Skip to main content

Posts

Showing posts from April 2, 2023

DK: MNGEREZA AWAAINISHA WADAU WALIOFANIKISHA MPANGO UWEKEZAJI MAJI ZANZIBAR

  Na Muandishi wetu Zanzibar@@@@ Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi (WAMM) Mhandisi Dkt Mngereza Mzee Miraji amesema Mpango wa Uwekezaji katika Sekta ya Maji Zanzibar 2022-2027 wenye lengo la kuimarisha sekta ya maji na kumaliza tatizo la maji safi na salama Zanzibar alianzisha kwa kushirikiana na Wadau wa Maendeleo mbali mbali. Mhandisi Dkt Mngereza aliyasema hayo jana katika hafla iliyoandaliwa ya kumkabidhiwa Tuzo ya Kifahari ya VIP Global Water Change Maker, Mhe Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Husseini Mwinyi iliyofanyika jana Ikulu Zanzibar. Alisema katika kipindi ulichoteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Nishati na Madini alichukuwa juhudi mbali mbali za kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama, kwa kukutana na Mashirika ya Kimataifa ya Misaada ikiwemo JICA, USAID, BPI, Banks ikiwemo AFDB, wawakilishi wa balozi mbalimbali ikiwemo UK, EU, JAPAN n.k. Alielezea kwamba hivyo Wizara ya Maji, Nishati na Madini (WMNM) na

ZUPCSA, YATAKA UAJIRI WALIMU WA SAIKOLOJIA SKULINI

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ JUMUIYA ya wanafunzi wa wa Saikolojia Chuo Kikuu Zanzibar (ZUPCSA) wameiomba Serikali kuajiri walimu wa saikolojia ambao watawasaidia wanafunzi na watoto waliofanyiwa udhalilishaji kuwapa ushauri nasaha. Walisema kuwa, wakati wanapita skuli kutoa elimu ya saikolojia, waligundua kuwa, kuna uhitaji mkubwa kwa walimu wa saikolojia, kwani waliopo ni wale tu waliopatiwa mafunzo ya muda mfupi, jambo ambalo halikidhi mahitaji ya kutoa elimu hiyo kwa wanafunzi. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Naibu Mwenyekiti wa Jumuiya ya wanasaikolojia Zanzibar na Mwenyekiti mstaafu wa jumuiya ya ZUPCSA ya ZU, Ramadhan Mohamed Hassan alisema kuwa, hali hiyo hupelekea umahiri wa kazi kuwa ni mdogo sana, kwa sababu kunakuwa na changamoto nyingi za kisaikolojia kwa wanafunzi. "Walimu waliopo ni wale waliopata mafunzo ya wiki mbili, hivyo inakuwa kazi hazifanyiki vizuri, kwa hiyo ni tunapendekeza waajiriwe walimu hasa waliosomea kada hiyo, ili kuondosha matati

SASA ARDHI YA ZANZIBAR KUSAJILIWA KWENYE MFUMO MAALUM

    Na Mwandishi wetu, Zanzibar Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi (WAMM) jana imesaini Hati ya Makubaliano na Kampuni ya Kitaifa ya Kijiografia na Misitu (IGN FI) ya Ufaransa kuhusu Mradi wa Taarifa za Usimamizi na Usaji wa Ardhi Zanzibar. Akizungumza mara baada ya hafla ya utiaji saini waziri dhamana wa wizara hiyo   Mhe. Rahma Kassim Ali amesema kufanya kazi kwa mfumo wa taarifa za Usimamizi na Usajili wa Ardhi utasaidia kwa kiasi kuondosha migogoro ya ardhi iliyokuwepo Zanzibar. Waziri Rahma aliyasema hayo baada ya kushuhudia hafla ya utiaji saini ambapo ilifanyika Wizara Ardhi na Maendeleo ya Makaazi, Maisara Unguja. Alisema hatua hiyo ya utiaji saini ina manufaa makubwa hasa katika kuondoa migogoro ya ardhi ambayo inaonekana kujitokeza kila siku.   “Tunaamini mfumo huo utasaidia sana kwani taarifa zitakuwa kwenye mfumo na mmiliki husika hasa wa ardhi atajulikana kwani taarifa za ardhi   zipo kwenye karatasi lakini mfumo sio rahisi kupoteza taarifa.” Alisema waziri

WANANCHI MSUKA PEMBA UZALENDO UMEWASHINDA, WATAKA UJENZI WA BARABARA YAO KWA KIWANGO CHA LAMI

        HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@ “HATUWEZI kwenda na kasi ya maendeleo, kwetu kutokana na uchakabu wa barabara,’’wanasema wananchi na watumiaji wa barabara ya Konde- Msuka. Wakaongeza kuwa, hata gari ya abiria hawana, shida kubwa hasa wanapotaka kwenda mjini kwa ajili ya kufuata matibabu. Wakizungumza na mwandishi wa makala haya, wananchi wa kijiji cha Msuka wilaya ya Micheweni mkoa wa kaskazini Pemba, wanasema hawajui ni lini watajengewa barabara hiyo. Kwa kuwa barabara huchangia pato kubwa katika maendeleo ya mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla, ndio maana wananchi hawa sasa wanataka kujengwa barabara ya kudumu. Kuna shughuli nyingi ambazo bila ya kuwepo miundombinu ya barabara haziwezi kufanyika ama kufanyika kwa wakati wake. Ingawa umuhimu wa barabara hauonekani kwa ghafla mpaka pale panapotokezea tatizo, ikiwemo wafanyabiashara, wanapotaka kuingiza ama kutoa bidhaa zao mbalimbali. Akina mama wanapotaka kufuatia huduma za afya katika hospitali kubwa ama za rufaa h

WANAWAKE PEMBA WAKERWA TABIA ZA WAENDESHA BODA BODA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ABIRIA wanawake kisiwani Pemba, wamelalamikia tabia ya baadhi ya madereva wa pikipiki ‘boda boda’ kuwaingia mwilini wakati wanapokuwepo kwenye vituo vyao, kutaka usafiri wa aina hiyo. Walisema mara unapofika kwenye eneo lao la vituo na kutaka usafiri, huvamiwa na kuanza kukukopea mizigo na wengine kuwashika mikono, wakivutiana kwenye chombo chake. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwenye eneo la Mtuhaliwa wilaya ya Mkoani Pemba, walisema wamekuwa wakisikitishwa na tabia hiyo. Mmoja kati ya wanawake hao aliyekataa jina lake lichapishwe alisema, baadhi ya waendesha boda boda hao, wamekua wakiwaingia mwilikini, kwa lengo la kufanya ushawishi. Alieleza kuwa, kinachowaudhi ni kule kuanza kupokea kuanzia mizigo mikubwa hadi vipochi vya mkononi, na wengine kukumata mikono. ‘’Ukiteremka gari tu, wanaaza kukuzonga, wengine wanakupokea hata vipochi vyenye simu, na wengine wanaanza kukushika shika mikono, wakitaka upande boda bado yake,’’alisema. K