Skip to main content

Posts

Showing posts from August 30, 2026

SITI FAKI ALI WA WETE: Ndie Mwalimu Mkuu alieondosha ‘sifuri’ skuli ya Utaani

                                   ‘Aweka mikakati wanabaki daraja la kwanza na la pili tu. IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA "Nilipoteuliwa kuwa Mwalimu Mkuu, mwanzo nilipata hofu hasa pale nilipojiona, naenda kuongoza watu wenye kiwango cha elimu sawa na mimi,’’anasema.    Ni maneno ya Mwalimu Mkuu skuli ya Sekondari ya Wanawake Utaani Wete, Siti Faki Ali mkaazi wa Chasasa Wete.   Mwalimu huyo ambae alitokea skuli ya Chasasa akiwa Msaidizi Mwalimu Mkuu, alipata hofu mara ya kupokea barua ya kwenda kuiongoza skuli hiyo.   Anasema, kwa vile ameshakaa uongozi katika mambo mbalimbali ya kijamii na Serikali kwenye nafasi ndogo ndogo, ndipo alipoona kwamba na nafasi hiyo anaweza kuiongoza.   Mara baada ya kukabidhiwa madaraka, alianza kuweka mikakati, ikiwemo kuondosha zero kwa wanafunzi kuanzia kidato cha pili hadi cha...