kua ni bhangi, baada ya ushahidi uliotolewa, kutowaunganisha na makosa yao. Aliyeaachia huru watuhumiwa hao ni Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim wa Mahakama hiyo, ambapo alitoa uamuzi huo, baada ya kusema ushahidi uliotolewa mahakamani hapo, kwenda kinyume na hati ya mashitaka.   Alisema, pamoja na upande wa mashitaka kuwasilisha mashahidi saba mahakamani hapo, lakini ushahidi wao umeshindwa kuthibitisha kwamba, kosa hilo lilifanyika sehemu ambayo hati ya mashitaka ya washitakiwa imeitaja. Alisema ushahidi uliotolewa na mashahidi wote saba, kutoka upande wa mashitaka, unaonyesha kwamba washitakiwa walitenda kosa hilo eneo la Machomane Shimoni, ambapo hati ya mashitaka inaonyesha kwamba, walitenda kosa hilo Machomane Shinani. Jaji Ibrahim alisema kuwa, hivyo sehemu iliyotaj

UTAFITI: WATANZANIA WAUNGA MKONO KUPUNGUZA UZALISHAJI GESI METHANE KUSHUGHULIKIA MABADILIKO HALI YA HEWA

  NA MWANDISHI WETU, Watanzania wameonekana kuunga mkono kwa kiasi kikubwa mipango inayolenga kupunguza uzalishaji wa gesi ya methane na kushughulikia mabadiliko ya hali ya hewa. Hii ni kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Global Methane Hub, shirika la kibinadamu linalojitolea kupunguza uzalishaji wa methane duniani. Utafiti huo, ambao ulijumuisha nchi 17 katika mabara sita, umetoa ufahamu wa jinsi jamii inavyoiona hali ya mazingira na njia za kisheria za kurekebisha hali hiyo. Matokeo ya utafiti huo yanaonesha kwamba asilimia 83 ya washiriki kutoka Tanzania wanapendelea sera zinazolenga kupunguza uzalishaji hatari wa methane, na kati yao, asilimia 49 wanatoa uungaji mkono mkubwa, kiwango ambacho ni cha juu zaidi kuliko nchi nyingine zilizofanyiwa utafiti. Zaidi ya hayo, asilimia 87 ya Watanzania wanaamini kwamba shughuli za binadamu ndio sababu kuu ya mabadiliko ya hali ya hewa, ikionesha ufahamu mkubwa wa umuhimu wa kuchukua hatua za kupunguza athari hizo. Utafiti huo pia unaones

MKUTANO WA MDIPAO, WAZAA MRADI WA MAJI SAFI NA SALAMA MKOANI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘’TUNA mwaka mmoja sasa, shida ya maji sisi wananchi wa kijiji cha Kinyasini wilaya ya Mkoani, tunaisikia kwenye vyombo vya habari,’’wanasema wananchi hao. Nilipotaka kujua kulikoni, wananchi hawa wanaishi kwenye vivuli vya raha na burudani, hasa kupitia haki ya msingi ya huduma ya maji safi na salama, hawakuwa wachoyo kusema ukweli. Rukia Ramadhan Bakari, akizungumza kwa shauku anasema, mkutano uliofanyika mwezi Febuari 2023, ulioitwisha na wasaidizi wa sheria wa wilaya ya Mkoani, ndio chanzo kikuu cha kuzaliwa kwa mradi huo. Mkutano huo pamoja mambo mingine ya kisheria, wananchi na hasa wanawake, walielezea changamoto yao ya ukosefu wa uhakika wa huduma ya maji safi na salama. ‘’Tulielezea changamoto yetu ya ukosefu wa huduma hiyo, mbele ya wasaidizi wa sheria, na wao walituahidi kwamba changamoto hiyo wataifuatilia,’’anakumbushia. Baada ya kimnya kirefu cha wiki tatu, waliitwa tena kupewa mrejesho na wasaidizi hao wa sheria, ingawa anasema

HATA HILI LA KUWASINDIKIZA WENZA KLINIKI WANAUME WANASUBIRI WATUNGIWE SHERIA?

