Skip to main content

Posts

Showing posts from May 28, 2023

WAZAZI, WALEZI WAWAPA TANO WAALIMU CONNECTING, KAZI IENDELEE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAZAZI na walezi wenye watoto wao skuli ya sekondari ya Connecting Continent ya Mgogoni wilaya ya Chake chake, wamesema wameridhishwa na juhudi binafsi za waalimu, katika kuwafundisha wanafunzi skulini hapo. Wakizungumza kwenye mkutano maalum uliofanyika skulini hapo, wenye lengo la kupokea matokeo ya muhula wa kwanza, wazazi na walezi hao, walisema kutokana na ugumu wa wanafunzi ulivyo, wanaridhishwa na juhudi zao. Walisema, wengi wao wamekuwa wakikosa muda wa kuwauliza watoto wao juu ya maendeleo ya elimu, lakini waalimu hao, wamekuwa wakibuni mbinu za kuwaendeleza wanafunzi. Wazazi hao walieleza kuwa, kwa muhula huu kwanza, wameridhishwa na matokeo hayo, ambayo kwa yale ya darasa la 12, kama yengekuwa ndio ya mitihani ya taifa, kusingekuwa na mwanafunzi aliyefeli. Mmoja kati ya wazazi hao Omar Mjaka Ali, alisema kama sio juhudi za waalimu hao na mbinu mbali mbali za kuwalazimisha wanafunzi kusoma, matokeo ya muhula wa kwanza, yasingekuwa mazuri.

WADAU: ‘WAHANGA WA UDHALILISHAJI WALIPWE FIDIA ZAO

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA “NILIAMBIWA mahkamani kua, mtoto wangu atalipwa shilingi milioni 1 ya fidia, tangu mwaka jana, mshitakiwa alipotiwa hatiani, lakini sasa ni miaka miwili hajapewa, mpaka mshitakiwa alipoondolewa hukumu kwa madai ya ugonjwa wa akili,’’anasema mzazi mmoja. Mama huyo mkaazi wa Wingwi Wilaya ya Micheweni ambae mtoto wake wa miaka mitatu (3) alifanyiwa kitendo cha ubakaji na kijana wa miaka zaidi ya 28. Anaeleza kuwa, alitegemea fedha hizo zitamsaidia kumshughulikia mtoto wake ambae aliathirika kisaikologia na kimwili, ingawa hajaulizwa chochote tangu kesi hiyo ilipopata hukumu mwaka jana. “Kinachoniumiza zaidi ni kuona yule mshitakiwa alitakiwa kutumikia chuo cha mafunzo miaka 30, lakini haijatimia mwaka, ameshatolewa eti kwa madai kuwa ni mgonjwa wa akili, na amekwenda Unguja Mental”, anaeleza. Anasema kijana huyo hajawahi kumuona wala kusikia kwamba ana ugonjwa wa akili, isipokuwa wanafanya hivyo ili asifungwe wala alimlipe fidia. Mama huyo sio peke y

WANAWAKE WANAOZALISHA BIDHAA ZA CHAZA LULU MAKOMBENI WALA HASARA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAUSHIRIKA wa ‘tujikombowe’ wa shehia ya Mkombeni wilaya ya Mkoani Pemba, unaojisghulisha na ufugaji wa chaza lulu, wamepata hasara ya zaidi ya shilingi 600,000 baada ya bidhaa zitokanazo na rasilimali hiyo, kukosa wateja. Bidhaa hizo aina herini pea 25, ambazo moja ni shilingi 25,000 wamelazimika kuzibakisha ofisini kwao, baada ya kukosa wateja kwa muda mrefu sasa. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, walisema awali walikuwa na changamoto ya ukosefu wa mashine ya kusarifia bidhaa hizo, ingawa baada ya kuipata sasa changamoto ni soko la bidhaa hizo. Walisema, kwa mara ya kwanza walizalisha herini hizo na kuziuza kwa thamani ya shilingi 300,000 ingawa kwa msimu mwengine walikosa wateja wa bidhaa hizo. Mwenyekiti wa ushirika huo Faida Faki Kombo, alisema kwa sasa hawajui herini hizo pea 25 wazifanye nini bali wanachoshuhudia ni kuendelea kuchakaa na kupoteza thamani. Alieleza kuwa, soko la wateja wao kwa sasa limepotea na kusababisha kupata

SKULI MPYA YA GHOROFA MWAMBE, KUPUNGUZA UFINYU WA NAFASI KWA WANAFUNZI?

      NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ILIKUA kama ndoto, kwa siku ya kwanza kati ya zile 360 zinazounda mwaka, kwa waalimu, wanafunzi, wazazi, walezi wa Mwambe, kunawa uso mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi. Sio tu kunawa uso, kwa maji kama ilivyozeeleka, wao walinawa kwa kumalizika skuli ya msingi ya ghorofa mbili eneo hilo la Mwambe. Hapa wazazi, walezi, wanafunzi na waalimu, maji kwenye upindo wa kucha ya mtoto mchanga, yalitosha kuwakogesha mwili mzima. Furaha yao, sio tu kuamka wakiwa wazima siku hiyo ya Januari 1, mwaka 2023, lakini ni pale waliposhuhudia jengo la kwanza la ghorofa katika eneo la Mwambe, na bahati nzuri sio la mtu binafsi, bali likiwa la serikali. WANANCHI MWAMBE Haji Omar Kheir, anasema aliposikia ahadi ya rais wa sasa wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, juu ya ujenzi wa skuli ya ghorofa, hakuamini akilini mwake. ‘’Si unajua baadhi ya wanasiasa wakitaka jambo lao, watakuahidi jambo hata ambalo yeye h