NA MWANDISHI WETU, UNGUJA@@@@ W aziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Riziki Pembe Juma amewataka wananchi kujiunga katika michezo mbali mbali ili kuimarisha afya zao pamoja na kuepukana na maradhi yasiyoambukiza. Kauli hiyo ameitoa mwishoni mwa wiki iliyopita wakati wa uekaji jiwe la msingi katika Mradi wa ujenzi wa viwanja vya Michezo midogo midogo iitwayo "Michezo kwa Maendeleo (Sports for Development) katika viwanja vya Mwera Regeza Mwendo Wilaya ya Magharib A. Unguja. Waziri Pembe alifahamisha kwamba hata viongozi wa dini na wataalumu wa Sekta ya Afya wamekua mstari wa mbele katika kuihamasiha jamii kufanya mazoezi au kujiingiza katika michezo mbali mbali ambapo hatua hiyo itasaidia kuimarisha afya na kuijiepusha na maradhi yasiyoambukiza ikiwemo kansa, kisukari na shindikizo la damu. Aidha alisema pia michezo ni ajira na sehemu ya kukuza uchumi kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla hasa kwa vijana wa jinsia zote, kwani michezo inawasaidia kujiepusha na v...