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ INGAWA kwa karne moja iliyopita, suala la wanaume kuhimizwa kuwasindikiza wenzao wao kliniki, halikuwa likisikika, na inawezekana ni kwa sababu ya afya zilivyokuwa za wajawazito hao. Maana tunaelezwa na kusifiwa kuwa, wajawazito wa enzi hizo za mababu na mabibi, walikuwa ‘fiti’ afya zao, hali iliyopelekea, hata siku moja kabla ya kujifungua, alikuwa anakwenda shambani kulima. Na ukweli unabakia pale pale kuwa, hata kwa wakati huo vyakula vyenye siha, rutba, damu na kuongeza nguvu kwa wajawazito, vilikuwa bwerere. Kwa miaka hii ya sasa, afya za wajawazito walio wengi na hasa ikiwemo ukosefu wa damu, ndio habari ya mjini, na ndio maana sasa wanaume wakatakiwa wawasindikize wenzao wao, kliniki. Tena, kwani ni kila siku, hapana walau kwa wiki ya kwanza ya kuripoti kliniki, ili sasa zile changamoto anazokabiliana nazo, na yule mwenza apate kuzijua, ingawa wapo waliowasugu. Hapa wacha niwaulize wale wasugu wa kusindikiza wenzao wao, hilo kwao ni zito,

TANZANIA YATEKELEZA AHADI YA BEIJING

  Na Salma Lusangi ,New York @@@@ Licha ya changamoto za kiuchumi Duniani, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweza kutekeleza hatua mbali mbali zilizolengwa ili kupunguza athari kwa wanawake, na kuimarisha dhamira ya Utekelezaji wa Jukwaa la Beijing na ahadi ya Kizazi chenye  Usawa. Kauli hiyo imetolewa katika mkutano wa Hadhi ya Wanawake (CSW68) uliyofanyika wiki iliyopita katika ukumbi wa Umoja wa Mataifa New York Nchini Marekani na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Riziki Pembe Juma wakati akitoa taarifa ya utekelezaji  masaula ya wanawake na wasichana nchini Tanzania. Amesema hivi karibuni Tanzania ilizindua Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Jinsia na Wanawake (2023) iliyopitiwa upya, ambayo pia inaangazia Bajeti inayozingatia Jinsia kama nyenzo muhimu ya kutathmini athari za kijinsia za sera ya uchumi mkuu na sera za fedha, kwa kutambua athari zake katika ukuaji wa uchumi, maendeleo ya rasilimali watu na ajira kwa usawa. Mhe, Riziki ame

KAMATI YA PIC YAIPONGEZA TANESCO KUWA WABUNIFU

  Na Mwandishi wetu, Mtwara@@@@ Kamati ya Kudumu ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma(PIC) imelipongeza shirika la umeme Tanzania –TANESCO kwakuwa wabunifu ili kuweza kuondoa changamoto ya umeme kukatika mara kwa mara kwa mikoa ya Lindi na Mtwara.  Baada ya ziara ya Rais kumalizika Septemba mwaka Jana shirika hilo lilichukua hatua za dharula kuleta mtambo wa kuzalisha megawati 20 mkoani hapa ukitokea ubungo ili kuweza kumaliza tatizo la umeme kukatika mara Kwa mara.  Akizungumza wakati wa ziara hiyo Mwenyekiti wa Kamati ya (PIC) Mh. Deus Sangu  amesema kuwa mtambo huo unaenda kuondoa tatizo la umeme kwa mikoa ya Lindi na Mtwara. Amesema kuwa mradi huo unauwezo wa kuzalisha megawati 20 ambapo mitambo ya zamani ikiwa na uwezo wa kuzalisha megawati 21. “Mradi huu umetekelezwa na Kampuni ya kizalendo ambayo imefanyakazi nzuri na kwa wakati ambapo walitakiwa kikabidhi Machi 30 lakini sassa wameanza majaribio ni vema wakandarasi wengine wakaiga uzalendo huu Mradi huu unaenda kuleta mapinduzi makub

