Skip to main content

Posts

Showing posts from April 14, 2024

SHARON ROBERT: KIONGOZI ALIYEVUNJA UKIMNYA KUWASTIRI WANAFUNZI SKULINI ZANZIBAR

    NA NIHIFADHI ISSA, UNGUJA@@@@ NI kawaida kwa watoto wa kike wakifikia umri kuanzia miaka 10, kubaleghe na kutokanana na maumbile siku hizo huanzia  tatu (3) h adi saba (7). Kiutaratribu watoto hutakiwa kwenda skuli kuanzia siku 20 hadi 22 kwa mwezi mmoja   lakini watoto wa kike hususan walioko vijijini, huenda skuli siku 15 hii hutokana na kuingia kwenye kawaida yaao na kukosa taulo za kujisitiri. Zanzibar yenye watu wapatao milioni 1.8 huku idadi ya vijana ikiwa ni Zaidi ya 600,000  inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa elimu ya afya na hedhi salama kwa wanawake Sharon Robert akiwa Mkurugenzi wa taasisi ya 'holding   hands foundation' alifanya utafiti mwaka 2019 na kugundua kuwa, watoto wakike wanaoishi nje ya mji wanakosa kwenda skuli siku 84 kwa mwaka, katika ya siku 180 wanazotakiwa. Akiwa mwanamke na kiongozi kwenye taasisi yake Hii ilimfanya Sharon kuanzisha kampeni ya kukusanya taulo za kike na kuwapa wasichana bure maskulini. Sharon alianza ugawaji wa ta

TAKALA SIO SULUHISHO LA JINAMIZA LA NDOA

  NA MARYAM NASSOR, ZANZIBAR WATU wamekuwa wakiamini kuwa talaka ndiyo kimbilio, la matatizo yote yanayowakumba katika maisha ya ndoa . Katika   dini ya kiislamu, talaka iko kisheria, ingawa maadiko matakatifu na yasio na shaka, ni haramu ambayo Muumba ameichukia. Na wapo wanaoamini hata wakati wa kutolewa kwake ama kuandika, Imani inakubali kuwa, mbingu hutikisika, ishara kuwa si uamuzi sahihi sana. Ijapo kuwa, maana ya ndoa ni mkataba wa hiari   ambao hufungwa kwa makubaliana baina ya mume na mke, ingawa pale inapofika   kuwa ndoa hiyo haina misingi ya kuendelea tena, basi hupelekea kutoka kwa talaka. Mohamed Issa Ali mwanaharakati wa haki za watoto kisiwani Pemba, anashangaa kuona wanandoa hao kutowafikiria watoto ambao watawakosesha mapenzi na malezi ya wazazi wawili. Na huwa hamufikirii hata kwa dakika chache tu, kuwa   lile janga la vitendo   vya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia kwa watoto hao. Utakuwa na uhakika gani kuwa, ule ulezi wa pande moja siku hizi unai

WANANCHI WATAKIWA KUJUA MBINU ZA WAHALIFU, KUDHIBITI UHALIFU

 IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA @@@ WANANCHI wa shehia ya Pandani Wilaya ya Wete wametakiwa kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya mbinu zinazotumiwa na wahalifu, ili vijiji vyao viwe katika hali ya salama. Akizungumza wakati wa kampeni yake ya kupita nyumba kwa nyumba juu ya kutoa elimu ya kudhibiti uhalifu katika kijiji cha Mwembe Butu, Mkaguzi wa shehia hiyo Inspekta wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Khalfan Ali Ussi alisema, kila siku wahalifu huandaa mbinu mpya, hivyo wawe makini. Alisema kuwa, ni vyema jamii kuwapa ushirikiano kikosi cha ulinzi shirikishi ili wajue mbinu zinazotumiwa na wahalifu wanaotekeleza uhalifu wao na kuweza kuwadhibiti. "Kampeni hii ni ya Familia yangu Haina uhalifu, hivyo tunataka tuhakikishe jamii inaishi bila ya kuwepo uhalifu na ndio maana tunachukua juhudi ya kutoa elimu nyumba kwa nyumba," alisema Mkaguzi huyo. Aidha Mkaguzi huyo aliwataka wanafamilia kuendelea kusimamia maadili mema ya watoto wao ili kujenga familia yenye heshima