NA MARYAM NASSOR, UNGUJA@@@ @ SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar, imesema mageuzi ya sera na sheria za habari nchini yaendane sambamba na kanuni na maadili ya vyombo vya habari. Akizungumza katika kongamano la madhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari, Katibu mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Fatma Hamad Rajab, akimuakilisha waziri wa wizara hiyo alisema hilo litafanikiwa. Alisema, Serikali ya awamu ya nane, inafanya juhudi kubwa ya kuweka mazingira rafiki kwa uhuru wa vyombo vya habari nchini, bila ya kuathiri uhuru wa mtu mwingine. Alieleza kuwa, hivyo wandishi wa habari wanatakiwa kufanya kazi zao kwa kuzingatia sheria, weledi na maadili, ili kunufaika na sekta hiyo. Nae Afisa sheria kutoka Tume ya Utangazaji Zanzibar Khadija Mabrouk Hassan, alisema rasimu ya sheria ya habari tayari inafanyiwa kazi kwa sasa na iko katika hatua za mwisho katika afisi ya Mwanasheria mkuu kwa hatua zaidi. Alisema, sheria zilizofanyiwa k