WANAFUNZI 274 WA MINUNGWINI WASOMA CHINI YA MITI

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA WANAFUNZI 274 wa skuli ya msingi Minungwini wilaya ya Wete Pemba, wanaendelea kusoma chini ya miti baada ya vyumba vinne vya madarasa walivyokuwa wakitumia kuchimbuka na kuvuja kwa muda wa zaidi ya miezi sita sasa. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi wazazi na walezi wenye watoto skulini hapo walisema, wanafunzi hao wanaendelea kukosa mtiririko mzuri wa masomo kutokana na kutumia eneo hilo kwa siku za kiangazi pekee huku siku za mvua zikiwa ni changamoto. Wazazi hao walisema kuwa, kutokana na kuharibika kwa madarasa hayo wana hofu ya kuporomoka kwa elimu skulini hapo kutokana na changamoto ya wanafunzi hao kusoma chini ya miti. Mmoja kati ya wazazi hao Fatma Jaffar Faki alisema kuwa hali hiyo haimpi usingizi kutokana na watoto wao kutokuwa na mazingira rafiki ya kusomea. "Tunapenda watoto wetu wapate elimu bora lakini kwa hali hii ya kuwekwa chini ya miti ni mtihani kwa sababu wakati wa upepo ni hatari, kwani hata tawi linaweza kukatika

TUMIENI MATOKEO YA SENSA KUFANYA UTAFITI-BALOZI HAMZA

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA WALIMU na wanafunzi wa vyuo vikuu kisiwani Pemba wametakiwa kuyatumia matokeo ya sensa katika kufanya shughuli za utafiti, ili kuwarahisishia katika kazi zao za kimasomo na kufundishia. Akifungua kikao cha usambazaji wa matumizi ya matokeo ya viashiria vya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 kwa wanafunzi na walimu wa vyuo vikuu kisiwani hapa, Kamisaa wa Sensa Zanzibar Balozi Mohamed Haji Hamza alisema, takwimu za matokeo ya sensa zitawarahisishia kufanya utafiti wa haraka. Alisema kuwa, ni vyema sensa ikatumika kwa ajili ya kufanya utafiti wa baadae kutokana na matokeo yaliyopatikana, hivyo ipo haja kila wanapofanya utafiti kutumia takwimu hizo kwa maendeleo yao na taifa kwa ujumla. ‘’Sensa ina vitu vingi sana tunavyoweza kuvitumia katika mambo yetu mbali mbali, ikiwemo ya kiutafiti, hivyo tuzitumie takwimu hizi za sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 kwa ajili ya kazi zetu,’’ alisema Balozi huyo. Aidha aliwahamasisha walimu na wanafun

SUNGURA: 'WELEDI, UMAHIRI KADA YA HABARI NI NGUZO MUHIMU

  NA MWANDISHI MAALUM, MCT-ZAZNAIBAR@@@@ Waandishi wa habari wametakiwa kufuata kwa kina maadili ya waandishi wa habari ili kukuza weledi na umahiri wa kada ya habari na kuzifanya taasisi za kihabari ziweze kuaminika na kuleta mabadiliko chanya katika jamii. Akizungumza na wadau wa habari katika ziara yake iliyofanyika Zanzibar tarehe 23 na 24 Machi Katibu Mtendaji wa Baraza la Hbbari Tanzania MCT  Ernest Sungura amesema kuwa   katika kufuata maadili hayo pia suala la kuzingatia vyanzo anuai vya habari havina budi kupewa kipaumbele. “Mara nyingi waandishi wetu wamekuwa na maradhi ya chanzo kimoja cha habari hali hii inapaswa kubadilika ili habari zetu ziweze kuwa na mawanda mapana zaidi na vyanzo vingi na tofauti vya habari”, alisisitiza. Amesema kuwa nguvu ya vyombo vya habari haina budi kutumika katika kujenga jamii iliyo bora na hivyo sauti za watu hazina budi kupewa kipaumbele. “taasisi za habari na vyombo vya habari havina budi kubadilika ili sauti za makundi ya pembezon